CHADEMA yaigalagaza tena CCM

CHADEMA yaigalagaza tena CCM

Hii kata ndiyo kile kimtaa ambacho marehemu HOLACE KOLIMBA,aliyekuwa katibu mkuu wa chama cha mapinduzi alikuwa anaishi. Pia Marehemu Williamu Mpiluka ,aliyekuwa mbunge wa Mufindi(CCM) alikuwa anaishi hapo. Nina huhakika familia zao mpaka sasa zinaishi hapo. Pia huku anaishi MANYERERE , pia Shule ya Mama Tibaijuka Babro JOHA girls ndiyo ilipo. Ongera Chadema

Kumbe na Kolimba alikuwa anakaa kule? Mie napajua kwa Mama Mpiluka,kule sio Manyerere tu pia Mapunda wa gazeti la Tazama anakaa kule huyu ni kada wa Magamba.Sioni future ya CCM kwembe na sehemu nyingine zozote zinazojengeka kwa Dar.
 
Ccm ni kama mbuyu,kura za mijini hazitusumbui sana,wapiga kura wako vijijini,na ndo tunawekeza nguvu nyingi huku mjini mfanye mnavyoona inafaa,na katiba lazima ipite,leo tuko loliondo tukirudi ni mkoa mzima wa arusha hadi kieleweke
Mulisema ni arusha na moshi tu,baadaye moto ukahamia kanda ya ziwa,kiutani utani mara sumbawanga wakatia chorus,mbeya,iringa,shinyanga,mara,nako moto umekolea,unakumbuka singida vijijini mlifanywa nini uchaguzi wa mitaa uliopita?sitaki tena kukuambia kitu ambacho mwenyewe unakiona!!kiufupi ni kuwa muda wenu wa matumizi umekwisha,kazi yetu ni kuwaonyesha tu watu expire date kwenye kopo la ccm,wenyewe wanajua la kufanya.
 
CC: Nape Nauye + Juliana Shonza; CDM inakufa kila kona ya nchi!! ha ha ha !
 
"Bila dola haya makitu niwepesi kama karatasi ........... !!" Sijui nani alisema haya maneno
 
Ni hivi Mkuu hawa wahuni akiwemo yule Mkuu wa kitengo chao cha ugaidi waliitabiria CHADEMA kufa hata kabla ya 2015. Nikasema Mungu ni mkubwa kwamba pamoja na utabiri huo wa hawa wahuni wa chama chetu kipenzi kuelekea kaburini bado kinafanya vizuri kwenye chaguzi nyingi nchini na kukiadhibu hicho ambacho kimejaa wahuni, wezi, wapokea rushwa, mafisadi, majangili na magaidi chenye uhai wa miaka chungu nzima ijayo.

Sijakusoma mtu wangu....
 
Ukimuuliza nape atakujibu hajui kama ulikuwepo uchaguzi atasema niko kwenye ziara na katibu mkuu wa chama huku ngorongoro
 
Wale magamba wa Lumumba hawajatia timu hapa.....
Na bado hizo ni mvua za rasharasha...desemba ni elininyo kabisa siyo tu wataacha kuingia huku JF bali watakimbia nchi kabisa nadhani wataelekea Somalia
 
Hao wana wa ccm,wafugaji wa fisi wa kisasa wako wapi?
Au wamewapeleka fisi kwenye maonyesho?
 
Back
Top Bottom