CHADEMA wasaliti - CUF

Nakupongeza sana kwa kujitokeza kwako na kutoa msimamo wako kuhusu kujiunga kwako na CUF. Nakuomba sana ukipata nafasi fanya ziara wilayani Kilwa ambako CUF mna wanachama wengi sana na mmefaanikiwa kuwa na mbunge. Wanachama wenu kule kilwa inaonekana hawajazielewa sera za chama chenu kwani wanaamini kuwa mwana CUF ni kuwa adui wa watumishi wa serikali na kwamba hawatakiwi kufanya shughuri yoyote ya maendeleo hata kama nikusafisha mazingira yao. Ajabu hawataki hata kuchimba vyoo kwa ajili ya shule zao. Uungwana uko wapi walimu katika shule kutojengewa vyoo na hivyo kuchangia choo kimoja na wanafunzi wao? Maelezo yanayotolewa eti CUF mnatangaza kuwa jukumu la kujenga vyoo shuleni ni la serikali. Sasa mchango wa wananchi ni upi? kwani mlipuko wa maradhi ukitokea watakaoathirika ninani?Tafadharini waelimisheni wana chama wenu umhimu wa kuchangia maendeleo yao.
 
CUF wameenda igunga kuisaidia CCM ishinde siyo yenyewe kushinda,wao CUF wanamuafaka na CCM huko Zanzibar sasa ndoa yao si bado haijavunjika wananchi tusiwaskilize hao ni ccm ya pili.

kha! mbona chadema magwanda wana muafaka na ccm arusha na halmashauri kadhaa hapa nchini? si mnevunja ndoa yenmu na nyie?? yani nyani haoni ****** wake!
 
<br />
<br />
hapa kuna pwent. Siasa hovyo sana
 
<br />
<br />
mkuu karibu sana hapa kwenye forum hii ili ujibu kero zetu juu yako.Je umebadilisha msimamo wako kwamba chadema ni chama cha kidini kama ulivyosema awali? Je kwanini wabunge wako bungeni walisema wanajitoa kwenye upinzani kwa vile unaongozwa na chadema? Je kwanini uliwahi kusema chadema ni chama cha vurugu kwa vile kinaongoza maandamano? Je kwanini misimamo ya ccm na cuf inafanana mnapoizungumzia chadema?
 
Mtatiro ni jembe la ukweli na ndiyo maana washabiki wa CHADEMA humu jamvini kila wakiona jina la Mtatiro wanakuja wakali kama pilipili,
Mtatiro msimamo wako nimeupenda, waache vijana wanaokimbilia vyama maarufu wakaendeleze umaarufu huko, hiyo CUF yako wanayoidharau kaa chini utulie uijenge ijengeke.

Mimi na watu wengi tuliosoma UDSM tunatambua uwezo na mchango wa Mtatiro katika harakati za kuwapigania watoto wa masikini, most of the time DARUSO nzima ilimkimbia na alibakia mwenyewe akiendeleza mapambano tangu enzi za Mwikwabe Mwita Waitara(Mtatiro akiwa mbunge, Magesa Mwita(Mtatiro akiwa Waziri wa Mikopo) na enzi za urais wa Daudi Deo( Mtatiro akiwa Waziri Mkuu) na Baadaye kuwa KATIBU MKUU wa Umoja wa vyuo vikuu Tanzania(TAHLISO). Mimi siamini kuwa Mtatiro amepitia nyadhifa zote hizi kwa tamaa yake au alipewa nafasi hizi kwa kuhongwa au kupendelewa, siamini kabisa na labda mtu anisistize kuwa alibebwa ili kushikilia nyadhifa hizo ambazo wanafunzi wengi wa vyuo vikuu walizitafuta bila mafanikio.

Kwa nature yake ni vigumu akiwa mahali na usitambue harakati zake, mara kadhaa aliwahi kufukuzwa chuo na kurudishwa na mara kadhaa amewahi kukaa lupango kwa ajili ya kuwatetea wenzie. Sielewi watu tuna chuki zipi kwa Mtatiro.

Alipomaliza Chuo kikuu alijiunga na CUF na baada ya muda mfupi akakabidhiwa wadhifa wa Mkurugenzi wa Haki za Binadamu wa chama hicho, baadaye mwaka 2010 Desemba akapewa Ukaimu naibu katibu mkuu na mwaka huu 2011 mwezi mei akachaguliwa rasmi kuwa naibu katibu mkuu Tanzania bara wa chama cha CUF. Sielewi huku nako alihonga, aliomba, alipewa kwa bahati mbaya au la.

Nashawishika kuamini kuwa Mtatiro ni kiongozi wa Ukweli na ni kiongozi tegemeo katika nchi yetu. Ni vigumu kwa chama kama CUF kwa umri wake kupewa unaibu katibu mkuu. Lazima waliompa nafasi hii wanaamini uwezo wake na wanaanza kujenga future ya CUF. Watu wote wenye upeo rasmi hawawezi kuthubutu kumdhihaki bila sababu za msingi .

Na kwa hali halisi ilivyo , tangu mtatiro amekuwa CUF walau CUF imeanza kuwa na uhai wa kutosha na vijana wengi wameanza kupendezewa na CUF, Mtatiro amekuwa akiiwakilisha CUF katika mijadala mikubwa kwa uwezo mpana na hivi sasa ameifanya CUF walau kuwa na uhai kwenye vyombo vya habari. Ukiwauliza watu wa ndani ya CUF watakwambia huyu ni NAIBU KATIBU MKUU wa kwanza kuonesha mafanikio makubwa sana katika chama hicho ambacho kilikuwa kimeanza kuporomoka kisiasa.

Kwa chama kinachobanwa kisisasa kama CUF itamchukua muda fulani kuanza kuirudisha CUF yenye matarajio, kwa sasa wadau wengi wanaweza kumcheka lakini ,ikiwa ataendelea na mbio hizi na akatumia uzoefu wake mkubwa wa uongozi ambao amewahi kuupata nyuma CUF ita-shine na wakati huo kejeli hizi zitaisha.

Nachoweza kumshauri Mtatiro ni kuwa aendelee kujiamini sana kama alivyofanya kipidi chote cha nyadhifa zote alizowahi kushika. Ajibu hoja na vijembe ambavyo chama chake kinapewa kwqa hoja bila kulalamika na atambue kuwa mamilioni ya watanzania wanamtizma kila siku na wanatambua uwezo wake mkubwa.
 

Sina nia ya kumtetea Julius lakini amekanusha kuhusishwa na kilichonukuliwa na mwanzisha thread hii. So logically this thread is now rendered redundant!

Haya mengine uliyoyaandika hapo juu sidhani kama ana sababu ya kuyajibu kupitia thread hii ya kizushi ambayo muanzishaji na wachangiaji waliomu-attack Julius walipaswa ku-apologize in the first place...

Sina nia yangu ku-stifle your freedom to express your opinion but ni muhimu kutumia hekima kwenye mambo basic.
 
Ndoa ya kwanza ilikuwa kule Kigoma, sijui ya nani ile? hii ya CUF ya pili na imefana sana, wana makamu wa Rais. Unalo?

kiukweli mwanzoni nilikuwa najua huwa unabishiaga hoja za ukweli kwa sababu yakuwa ccm lakin leo nimetambua sasa kwamba hata uwezo wako wa kufikiri una mushikheri! Kilichofanyika Kigoma ni kugawana madaraka kutokana na idadi ya madiwani kuwa sawa kati ya ccm na Chadema issue ikawa lazima waongoze kwa awamu' sasa unahusisha vipi na ruala la cuf na ccm kule Zanzibar ili hali hawa wanaongoza kwa pamoja serikali moja tena inaitwa ya kitaifa!
 
ukumbukwe kipindi anatolewa kwenye madaraka ya serikali pale chuo kikuu cha dsm, aliambiwa ni mtu wa kukurupuka. kwa hiyo si mshangai
 
<br />
<br />
mkuu inaonekana unamfahamu Mtatiro kuliko anavyojifahamu mwenyewe mpaka inatia shaka.
 
<br />
<br />
wewe ni nani hata umtetee? Ni katibu muhtasi wake? Tunamtaka akanushe madai yake yote na matusi yote aliyoitukana chadema.Ambalo chadema hawatamsamehe kirahisi ni ule uzushi wake kwamba chadema ni chama cha kidini.Hiyo ni dhambi kubwa kuwahi kufanywa na mwanasiasa tena kijana.
 
kuna watu walisema humu kuwa hakuna mgogoro kati ya CUF na CCM,kilichopo ni mambo ya wanandoa wanagombana na kupatana, na sasa ona wanampango wa kushambulia CHADEMA. mbona hasemi kuhusu kuishambulia SAU? au hajui kuwa nacho kimegombea? sasa noona lengo la CUF c kushinda ila no kukishafua CHADEMA.
 
<br />
<br
Usemi huu wanakosea kuutoa Igunga wakatoe LINDI walikozoea kutolea ndio madhara ya kopi and paste majungu
 
Junior Member



Join Date : 4th September 2011
Posts : 1
Rep Power : 0
Huyu ni mtatiro kweli?
kwa hiyo kaamua kujiunga chap chap ila kukanusha?
kwanini anaichukia Chadema?
kwanini anaona CCM itashinda?
Duh? maswali mengi kuliko majawabu? haya!
 
mtatilo uko sawa hawa chadema kidomo domo sana, kazi yao kuhubili tumbo tumbo tumbo tu.
 
cdm haipo tena wafuasi wake waliokipa kura wamerudi kwenye chama chao ccm, na siku za chadema katika ramani ya siasa za tanzania zinahesabika.
 
  1. Sijawahi kusema chadema ni chama cha kidini labda u-prove hapa, na uki-prove kuwa nimewahi kusema hivyo naahidi nitajiondoa hapa JF kama adhabu binafsi ya kukimbia maneno yangu.
  2. Wabunge wa CUF hawakuwahi kujitoa katika kambi rasmi ya upinzani inayoundwa na CHADEMA, badala yake chadema ndiyo waliweka msimamo kiwa hawawezi kufanya kazi na CCM "B"(yaani CUF) na mie nikasema hatutawalamba miguu kuwabembeleza tufanye nao kazi as long as hawatutaki. Baada ya muda utakumbuka Freeman Mbowe alijitokeza na kutaka wabunge wetu wajiunge na kambi yake tukakataa na kuwaambia CHADEMA iweje majuzi watukatae na kuzunguka nchi nzima wakituita "CCM B" then baada ya muda wanabadilika na kutaka tuingie kwenye kambi yao, ina maana wako tayari kufanya kazi na CCM "B", tukawaambia sharti moja kubwa ni kuwa warudi kule kote walikopita na kutangaza kuwa hawawezi kufanya kazi na chama ambacho ni CCM B wakatusafishe, unfortunately hawakuweza kufanya hivyo, nasi kama chama cha siasa tukasema hatujihusishi na hiyo kambi ya KUDENGULIWA na SITAKI NATAKA.
  3. Mimi sikuwahi kusema kuwa chadema ni chama cha vurugu unless you prove it, kuna wakati palikuwa na mjadala wa maandamano ya CHADEMA na waandishi walitaka kujua msimamo wetu juu ya maandamano hayo nami nilieleza kwa uwazi kuwa maandamano hayo ni kitu cha kawaida na ni haki ya kikatiba na nikaeleza namna hata ambavyo CUF huandamana mara nyingi sana na ninakumbuka kuna magazeti niliyaona yakieleza kuwa CUF yaunga mkono maandamano ya CHADEMA. Tulichotofautiana na CHADEMA ni suala la kung'oa serikali kabla ya 2015, nilisema kwa msisitizo kuwa CUF haiwezi kushiriki mapinduzi yoyote ya nguvu kwani ikiwa watanzania hawaitaki CCM kwa dhati wafanye hivyo 2015 na waweke serikali wanayoitaka, na nilisema hizi falsafa za kung'oana madarakani kwa nguvu mwisho wa siku huwafaidisha wachache tu na wao pia hung'olewa baada ya muda kwa nguvu. Na nikasema ki_itikadi CUF haiamini katika mfumo wa serikali za mabavu. Na nikasema kama tatizo letu ni kuibiwa kura kila mwaka tulipiganie kwenye katiba na tupate tume huru ya Uchaguzi itakayotenda haki na badala yake tusiwekeze nguvu na hadaa katika serikali iliyochoka na ambayo ipo kisheria(hata kama mimi na wewe hatuitaki). Na hadi leo msimamo wa CUF uko hivyo, kuwa hatuamini katika serikali za kuondoana kwa nguvu kwani tunajua madhara ya hali hiyo. Kwa hiyo sikuwahi kuita chama chochote kuwa ni chama cha vurugu.
  4. Suala la wabunge wa CCM na CUF kuizungumzia CHADEMA kwa mtizamo mmoja haliko sahihi. Mitizamo inatofautiana sana kutegemeana na tofauti za vyama hivi. Hapa nilihitaji kuona ukieleza pia namna gani ambavyo Wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakiisema vibaya CUF na kuisolola CUF kwa kila namna. Kwa mfano, CHADEMA baada ya Uchaguzi wamezunguka nchi nzima wakitangaza kuwa CUF ni CCM "B", CUF ni wakala wa CCM, CUF siyo chama cha upinzani n.k..... Mbona katika kipindi hiki sikusikia mkiishtumu CHADEMA kuwa inaitukana CUF? Sasa kwa nini CUF wakijibu hoja hizohizo na kuieleza CHADEMA ilivyo mnakasirika, mnadhani CUF hakuna binadamu ambao pia kimaumbile husikia maumivu wanapoona ukweli unapotoshwa kuhusu chama chao kwa faida na maslahi ya chama kingine>?
Nachotaka kusisitiza hapa ni kuwa usitarajie hata siku moja kuwa CHADEMA au chama chochote kile wataitukana CUF au kuizulia masuala ya uongo halafu CUF ikakaa kimya, hatutakaa kimya! Tutajibu kila Propaganda kwa kutumia ukweli halisi na uzuri wa ukweli ni kuwa wenyewe hudumu. HATUTOKAA KIMYA unless otherwise vyama vinavyotutukana bila sababu viachane na ajenda hiyo.

Nimejitahidi kujibu dukuduku lako kwa kadri ya upeo na maono yangu, majibu haya yanaweza yasikuridhishe au la lakini yote haya tunayafanya kwa sababu hatuna budi kufanya vinginevyo. Kama pana maoni, maswali au ushauri mwingine nitumie kwenye juliusmtatiro2011@yahoo.com au tembelea ukurasa wangu wa face book na ku_post chochote utakacho nami nitakujibu.

Asante,
Mtatiro.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…