Katika hali ya kushangaza Naibu Katibu Mkuu wa CUF Julius Mtatiro amesema CHADEMA kufanya maandamano na Mkutano Temeke Mwisho ni kuingilia ngome yao.
Akizungumzia mwaliko wa CHADEMA kuitaka CUF kushiriki mapokezi ya wabunge wa upinzani kesho na hatimaye kushiriki mkutano wa pamoja Mtatiro amesema kamwe CUF haiwezi kushirikiana na CHADEMA.
Mtatiro amesema mwaliko wa CHADEMA ni wa kisanii na wamegundua Temeke ni ngome kuu ya CUF kwa hiyo CHADEMA haiwezi kupata watu mkutanoni bila kuishirikisha CUF.Mtatiro ameuliza tangu lini Chadema imegundua CUF siyo CCM B? Mtatiro amelalamika CHADEMA inatafuta umaarufu Temeke kupitia mgongo wa CUF.
Kwa upande wake Chama cha NCCR Mageuzi kupitia Katibu Mkuu Sam Ruhuza kimesema kitashiriki kikamilifu mapokezi hayo kwani CHADEMA siyo adui yao bali adui yao ni CCM tu.
Wabunge wa CHADEMA na NCCR waliungana pamoja bungeni kupinga uonevu,ukandamizaji na udhalilishaji wa Spika wa bunge Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai dhidi ya Upinzani bungeni.Hata hivyo mara zote CUF wamekuwa wakiungana na wabunge wa CCM kuwapinga wapinzani wenzao.
Kesho Jumapili CHADEMA imepanga mapokezi makubwa na maandamano kisha mkutano mkubwa wa hadhara Temeke Mwisho kwa lengo la kulaani ukandamizaji wa Spika na Naibu wake.
Source:Tanzania daima/Nipashe.
Akizungumzia mwaliko wa CHADEMA kuitaka CUF kushiriki mapokezi ya wabunge wa upinzani kesho na hatimaye kushiriki mkutano wa pamoja Mtatiro amesema kamwe CUF haiwezi kushirikiana na CHADEMA.
Mtatiro amesema mwaliko wa CHADEMA ni wa kisanii na wamegundua Temeke ni ngome kuu ya CUF kwa hiyo CHADEMA haiwezi kupata watu mkutanoni bila kuishirikisha CUF.Mtatiro ameuliza tangu lini Chadema imegundua CUF siyo CCM B? Mtatiro amelalamika CHADEMA inatafuta umaarufu Temeke kupitia mgongo wa CUF.
Kwa upande wake Chama cha NCCR Mageuzi kupitia Katibu Mkuu Sam Ruhuza kimesema kitashiriki kikamilifu mapokezi hayo kwani CHADEMA siyo adui yao bali adui yao ni CCM tu.
Wabunge wa CHADEMA na NCCR waliungana pamoja bungeni kupinga uonevu,ukandamizaji na udhalilishaji wa Spika wa bunge Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai dhidi ya Upinzani bungeni.Hata hivyo mara zote CUF wamekuwa wakiungana na wabunge wa CCM kuwapinga wapinzani wenzao.
Kesho Jumapili CHADEMA imepanga mapokezi makubwa na maandamano kisha mkutano mkubwa wa hadhara Temeke Mwisho kwa lengo la kulaani ukandamizaji wa Spika na Naibu wake.
Source:Tanzania daima/Nipashe.