CHADEMA yambeba Odinga


IDU memorandum yake inasema wazi wazi kuwa ni muungano wa vyama vyenye kushabikia ukristo kitu ambacho ndicho Republican Party ya USA wanachofanya. Kwa hiyo kama CDM nao wanashabikia ukristo, basi inabidi waliseme hilo wazi na kuwa wanafuata matakwa ya IDU hata kama ni hatari kwa taifa.



Kwa hiyo chama cha Ahmedinajad wa Iran kikiwapa CCM mamilioni kwa ajili ya uchaguzi 2015, wewe huoni kuwa watakuwa wanaiingilia demokrasia yetu?
 
 

Si suala la kwamba ccm wamefanya ama hawajafanya, muhimu ni kuangalia kama ushirikiano huo una athari gani kwa chama chetu ama nchi yetu. Vyama vya siasa duniani kote vinashirikiana katika nyanja mbalimbali kadri ya mahitaji ya kila chama na nchi husika.

Lakini najua ninyi mliolishwa nyamafu na ccm huwa mkiona jambo limefanywa na Chadema hamuachi kutokwa na mapovu. Kila jambo linalofanywa na Chadema huwezi kulifananisha na jinsi ccm wanavyolifanya ama kutaka kuigeuza ccm kuwa ndio msahafu huo ni ufinyu wa fikra.

Na kuna mambo mengi ambayo yanafanywa na ccm si kwakuwa ni ccm bali kwakuwa ndivyo mfumo wa maisha ulivyo ama mfumo wa kijamii unavyotaka na si suala la ccm. Ukweli ni kwamba ccm hawajawahi kuasisi kitu chochote ambacho kimeweza kutumiwa kama mfano huko duniani kwahiyo jaribuni kupanua akili yenu kutooona kila kitu kwa miwani ya ccm.
 
Tunasubiri kuona CCM wakipiga kelele kuhusu hili na mwanasheria mkuu awafungulie mashitaka CHADEMA.
 
Kweli kabisa mkuu, tena baada ya hizo kampeni Komba akapewa zawadi ya shule. Kuna Shule hipo kule mbweni inaitwa Bakili Muluzi Sec. inamilikiwa na huyu komba...

sasa hili jamaa na njaa zake limeingia ccm ukubwani 2005 na kwanza kubwabwaja tu bila kujua hapo nyuma hilo chama lake mfu lishafanya hivo,. Iacheni chadema ifanye mambo yake kama haivunji sheria
 
Ni jambo la hatari sana chama cha siasa au hata mwanasiasa binafsi kutoka nchi "A" Kuingilia na kushiriki kwa namna yoyote ile kwenye masuala ya kisiasa ya nchi "B". Jambo hili nihatari bila kujali chama au mwanasiasa anayefanya mchezo huo.Kama CCM walikosea huko nyuma; basi hiyo haiwezi kuwa sababu ya msingi kwa CHADEMA kufanya kosa hilo hilo.
 
Kwa hiyo Islamic Coalition Party ya Iran ikiwatumia CCM helcopta 20 na pesa $100,000,000 ili washinde uchaguzi 2015 wewe utajisikiaje?


Wewe mbona ni mugumu sana kuelewa? kwa nini unashindwa kukubali baada ya kugundua kuwa uliweka hii post yako pasipokuwa na utafiti na watu wanaojua wameshakujibu kuwa hiki ni kitu ambacho kinakubalika kimataifa!

Wewe umebaki na na mambo ya uisilamu tu, hivi ni kwanini mifano yako yote inalenga huko? Au ndo udini unakusumbua mwenzetu!
Jibu ni kwamba kama CCM wana uhusiano na vyama hivyo basi wako huru kupokea lakini!
 
Mkuu ili Uhuru Kenyata aendelee kulinda mali za familia, fikilia athari za Kenyata kingdom kuporomoka!!!Thirty six thousand hekters of land, from coast Mombasa to Nakuru, to mention a few!!!!!
 
Tunashukuru kwa darasa, JF utajifunza mengi labda kama hutaki kujua!!!
 
Kama habari hii ni ya kweli, CDM wamefanya kitu cha kipuuzi na kipumbavu.
unashangaa?chadema ndo zao hizo,yaani wameshaweka mia kwa mia kuwa odinga anashinda.VIPI AKISHINDA UHURU?si ndio mambo ya aibu hayo.

Juzi hapa wanampa kawambwa siku 14,aache kazi au la kitawaka.siku zimeisha nasikilizia watafanyaje .
 
Mkuu na waziri Makufuli nasikia alikuwa huko akihamasisha wapiga kura, basi na yeye sasa amegeuka CHADEMA???
 
unashangaa?chadema ndo zao hizo,yaani wameshaweka mia kwa mia kuwa odinga anashinda.VIPI AKISHINDA UHURU?si ndio mambo ya aibu hayo.

Juzi hapa wanampa kawambwa siku 14,aache kazi au la kitawaka.siku zimeisha nasikilizia watafanyaje .
Wewe umefurahi watoto woote nchi nzima SIXTY % kufeli, kwa hiyo CHADEMA ni mazumbukuku??? Unataka waziri aendelee kutuletea matahira kwenye system ya nchi yetu, na kwa nini asijiudhuru????

 
Siku hizi ulinganishwaji wa mambo si mtu anafanya nini, na wala si siasa tena, zinalinganishwa dini, eti je Islamic coalition? Je Christian union? Utadhani kuna mahubiri ya injili au kusilimishana hapa, nakerwa si kidogo!!
 
kwahiyo mtu akitaja iran tu tayari amekua mdini?.

Kama hivyo ndo unavyofikiri,itabidi urudi standard one.
 
Wewe umefurahi watoto woote nchi nzima SIXTY % kufeli, kwa hiyo CHADEMA ni mazumbukuku??? Unataka waziri aendelee kutuletea matahira kwenye system ya nchi yetu, na kwa nini asijiudhuru????

kwahiyo hao kufeli kasababisha shukuru?kama ndiyo HOW?.
 

Taifa lipi hilo linalokubali kuingiliwa kwenye chaguzi zake?
 
Mnanikumbusha tulivyomsimika Rais wa Comoro.
Mbona tumesaidia kwa Kabila chini ya Banyamulenge tukamtoa Mobutu.
Mbona misaada ni Kawaida jamani.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…