CHADEMA yaisambaratisha CCM Ngorongoro

CHADEMA yaisambaratisha CCM Ngorongoro

kweli vijijin wameamka dar ni kama mji wa sirte libya tutaukomboa kwa nguvu tena 2014
 
Magamba hayo lazima yavuke. Vijitu 800 katika wilaya ya watu millioni 4 ni kama ushuzi wa ngomani, upo lakini haunusiki.!

Tanzania bara ina zaidi ya wilaya 100, kama kwa upeo wako wilaya inaweza ikawa na watu milioni 4, basi sensa ijayo tanzania tutakuwa zaidi ya milioni 400, pole sana ! hii ni aibu yaani umeshindwa kuelewa jambo dogo hili ! on average wilaya nyingi za tanzania ni watu 400,000 hapo ni watu wazima na watoto wakiwemo, na idadi ya watu wazima ni wachache kuliko watoto, kwahiyo watu 800 ni wengi mno
 
mwenye imani kuwa ccm bado ina wafuasi ni nape na mkama.............hata kikwete anajua ccm saaizi haina mwanachama hata mmoja...waliopo ni kwa ajili ya kuendelea kukwapua mihela kwa njia za kifisadi,,.....
 
sasa mnataka nape afanye nini kwa wakati huu hata yeye anaona chama kinavyo poromoka na mbaya zaidi hawezi kuzuia hayo maporomokokwani yanakuja na majabali makubwa sana yana bomoa vizingiti vyote vilivyopo inabidi atazame tu na kubaki ofisini la sivyo yatamsomba nayeye.
Nape kama publicity master anatakiwa angalau abuni operations zitakazorudisha matumaini. Unajua watu sasa wameelimika zamani ilitosha kutoa tamko toka Lumumba kwenye RTD na watu wakafuata siku hizi ni tofauti kabisa. Mfano kama CDM wameanzisha M4C wao CCM wanaweza kubuni Operation Mapinduzi Daima OMD ni mfano tu wakaipeleka mikoani, sijui wanashindwa nini wakati funds kwao si tatizo.
 
Magamba hayo lazima yavuke. Vijitu 800 katika wilaya ya watu millioni 4 ni kama ushuzi wa ngomani, upo lakini haunusiki.!
jaribu kushilikisha ubongo wako na siyo hayo makamsi na usijaribu kuwafanja wana JF wajinga eti wilaya ya watu milioni 4, hizi takwimu za mwaka gani.....
 
CHADEMA kimevunjavunja ngome ya CCM wilaya ya Ngorongoro ambapo wanachama 800 wa CCM walijitoa katika chama hicho na kujiunga na CDM.

Tulikuwa njiani kuwafukuza uanachama - Nnauye Jr
 
Last edited by a moderator:
jamani mwendeni muleba watu wanamwamuko lakini hawana kiongozi
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kimevunjavunja ngome ya CCM wilaya ya Ngorongoro ambapo wanachama 800 wa CCM walijitoa katika chama hicho na kujiunga na CDM.

Tukio hilo kubwa lilitokea juzi baada ya Mbunge wa Karatu Mchungaji Israel Natse kufanya mkutano mkubwa wa hadhara wilayani hapo na kutoa somo kubwa la uraia kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Akikabidhi kadi mpya kwa wanachama hao Mchungaji Natse aliwataka wakazi hao kuwa mabalozi wa
CHADEMA katika maeneo ya vijijini wanakotoka na kuwaambia sasa hivi hakuna kulala mpaka CHADEMA itakapokamata dola mwaka 2015.

Baadhi ya wanachama wa
CHADEMA walimweleza Mchungaji Natse kuwa wamekuwa wakipata vitisho kutoka kwa viongozi wa serikali wilayani hapo wakilaaniwa kwa uamuzi wao wa kuipinga CCM.

Hata hivyo wanachama hao wameahidi kupambana mpaka tone la mwisho.

Source: Mwananchi Alhamisi Uk 16

lahaulaa....mie hata siseme....wacha mote wa mageuzi ufanye kazi yake......
 
Nape kama publicity master anatakiwa angalau abuni operations zitakazorudisha matumaini. Unajua watu sasa wameelimika zamani ilitosha kutoa tamko toka Lumumba kwenye RTD na watu wakafuata siku hizi ni tofauti kabisa. Mfano kama CDM wameanzisha M4C wao CCM wanaweza kubuni Operation Mapinduzi Daima OMD ni mfano tu wakaipeleka mikoani, sijui wanashindwa nini wakati funds kwao si tatizo.
Mkuu Feedback, Siku hizi na wewe unasahau sana...chadema ilipotangaza maandamao nchi nzima CCM wakaja na kujivua gamba lakini angalia nini kimetokea...kuna wananchi kwasasa wana hasira sana na CCM eti leo CCM waje pale uwanja wa NMC nao waitishi mkuano siwatavuna aibu na ndipo watakuwa wanautangazia umma biashara ya CCM imekwisha, mimi naona bora wakae kimya wapange baraza lao litakalo tuwezesha maisha kuwaangala kaahueni vinginevyo tutawapopoa mawe tu....
 
Hatupanii kuiua CCM bali kuipunguza, unataka kuileta CCM kwenye uwiano ulio sawa ili uwajibikaji uwepo.
Umesema yaliyo moyoni mwangu, kuiua CCM ni kuiua Tanzania,
ni vigumu sana kwa nchi kuendelea bila kuwa na upinzani imara.
 
Tulikuwa njiani kuwafukuza uanachama - Nnauye Jr
Taarifa nilizo zipata muda si mrefu ni kuwa taasisi mbili za CCM zitakufa kabisa baada ya mkutano wa Jumamosi utakao fanyika NMC kwani kuna viongozi wengi sana kutoka UVCCM na umoja wa wanawake CCM kuhamia CHADEMA....tunasubiri tamko la nape aseme alikuwa na mpango wa kuwafukuza...
 
Magamba hayo lazima yavuke. Vijitu 800 katika wilaya ya watu millioni 4 ni kama ushuzi wa ngomani, upo lakini haunusiki.!

Kuna wilaya yenye population ya million 4 nchi hii? Nape, kazi unayo! Ukiendelea na kazi yako hadi 2015 lazima utakuwa kichaa! Kwa watu wa aina ya huyu mtalishwa kasa wenye sumu hadi muishe!
 
Umesema yaliyo moyoni mwangu, kuiua CCM ni kuiua Tanzania,
ni vigumu sana kwa nchi kuendelea bila kuwa na upinzani imara.
CCM inatakiwa ife kabisa na hilo litatokea siku wakiwa chama cha upinzani ndiyo itakuwa mwisho wao kwani mtifuano uliko CCM ni mkubwa ila kwa kuwa ni chama tawala ndiyo maana unaona watu wameng'angana nacho..CCM walisha zoea ruzuku kubwa na kodi ya mapango wanayo amini kuwa ni ya CCM lakini siku chama makini kikiengia madarakani viwanja vilivyo jengwa enzi za babu/Baba zetu lazima zirudi kwa wananchi mfano uwanja wa Sheikh Amri Abeid iweje uitwe uwanja wa CCM wakati baba yangu alishiriki kuujenga huku akiwa hana kadi ya Tanu/CCM pia kuna wachina walikuja kutusaidia kuujenga....
 
Kuna wilaya yenye population ya million 4 nchi hii? Nape, kazi unayo! Ukiendelea na kazi yako hadi 2015 lazima utakuwa kichaa! Kwa watu wa aina ya huyu mtalishwa kasa wenye sumu hadi muishe!
hata mimi nimeshangaa sana Dar inawatu wengi sana lakini inasemekana wako takribani mil 5, iweje wilaya ya porini iwe na watu mil 4 au alijumlisha na wanyama na miti....
 
Mkuu una maneno machafu sana.Nisije nikakujibu ukanisababishia BAN kama ulivyomsababishia MOLEMO
USIMWOGOPE HUYO NI MEMBE IN ACTION!! mzee hata zamu yako ya vijiti vya magamba ikifika ni lazima ukimbie kaya tu!!
 
Mkuu Feedback, Siku hizi na wewe unasahau sana...chadema ilipotangaza maandamao nchi nzima CCM wakaja na kujivua gamba lakini angalia nini kimetokea...kuna wananchi kwasasa wana hasira sana na CCM eti leo CCM waje pale uwanja wa NMC nao waitishi mkuano siwatavuna aibu na ndipo watakuwa wanautangazia umma biashara ya CCM imekwisha, mimi naona bora wakae kimya wapange baraza lao litakalo tuwezesha maisha kuwaangala kaahueni vinginevyo tutawapopoa mawe tu....
Mkuu Crashwise sijasahau, nakumbuka baada ya kikao cha Dodoma kina Nape waliongozana Iringa, Mwanza na kwingineko kwa kutafuta sifa tu, sidhani kama walikuwa serious, ilikuwa ni zuga au kwa msemo wa mitaani walikuwa wanampaka mafuta mwanzilishi kwa mgongo wa chupa, ndiyo maana operation vua gamba haikufika popote.
 
Back
Top Bottom