CHADEMA wanajidanganya tena sana

CHADEMA wanajidanganya tena sana

Chadema ilipoangukia ni pale ilipo changanya maji na mafuta na zaidi kibaki kuwa chama cha ruzuku na ndugu zake mbowe hapo hakitanyanyuka tena
Mbowe mtu wa ajabu, eti wakionewa na kupigwa na polisi ili kuikomesha ccm ni kususia uchaguzi, nimecheka sana, afu eti anasema anaomba tume iandae uchaguzi mpya..
 
Mbowe mtu wa ajabu, eti wakionewa na kupigwa na polisi ili kuikomesha ccm ni kususia uchaguzi, nimecheka sana, afu eti anasema anaomba tume iandae uchaguzi mpya..
Kazi yake ni kuigaiga tu hapo ana muiga odinga yeye alidhani chama niyeye kumbe watu wanafuata agenda
 
Swala hapa sio nani ashide! Swala ni Demokrasia idumishwe na Anayeshinda iwe ameshida kihalali ! Ila wewe unaonekana unashabikia as if ni simba na Yanga! Ok Let say Kunabakia Wabunge 2 wa Upinzani 2020 Faida Utakayopata kama Mwananchi ni nini? Itakuwa ni Majanga zaidi hata kwa CCM kwenyewe! Kukiondolewa kushinda Uchaguzi kwa Hila! Anayeshinda atakaa akijua asipofanya aliyotumwa na Wananchi next election watamtosa! Na hii inampa mwananchi nguvu na Ni Faida kwa Taifa zima. Anayejua atashinda kwa wizi,

Atanunua Ndege bila Budget
Atawavunjia nyumba na kuponda ponda sahani, kabati, sufuria na vyungu!
Atapandisha cheo watoa rushwa na wachuuzi wa madiwani
Atawapiga wabunge wenu risasi
Atahonga wabunge wake kwa pesa za hazina!
Kwani Mtamfanyaje? Mupe kura msimpe atajishidisha tu!
Wewe endelea kubaki na mawazo haya ya kitoto, duniani kote wanatumia sana ujanja kwenye siasa hasa fursa ya kufanya ujanja inapokuwepo. Siku mkija kustuka kuwa Chadema mnatakiwa kubadilika na kuja na mbinu ya kuchukua na kushnikiza kutangazwa ushindi wenu basi na wanachama wenu watakuwa tayari wameshawachoka. Chadema kikitaka kufanikiwa kisiasa ni lazima kiondoe uongozi wa wazee hawa akina Mbowe, Lowasa, Sumaye na wengine kwani wapo pale sio kufanya siasa za ushindi bali wapo pale kwa kutumia siasa kufanya biashara na kulinda Mali zao
 
Mwandishi wa Uzi huu aliona mbali. Ukimuonesha mtu udhaifu wako atakupiga milele
 
Chadema Imeuawa Na Luwasa,mbowe Ameshndwa Kuongoza Chama,amebaki Kulialia Tu,aachie Nafasi Ya Uewenyekiti Kwakina Juakali Na Heche
 
Ukifika katika mji na kuona mwendawazimu anaheshimika huku wenye busara wakidhikakiwa ogopa! Ukiona ujinga unasifiwa huku weledi ukifanyiwa kejeli tambua hapo "hamna kitu" zaidi ya yote ukiona mtu amejipanga kwenda kununua shuka akafika dukani na kununua radio jua tuna matatizo makubwa!!!
Wananchi hatujajua tunahitaji nini, na wanasiasa wetu hawajatambua wanapaswa kutupeleka wapi!? Watawala nao hawajafahamu kama wanaeleweka sera zao ama la!!? Kinachotisha ni mlipuko wa volcano.
Twafwaa!!
 
Na watawanyang'anya kila kitu..

2020 mbunge wa upinzani/chadema atakayerudi bungeni atakuwa ni msaliti wa chama!

Uchaguzi wa 2010 malalamiko ya kuibiwa kura..
Uchaguzi 2015 chini ya tume ile ile mliyolalamikia mnashiriki tena uchaguzi na kwa matumaini chungu mzima ya kushinda..

Bado tena 2020 nimeona kuna watu wanajipa matumaini ya kuishinda CCM chini ya tume ile ile waliyolalamika haiko huru!

Hii ni akili ya wapi? Ukiangalia kwa jicho lisilo la kishabiki ni kama Upinzani wa nchi hii unashirikiana na Chama dola kuwapa matumaini wananchi.

Mwingine kule Zanzibar alikuwa anawaambia watu bado kidogo ataapishwa kuwa rais..si maajabu haya?
 
Nadhani imefika sehemu inabidi kuachana Na Siasa kila mtu apambane Na Hali yake,haiwezekani Kimara Mbezi wamevunjiwa nyumba juzi tu hata hasira hazijaisha uchaguzi kata ya jirani Saranga CCM wanashinda tena kwa Kura nyingi tu. Ni ujinga kuwapigania Watanzania,kila mtu apambane na Hali yake
 
chadema wanaumizwa na vyombo ambavyo kimsingi ndivyo vilivyotakiwa kuwalinda hivyo chadema ni sawa na mtoto yatima ambae watu wameamua kumzulumu mali zake,ila kinachojengwa hapo ni kujenga uadui wa kutosaidiana kati ya chadema na ccm,sidhani kama itakuwa ni busara kumsaidia mwanachama wa ccm anaefuraia kupigwa risasi Lisu hata kama ni ndugu yako,hivyo hata michango ya harusi,misiba yatakuwa kila mtu na chama chake na hilo linatakiwa chadema walitangaze mapema maana kwa kuwa wao ni wanyonge wataweza kusaidiana zaidi kuliko ccm ambao wengi wao ni wanafiki mimi kuanzia leo sintomsaidia mwananchama yeyote yule wa ccm hata kama tumezaliwa tumbo moja
 
I salute you Marandu. Mimi nashauri ubaki huko huko uliko. Usije huku TZ kipindi hiki hadi hadi hapo upinzani watakapo chukua madaraka ya hii nchi. Kwani ninaamini watu wasiojulikana wana kutamani sana. Nakusihi sana utumie media zingine pia ambazo Watanzania wengi zaidi wataweza kufikiwa na haya unayoyaeleza na kufundisha. They are very useful. I believe you can do that. Utusaidie bro kutuongezea nguvu sisi Wa - TZ tunaoamini katika siasa za haki na demokrasia.
 
Kaka mimi naipenda sana democrasia na haki. naungana na wew 100%. Cdm imekuwa tofauti na miaka ya nyuma, sasa hv imejawa na viongoz wanaolalamika muda wote badala ya kukaa chini na kuja na mikakati imara ya kupambana na huu utawala wa hovyo. Uchaguzi mdogo kama huu cdm wametishwa kias hiki na wakatulia, uchaguz ujao watalia zaid ya leo. Wataalamu wa sayansi ya siasa waliopo hapa jf wakae na viongoz wa cdm na kuwashauri na kama wapapuuza basi watakuja kuyaona matokeo ya uchaguz ujao. Mtaporwa majimbo yote na mtabaki kusema Mungu anajua
 
Umejieleza sana but nilitaka kuona hitimisho lako ni la aina gani.
Udikiteta umetamalaki idara zote za nchi.
Waliopotezwa, waliouawa, waliopigwa risasi, waliofunguliwa kesi za uchochezi, waliojeruhiwa wakabaki vilema wote walikutwa na hayo wakiipigania haki yao na ya kwako pia wakipinga udikiteta ktk nchi yao na kutaka haki itendeke.
Ikiwa mtu kafikwa na hayo wewe ulitaka yamfike yapi ili ujidhihirishe kuwa ni mpambanaji.
On my side naipongeza upinzani kwa jitihada zao kwani yanayofanyika sasa hata Idd Amini Dada nahisi hajawahi yafanya.
Unyama wa serikali hii ni grade wanu duniani. Aliyofanyiwa Dr Shika na watesaji urusi wamefanyiwa wenzetu tayari ktk nchi hii.
Sina imani na ccm, sina imani na viongozi wake maana wanayoyafanya hata shetani anawashangaa.
Angalia kifo cha mawazo, mwangosi, maisha ya kibiti, aliko saanane, ya mbowe kuharibiwa bustani, kukomeshwa kwa fao la kujitoa, maslahi ya watumishi, maisha ya wakulima, gharama za elimu hakika napata kinchefuchefu kusikia neno ccm na kuona vazi la kijani(kumradhi watani zangu yanga).

Hitimisho ni Kuweka pembeni Ajenda ya Kuchukua Dola kwa sasa! Bali personally kupambana kuli isolate na kulimaliza Joka na stooge zake wachache waliotangaza vita haramu ya kunyang'anya uhuru kwa kumwaga damu zetu na uhuni wa aina nyingi. Kutoa Fundisho kuwa Unduli unagharama yake na haulipi.
 
Uzalendo na ujenga nchi ni kuwa mwanachama ama shabiki wa CCM!! Kweli nchi ina umoja!! Bila kuwa na katiba mpya ya wananchi ni kujilisha upepo.
 
Back
Top Bottom