fasiliteta
JF-Expert Member
- Jul 2, 2014
- 2,165
- 3,655
Ndugu zangu CHADEMA ukweli tutauseme hata Kama hamtaki Ila tutasema tu, nyinyi ni jipu kubwa Sana katka ustawi wa vyama vya upinzani kiasi kupoteza Imani kubwa kwa wananchi tulowaamini kabla ya kuja kugundua uovu mloficha ndani ya nafsi zenu.
Hakuna wananchi wenye akili wanaoendelea kuwasapoti kwa Sasa hata mje na beti za mapambo na mapambio,nyinyi CDM mnauwezo mkubwa wa kupaka rangi nyeusi kuonekana nyeupe kwa kutumia chaki kisa tu ni nyeupe.
Watanzania wa Sasa si wa zama zile za miaka kumi nyuma.Hatutaki ujinga wenu wa uroho na uchu wa madaraka kwa njia yoyote(Haramu au halalali),yalotokea 2015 kwa upepo wa mabadiliko ovu yametufunza mengi Sana.Sasa tumeamka
Na kweli kabisa tumeamka Sana maana si kwa kuaminishwa kule mtu Fisadi papa miaka zaid ya 10 afu tubadilishiwe gia angani.
Watz wa juz,Jana si wa Leo maana si kwa ajenda za nchi Haina ndege Kisha zinunuliwe na tubadilishe ajenda kua ni ndege hazituletei kula.
WaTZ sisi so wale wa kuaminishwa kua tunataka democracy Kisha mwenyekiti wa chama adumu zaidi ya vipindi 3-4 huku akimfyekelea mbali kila aliyetaka hicho kiti.
WaTZ wa Sasa si wale wakihoji matumizi ya ruzuku basi wanafukuzwa ndani ya chama huku wakiangalia ruzuku zikitafunwa.
WaTZ wa sasa sio wale wa Jana wakuona gari ya chama ikiandikwa kadi ya umiliki jina la mwanachama.
WaTZ wa Sasa si wale wa Jana wa kukaa na Dr.slaa kupambania na kuusemea ufisadi Kisha tunayemtaja Fisadi papa na genge lake aje apewe nafasi ya kugombea huku Dr.slaa akiwekwa pembeni kisa tu Hana fedha ya kampeni.
WaTZ wa Sasa si wa Jana wa kuimba mabadiliko na kuzungusha mikono ya mabadiliko kwa ajili tu ya kuhalalisha uovu.
WaTz wa Sasa si wakuingia barabarani wavunjwe mikono Kisha familia zao zigharamike huku familia za viongozi wa CDM wakipiga zao Heineken,huku wakila Bata na kusoma ughaibuni.
WaTZ wa Sasa si wajinga kiasi Cha kujua Chama ni nn na Sacco's ni nn.
WaTZ wa Sasa si wa kuwaambia corona ipo Kisha wewe usionyeshe hata mfano wa tahadhari na kuunga mkono mikusanyiko huku 2meter Distance kugeuka zero distance.
Tuacheni unafiki tusonge mbele Kama nchi,CHADEMA Mnamakandokando mengi Sana.
SISI SI WADANGANYIKA TENAAAA.
Hakuna wananchi wenye akili wanaoendelea kuwasapoti kwa Sasa hata mje na beti za mapambo na mapambio,nyinyi CDM mnauwezo mkubwa wa kupaka rangi nyeusi kuonekana nyeupe kwa kutumia chaki kisa tu ni nyeupe.
Watanzania wa Sasa si wa zama zile za miaka kumi nyuma.Hatutaki ujinga wenu wa uroho na uchu wa madaraka kwa njia yoyote(Haramu au halalali),yalotokea 2015 kwa upepo wa mabadiliko ovu yametufunza mengi Sana.Sasa tumeamka
Na kweli kabisa tumeamka Sana maana si kwa kuaminishwa kule mtu Fisadi papa miaka zaid ya 10 afu tubadilishiwe gia angani.
Watz wa juz,Jana si wa Leo maana si kwa ajenda za nchi Haina ndege Kisha zinunuliwe na tubadilishe ajenda kua ni ndege hazituletei kula.
WaTZ sisi so wale wa kuaminishwa kua tunataka democracy Kisha mwenyekiti wa chama adumu zaidi ya vipindi 3-4 huku akimfyekelea mbali kila aliyetaka hicho kiti.
WaTZ wa Sasa si wale wakihoji matumizi ya ruzuku basi wanafukuzwa ndani ya chama huku wakiangalia ruzuku zikitafunwa.
WaTZ wa sasa sio wale wa Jana wakuona gari ya chama ikiandikwa kadi ya umiliki jina la mwanachama.
WaTZ wa Sasa si wale wa Jana wa kukaa na Dr.slaa kupambania na kuusemea ufisadi Kisha tunayemtaja Fisadi papa na genge lake aje apewe nafasi ya kugombea huku Dr.slaa akiwekwa pembeni kisa tu Hana fedha ya kampeni.
WaTZ wa Sasa si wa Jana wa kuimba mabadiliko na kuzungusha mikono ya mabadiliko kwa ajili tu ya kuhalalisha uovu.
WaTz wa Sasa si wakuingia barabarani wavunjwe mikono Kisha familia zao zigharamike huku familia za viongozi wa CDM wakipiga zao Heineken,huku wakila Bata na kusoma ughaibuni.
WaTZ wa Sasa si wajinga kiasi Cha kujua Chama ni nn na Sacco's ni nn.
WaTZ wa Sasa si wa kuwaambia corona ipo Kisha wewe usionyeshe hata mfano wa tahadhari na kuunga mkono mikusanyiko huku 2meter Distance kugeuka zero distance.
Tuacheni unafiki tusonge mbele Kama nchi,CHADEMA Mnamakandokando mengi Sana.
SISI SI WADANGANYIKA TENAAAA.