CHADEMA yampigia magoti Dk. Slaa. Wamtaka arejee kwenye ukatibu mkuu, mwenyewe 'awatolea nje'

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,895
20,392
DSC00940.jpg


Wadau, amani iwe kwenu.

Kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, zimesambaa taarifa za CHADEMA kumuomba Dr Slaa kurejea chamani na kwenye nafasi yake ya Ukatibu Mkuu. Tafsiri ya ombi hilo la CHADEMA kwa Dr Slaa ni kwamba hawajapata mtu wa kuvaa viatu vya Dr Slaa ambavyo hakuna mwenye uwezo wa kuvivaa. Hapa maneno ya Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Tundu Lissu kuwa viatu vya Dr Slaa ni vikubwa na kwamba hakuna mwenye uwezo wa kuvivaa ndani ya CHADEMA yanapodhihiri.

Hata hivyo, sina hakika kama CHADEMA wametafakari kwa kina kabla ya kufanya maamuzi hayo. Sina hakika pia kuwa CHADEMA wameshughulikia kiini cha Dr Slaa kujiuzulu Ukatibu Mkuu na kutimkia Ughaibuni kabla hawajamuomba kurejea chamani. Kwa kujikumbusha tu ni kwamba, Dr Slaa aliamua kujiweka pembeni baada ya wenye chama kulazimisha kumteua Fisadi Lowasa kuwa mgombea Urais wa chama hicho na mwamvuli wa UKAWA. Hicho ndicho kiini cha Dr Slaa kujiweka pembeni. Hivyo kama CHADEMA wana dhamira ya dhati ya kurejea kwenye misingi yake, wanapaswa kwanza kudeal na chanzo na si kufunika kombe ili mwana haramu apite.

Aidha, wakati CHADEMA wakichukua hatua hiyo ya kumuomba Dr Slaa kurejea chamani, Fisadi Lowasa ambaye alisababisha Katibu Mkuu huyo kutimka, ametangaza kugombea tena nafasi ya Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa 2020. Hii maana yake ni kwamba, kama ilivyotokea 2015, ndivyo itakavyokuwa 2020. Mgombea ni yule yule na mazingira yaliyomkimbiza Dr Slaa ni yale yale.

Taarifa za chini chini zinasema kuwa Dr Slaa amekataa wito huo wa CHADEMA huku akihoji haya niliyoweka hapa JF kwa faida ya Watanzania wengi. Pia kuna nyeti nyingine kuwa huenda fisadi Lowasa anataka kuelekeza hasira zake kwa Dr Slaa ikiwa ni ule mkakati wake wa kuwashughulikia wale wote waliokwamisha ushindi wake. Hivyo kitendo cha viongozi waandamizi wa CHADEMA kumuomba Dr Slaa arejee chamani ni kama mtego kwa Dr huyo wa Theolojia ili akishafika tu chamani aangukie mikononi mwa wabaya wake ambao wamejipanga kisawasawa kumshughulikia kwa namna watakayoona inafaa.

Hapa sasa ninapokumbuka misemo kadhaa ya kiswahili. USITUKANE MAMBA KABLA HUJAVUKA MTO; USITUKANE WAKUNGA WAKATI UZAZI UNGALIPO; SIZITAKI MBICHI HIZI nk. Kejeli, dharau, matusi, vitisho na kila aina ya upuuzi ulioelekezwa kwa Dr Slaa na wafuasi, viongozi, wapenzi na makada wa CHADEMA na UKAWA sikutegemea kama wangekuwa na ujasiri wa kumuomba Dr Slaa kurejea chamani.
 
Mleta mada hakuwa ameandika chanzo cha habari yake, mchangiaji mmoja katuwekea gazeti la TAZAMA.

Nimeshangaa sana maana TAZAMA ndiyo nimelisikia leo, sijui ni gazeti la kitongoji gani hapa bara au ni la visiwani? Ujinga mtupu!
 
Mleta mada hakuwa ameandika chanzo cha habari yake, mchangiaji mmoja katuwekea gazeti la TAZAMA.

Nimeshangaa sana maana TAZAMA ndiyo nimelisikia leo, sijui ni gazeti la kitongoji gani hapa bara au ni la visiwani? Ujinga mtupu!
Haijalishi chanzo kimetoka gazeti gani. Muhimu hapa ni hoja iliyowasilishwa
 
Haijalishi chanzo kimetoka gazeti gani. Muhimu hapa ni hoja iliyowasilishwa
Gazeti la Tanzania Daima likiandika JK afanya mpango wa kujiunga na UPDP kumsapoti Dovutwa hapo kuna hoja ya kujadili? Utakuwa mpuuzi kama habari hiyo hutakiangalia chanzo chake.
Ndio maana kagazeti hako watu hawajihangaishi
 
Gazeti la Tanzania Daima likiandika JK afanya mpango wa kujiunga na UPDP kumsapoti Dovutwa hapo kuna hoja ya kujadili? Utakuwa mpuuzi kama habari hiyo hutakiangalia chanzo chake.
Ndio maana kagazeti hako watu hawajihangaishi
Kwa kawaida sitegemei chanzo kimoja ninapoandika habari yangu.
 
Ni kweli viatu vya Dr nivikubwa tukiangalia mtu wakuweka hapa bado Kazi hipo hila nafikiri busara itatumika hpa
 
Hahahahaha!! Unashusha nyuzi tu, kitu from Lumumba kimeitika chwaaap!

Na hii ilivyojibu faster itakuwa M-PESA
Hahahahahaaaaaaaa! Ni nini tena hiiiii? Fisadi Lowasa kawapoteza kabisa wapinzani
 
Ni kweli viatu vya Dr nivikubwa tukiangalia mtu wakuweka hapa bado Kazi hipo hila nafikiri busara itatumika hpa
Hakuna busara zaidi ya kukiri makosa, kumuomba radhi Dr Slaa na kujinyenyekeza kwake. Kubwa zaidi ni kumfukuza fisadi Lowasa ndani ya CHADEMA
 
Hahahahahaaaaaaaa! Ni nini tena hiiiii? Fisadi Lowasa kawapoteza kabisa wapinzani
Mshukuru JK kuwaombea awafikirie kidogo coz hali yenu ilikuwa mbaya sana. Mlishapotea kabisa hata maji ya kunywa ilikuwa ni shida.

Lkn kwanini Lowassa nae asiende Palestina kufanya usafi yaani mmemuona Mramba na Yona Tu.
 
Ndio mahana nimesema busara hitatumika hakuna ambae akisei nikweli tuliteza kumuondoa katika chama hila now anaweza kurudi
 
Nyie wafia chama ambao hamtambuliki makao makuu, mshapeleka taarifa zenu? jifunzeni kwa vijana wa Makamba
 
Ndio mahana nimesema busara hitatumika hakuna ambae akisei nikweli tuliteza kumuondoa katika chama hila now anaweza kurudi
Swali la kujiuliza, je CHADEMA mpo tayari kumfukuza Lowasa ili Dr Slaa arejee chamani?
 
Nyie wafia chama ambao hamtambuliki makao makuu, mshapeleka taarifa zenu? jifunzeni kwa vijana wa Makamba
Mkuu, mimi si mmoja wa makada maslahi. Nipo kwa ajili ya kukijenga chama. Sihitaji fadhila kutoka kwa yeyote
 
Mshukuru JK kuwaombea awafikirie kidogo coz hali yenu ilikuwa mbaya sana. Mlishapotea kabisa hata maji ya kunywa ilikuwa ni shida.

Lkn kwanini Lowassa nae asiende Palestina kufanya usafi yaani mmemuona Mramba na Yona Tu.
Lowasa atashtakiwa na kuhukumiwa na Mahakama ya Majizi na Mafisadi. Ukimpeleka kwenye hizi mahakama za kawaida ni kujisumbua tu
 
Back
Top Bottom