Molemo bado hujanijibu swali langu kamanda,
mi sijapinga kuwepo mapingamizi,je kwa walivyopanga serekali yalipaswa kutolewa maamuzi lini?ili hata mgombea akilishinda pingamizi aweze kwenda kupigiwa kura???
Huu ni uhuni uliopitiliza yaani ukawa kwanini tusifungue kesi mahakamani kupiga hii rafu?
Mbona Jimbo la segerea Chadema wameshinda mitaa mingi lakini siskii chochote?
Ongera sana chadema na wanaukawa wote!!
Safiii xnaa chademaa
kama anakubalika ukonga si amwachie HECHE tarime na yeye awakongori magamba hapo dar?
Molemo?
Km ni post za CHADEMA muwe mnasema hili Jukwaa ni lenu maPro na BAVICHA
WW POST za ajabu ajabu tuziache zipite
Dr. Slaa ailipua Ikulu
mara tunaletewa
'MBOWE KUPOKEWA KWA MAANDAMANO DAR'
CHADEMA Yaizika CCM Ukonga
km habari ni ya kutunga pelekeni Buguruni lakini sio matusi maana habari haijakamilika lakini habari inakuja km kweli imekamilika
sasa hapo ndio CCM kazikwa ukonga? Heading zinatisha nyau kwanini nisiziite za kitoto?
Marire
Haya mambo yanazungumzika usihofu.Bahati njema Chadema ina hazina ya viongozi wenye hekima kubwa hususan majemadari wakuu Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa.
Hawa CCM wana mgogoro mkubwa huko Ukonga.Jerry Silaa na Eugene Mwaiposa wanaparurana kila mtu anataka agombee ubunge Ukonga.
Wananchi wanaona wote hawafai na wanapalilia matumbo yao tu kwa sababu wote wameshindwa kuwasaidia wananchi wa Ukonga kuepuka dhahama ya ubovu wa barabara.
Jerry Silaa ambaye ni Meya wa Ilala na mjumbe wa Kamati Kuu CCM kushindwa vibaya kwenye mtaa wake ni rasharasha tu..za masika zinakuja!
Bora ya wewe umegundua hizi habari za Mleta mada ni kujipiga Chapuo na maPro mengi tu ya CHADEMA
Hivi wameshinda mitaa mingapi mpaka waitane majina ya Kikamanda?
kumbe uchaguzi unarudiwa
kumbe wameshinda mitaa miwili tu?
kweli mahali akikutana Mchagga na Mkurya ni vigumu kutawalika
yetu macho
wakati ukifika atapima upepo mkuu. na ujue jimbo la Ukonga litagawika mwaka ujao. ngoja tusubiri muda ukifika tutafanya tathmini kamanda Waitara agombee Dar na Heche agombee Tarime ili tuwakamue vizuri magamba.
Mkuu Molemo huyu m/kiti aliyepigwa kimbunga na Kamanda Mwikabe alianza kuchonga hii barabara ya kivule sasa matokeo yalipotoka kasimamisha kuchonga i mean kasusa kumalizia! hebu ongea na Mwikabe afanye mchakato wa kumalizia ....
cc: Mwita Maranya
Operesheni ya Chadema ni Msingi na vuguvugu la Movement for Change jimboni Ukonga imeonekana kukisimika vyema chama hicho jimboni humo.
Wanachama wa Chadema jimboni Ukonga hawasiti kuupongeza uongozi wa jimbo hilo chini ya Mwenyekiti Thomas Nyahende maarufu kama Mwita Maranya kwa kazi kubwa waliyofanya tangu waingie madarakani.
Jimbo la Ukonga lenye ubovu mkubwa wa barabara limekuwa ngome kuu ya CCM kwa miaka mingi.
Hata hivyo katika uchaguzi uliofanyika wa Serikali za Mitaa wiki iliyopita Chadema wamejipatia ushindi mkubwa katika mitaa 10 huku washirika wao CUF chini ya mwavuli wa Ukawa wakijipatia mitaa 2.
Kikubwa zaidi ni kwa chama hicho kuweza kujipatia mitaa miwili muhimu.Mitaa hiyo ni ule anaokaa Meya wa Ilala Jerry Silaa wa Guluka Kwalala Gongolamboto na Mtaa wa Kivule unaoaminika kuwa na wakazi wengi zaidi kuliko mtaa wowote DSM.Kwa mfano katika mtaa huo wa Kivule mshindi alikuwa ni Afisa wa Chadema makao makuu Kamanda Mwita Mwikabe Waitara aliyepata ushindi wa kimbunga wa kura 1262 huku CCM wakiambulia kura 663
Kabla ya uchaguzi huu upinzani kwa ujumla walikuwa wanaongoza mitaa 2 tu kwa jimbo zima.
Jumapili wiki hii kutakuwa na marudio ya uchaguzi kwa mitaa 23 ambayo haikufanya uchaguzi wiki iliyopita.
Katika mahojiano na wanachama na baadhi ya viongozi wa misingi wamepongeza uongozi bora wa Mwita Maranya unaoshirikisha viongozi wote wa ngazi za chini na uwajibikaji uliotukuka.
Pia wanachama wameutaka uongozi wa Jimbo kutokubweteka kwa matokeo haya mazuri bali waendelee kukijenga chama bila kuchoka ili mwakani waweze kupata mbunge na madiwani wengi kwa lengo la kuongoza Manispaa ili walau wasimamie fedha za wananchi na hatimaye barabara za Ukonga zijengwe.
Acha uongo mkuu yani mnajitekenya na kucheka wenyewe ebu tuambie jimbo la ukonga lina mitaa mingapi na nyie Chadema na Ukawa mmepata mitaa mingapi kwa ujumla wenu na utuambie CCM imechukua mitaa ipi ni vizuri ukataja kata zilizopo na mitaa yake kwa jimbo la ukonga fanya hivyo tutakuelewa vinginevyo mnajidanganya kwa kujitekenya na kucheka wenyewe
Hapo sasa tuko pamoja Kamanda.
Chadema wameshapanga kutumia jopo la wanasheria wake kupigania demokrasia mahakamani.
Kwa mfano tayari Chadema tumefungua kesi kule Shinyanga kwa sababu wagombea zaidi ya 2000 walienguliwa kule Meatu kwa hila za CCM na hivyo wagombea wote wa CCM wakatangazwa washindi.
Mahakama gani? Hii iliyopewa milion 800 na Rugamalila, ama nyingine. Labda UKAWA ianze lampaini nyingie kali ya watumishi kama majaji wa mahakama za wilaya, mikoa ili wawe neutral maana hata hizo za Ruge haziwafikii. Kuna haja ya kazi kubwa kuelemisha watumishi wa umma polisi,jeshi, mahakimu, waalimu nk wasaidie vita hii ya operationn delete CCM