brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,879
- 7,393
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeibuka na ushindi dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa marudio wa Serikali za Mitaa katika mtaa wa King'azi B, Kata ya Kwembe, jijini Dar es Salaam.
Akitangaza matokeo hayo, Msimamizi wa uchaguzi huo, George Lupia, alisema Chadema kimeshinda nafasi zote hizo dhidi ya wapinzani wake CCM na hivyo kuwa viongozi wa mtaa huo.
Msimamizi huyo alisema kuwa mgombea wa Chadema, Donath Mtemekele, alishinda kwa kupata kura 585 huku wa CCM, Daud Ngaliba, akipata kura 376 na kwamba kura 18 ziliharibika.
Chanzo:EATV radio
Akitangaza matokeo hayo, Msimamizi wa uchaguzi huo, George Lupia, alisema Chadema kimeshinda nafasi zote hizo dhidi ya wapinzani wake CCM na hivyo kuwa viongozi wa mtaa huo.
Msimamizi huyo alisema kuwa mgombea wa Chadema, Donath Mtemekele, alishinda kwa kupata kura 585 huku wa CCM, Daud Ngaliba, akipata kura 376 na kwamba kura 18 ziliharibika.
Chanzo:EATV radio