CHADEMA wapelekana kortini

CHADEMA wapelekana kortini

Umenikosha kwa sentensi yako fupi na iliyobeba maana kubwa.

Hiyo ndiyo Democracy ya kweli, kama hukubaliani na jambo unapeleka shauri lako kwenye chombo cha kutafsiri sheria ili haki itendeke na sio 'kumpiga mtu bomu' au 'kitu kizito'.
 
Kwenda mahamani ni haki yake, we unadhani huku ni ccm kwenye nidhamu ya woga kama jamaa wako wa nzega? Acha waende kutafuna haki yao pale wanapooa wameonea huko ndiko tutajua kila kitu
 
Unatakiwa nawewe ujaribu kutumia kichwa chako vizuri. Kama kila siku unasema kwa sentensi fupi hivi zisizo na maana wala facts utabaki kuwa mzushi na muongo tu.

Hebu jaribu kuthibitisha kauli yako ili ueleweke mkuu.

nilishasema siku nyingi tu cdm ni wasanii
 
hapo hawajachukua dola!! ugomvi moja kwa moja, je wakichukua??

Neno ugomvi kwako ni MSAMIATI chama kupitia vikao halali vimefukuza wahuni halafu wahuni wamekimbilia mahakamani hapo ugomvi uko wapi, ugomvi ni kama ule wa NZEGA watu wanashikiana BASTORA.
 
Hakuna mtu bora kuliko chama.matata na chagulani wamefika hapo kupitia chama.matata alikua ccm,alikuwa anagombea udiwani kupitia ccm,kwa mujibu wa watu ni kuwaalipata kura 2 ktk kura za maoni.baada ya kushindwa tu aliamua kugombea kwa tiketi ya cdm na kupata udiwani.Matata na chagulani wamekubalika kupitia chama.wengi wa madiwani wa cdm mza hawana elimu na waligombea basi tu baada ya watu kutojitokeza wakijua kuwa cdm haina nguvu mza.Hata Wenje asijisifu,naye aliingia kwa kubahatisha,hakuwahi kujulikana na hakupewa kabisa nafasi ya kushinda.viongozi wa chama mza sasa hivi hawawezi kuendana na kasi ya ukuaji wa chama,kwani cdm inakua kwa kasi sana mza.kuhusu chagulani kuzuiwa kufanya mkutano hizo ni njama za ccm kutaka kumpa umaarufu tu.huyo dogo hana lolote.sisi wana mza tunasubiri kwa hamu huo mkutano wa kujimaliza kabisa kwani hatapata watu zaidi ya wanaccm wenzake walioandaliwa.
 
Gwandaz, walikuwa wanasema hawana imani na mahakama. Kulikoni?
 
Jifunze spelling ndugu yangu, pamoja na hayo fuata link iliyotolewa ili ujue kama suala hili ni personal interest au ni suala la wakubwa wa chama kuminya democracy. Hiki ndio chama ambacho kinatuomba watanzania ridhaa ya kutuongoza wakati wanashindwa kujali maamuzi ya watu zaidi ya 3000 waliomchagua Mhe. Henry Matata. Wanajifungia watu 20 wanatoa maamuzi bila maamuzi hayo kujadiliwa na Kamati ya utendaji ya Wilaya ambapo diwani huyo anatokea. Suala hili linafanyika kwa sababu tu ya kumfurahisha Baba Junior.

Matata anataka angejadilikwa na kamati ya wilaya kisha mkoa.Je huko kamati ya wilata na mkoa kuna watu wangapi.Period
 
Kwa akili yako ndogo, usanii wao upo wapi?

Kifarutz;Kila siku huwa sikubali siasa hizi zilizoibukia CHADEMA za kufukuza viongozi waliochaguliwa kwa kura za wananchi!Haiwezekani na ni kuiminya demokrasia kwa KAMATI KUU-CHADEMA yenye wajumbe si zaidi ya 20 KUWAFUKUZA MADIWANI/WABUNGE waliochaguliwa kwa kura nyingi za wananchi tena wengine wasio shabikia chama chochote(independents)!

Siasa hizi za kufukuzana nazipinga;kama mwakilishi kaenda kinyume na CHADEMA na hataki kujirekebisha inabidi tu ATENGWE NA APUUZWE hadi mwaka 2015!
 
Gwandaz, walikuwa wanasema hawana imani na mahakama. Kulikoni?
Shule muhimu: CDM haina imani na baadhi ya majaji na mahakimu wa mahakama si mahakama na ni baadhi... ok na toka Lissu awaumbue live wamenyooka! subiri hukumu ya Lema uone wanavyojipendekeza.
 
Shule muhimu: CDM haina imani na baadhi ya majaji na mahakimu wa mahakama si mahakama na ni baadhi... ok na toka Lissu awaumbue live wamenyooka! subiri hukumu ya Lema uone wanavyojipendekeza.

Bado hujajitetea ipasavyo, kama umechanganyikiwa vile.
 
Hizo ndo sera zilizotufikisha hapa, kamwe siziungi mkono. Msaliti yeyote inafaa atimuliwe mara moja. Chenge mwizi, Jairo, Ngeleja, Kikwete etc.. ni mifano mizuri, hao ni wasaliti wa taifa! Sera za kuvumiliana na kulindana hazina nafasi CDM. Tunachukia kumfukuza mtu ila usaliti tunauchukia zaidi. Kumbuka kuwa CCM ni mafia, wameingiza mapandikizi ndani ya chadema hivyo basi to make a story short maamuzi ya mwisho yanabakia kwa kamati kuu. Chadema bahati nzuri hatuna ombwe la uongozi. I repeat, hatufurahii kufukuza watu ndani ya chama. Bado shibuda huyu naye ni pandikizi na mabwepande
 
Mimi ni Mmoja wa watu waliotoa onyo kwa CHADEMA kuruhusu matata kugombea na kushinda umeya wa jiji la mwanza kwa sababu ya historia yake ya Ujambazi na Ukwepaji wa Kodi, hata Hotel yake ya Magnum pale ilipojengwa ni eneo la uwanja wa wazi ambalo alilichukua kibabe wakati huo kaka yake akiwa kigogo hapo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Mwanza.

Na ninaendelea kuunga mkono maamuzi ya kumfuta uanachama Japo yamechelewa sana
 
DIWANI wa Kata ya Kitangiri, Henry Matata ambaye amevuliwa uanachama na Kamati Kuu ya Chadema, amewasilisha mahakamani zuio la kutekelezwa kwa uamuzi huo.

Matata aliwasilisha hati ya kuomba Mahakama izuie uamuzi huo wa Chadema jana, kwa madai kuwa umekiuka Katiba ya chama hicho.

Akizungumza jana baada kuwasilisha hati hiyo mahakamani, Matata alidai kuwa kabla ya uamuzi huo wa Kamati Kuu, alipaswa kujadiliwa na Kamati ya Utendaji ya Wilaya na Mkoa.

"Hakuna mwenye ubavu wa kuzuia Mahakama kufanya uamuzi, wanapaswa kuheshimu uamuzi wa Mahakama … mimi nimechaguliwa na watu zaidi ya 3,000, Kamati Kuu yenye watu 20 haiwezi kunyima haki watu wangu walionichagua kutokana na majungu ya wachache," alidai.

Alidai kushangazwa kuona kuwa Kamati Kuu inatoa uamuzi wa kumvua uanachama kabla ya kujadiliwa katika ngazi ya wilaya na mkoa.

Matata alidai kuendelea kupigania haki yake ya msingi kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho na kueleza kuwa uamuzi wa kumfukuza ulikuwa kinyume cha Katiba ya Chadema na ulilenga kumdhoofisha kisiasa, kutokana na viongozi wa ngazi za juu na wabunge wa chama hicho kumhofia kisiasa.

Mbali na kwenda mahakamani, Matata pia alitangaza nia yake ya kuwania umeya wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela.

Matata alidai kuwa chokochoko dhidi yake zilianza mapema, baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka juzi ambapo alichukua fomu ya kuwania umeya wa Jiji la Mwanza, lakini Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa aliamua kupindisha Katiba ili kumwengua.

Alidai kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Chadema, Meya anapaswa kuchaguliwa na kamati tendaji za wilaya na mkoa, baada ya kupigiwa kura, lakini Dk Willibrod Slaa na baadhi ya wabunge wa chama hicho, waliingilia kati na kumpendekeza meya aliyetimuliwa, Josephat Manyerere.

Mbali na Matata, Diwani wa Kata ya Igoma, Adam Chagulani (Chadema) amelazimika kusitisha mkutano wake wa hadhara wa kuelezea wananchi wake sakata la kuvuliwa uanachama, baada ya kudai kuwa Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje (Chadema), amekuwa akitumia watu kumfanyia vurugu.

Alidai baada ya kutangazwa kuvuliwa uanachama, alifanya mkutano na wananchi wake kuwaelezea kilichotokea na uamuzi ambao atachukua.

Chagulani alidai kuwa ingawa polisi walisitisha mkutano, kabla ya hapo Wenje alikuwa amepeleka wapambe wake kutoka mjini kwenda Igoma kwa kukodi magari na kuwanunulia ‘viroba’ ili wafanye fujo.

Hata hivyo, Wenje akizungumza kwa simu na gazeti hili alielezea kushangazwa na tuhuma hizo kwani yeye aliondoka Mwanza tangu Septemba 7, kushiriki kikao cha Sekretarieti na Kamati Kuu na bado hajarudi.

Naye Arnold Swai anaripoti kutoka Moshi, kwamba Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama amepinga safari ya madiwani wa Manispaa ya Moshi inayoongozwa na Chadema kwenda Kigali, Rwanda kwa madai kuwa bajeti iliyotengwa ya Sh milioni 123 ni kubwa.

Gama alitoa uamuzi huo jana, wakati akizungumza kwenye kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa, kilichohudhuriwa na madiwani hao na baadhi ya wakuu wa idara wa Manispaa ya Moshi.

Kwa mujibu wa Gama, safari hiyo haina tija, endapo watatumia kiasi kikubwa cha fedha hizo. Alisema madiwani kwenda kujifunza ni jambo la msingi lakini si kutumia fedha nyingi kiasi hicho, ambazo ni kodi za wananchi wanaohitaji maendeleo.

“Si kwamba nawakatalia lakini nasema safari kama hii ya wakati mmoja na mara moja tu kwa mwaka, siwezi kuikubali kutokana na matumizi makubwa ya fedha, wakati shida za wananchi hapa ni nyingi, kama mnataka, basi waende wachache watumie Sh milioni 20, hapo sina pingamizi,” alisema Gama.

Alisema kabla hajamshauri Waziri husika kutoa kibali cha kuwaruhusu kusafiri nje ya nchi ilibidi ajiridhishe kwanza na ndipo alipobaini kuwapo kwa kasoro ambazo ni kikwazo cha safari hiyo.

Gama alisema moja ya matatizo ni msafara wa watu 57 wanaotarajiwa kwenda Kigali kwa siku saba huku malipo ya posho zao yakionesha watalipwa siku tatu, jambo ambalo si sahihi.

Alieleza, kwamba kutokana na msafara huo zaidi ya Sh milioni 200 zingetumika na kuagiza waende wachache, ili fedha zingine zitumike kwa maendeleo.

Meya wa Manispaa hiyo, Japhary Michael (Chadema) alisema anashangazwa na uamuzi wa Gama kupinga safari hiyo wakati ipo kikanuni na kulaumu kitendo cha kuzungumzia suala hilo kwa vyombo vya habari.

Michael alisema wamekubaliana vizuri na uamuzi uliotolewa na Gama na hawana pingamizi juu ya hilo, lakini alieleza kuwa ushauri huo wangepewa kwenye vikao vya ndani na si mbele wanahabari.

Chanzo: HabariLeo

Uchu wa madaraka

Matata waulize wenzako wa arusha uzuri wa cdm maamuzi yao uwa awakurupuki kutumia magazeti na mahakama ni kubuy time .M4c ikija mwanza ukweli wenu utawekwa hadharani.
 
Duh ,wanalaani kitendo cha mishe zao kutangazwa katika vyombo vya habari.
 
Back
Top Bottom