CHADEMA wanafaidika na Caller tunes charges??

CHADEMA wanafaidika na Caller tunes charges??

Kigarama

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2007
Posts
2,492
Reaction score
1,239
sasa watu wengi sana hapa kwetu Tanzania simu zao zina miito (Caller tunes) ya nyimbo za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na ninavyofahamu mimi miito hiyo hukatwa gharama za kuitumia na makampuni ya simu husika.

Labda tusema kuna watu milioni moja wanatumia miito ya nyimbo za CHADEMA. kwa kukatwa shilingi 350 kwa kila mwezi. Makampuni hayo ya simu yatakuwa yanaingiza shilingi milioni 350 kwa mwezi. CHADEMA wana mgao katika mapato hayo au hawana hati miliki ya nyimbo zake??
 
Nifanyeje niupate huo wimbo wakuu? Na unaitwaje? Nauhitaji kwa hakika.
 
ni namna nzuri sana ya cdm kujitangaza pia kusambaza ujumbe wa haja ya kutokomeza ufisadi. wakati wa kampeni caller tunes hizo zilikuwamo makampuni yote ya simu tigo,airtel na voda ikaondolewa,haiyumkini serikali/ccm ilipiga marufuku makampuni hayo kutumia caller tunes hizo. kama imerudi its a good move
 
Anaye fahamu jinsi wimbo huu unavyopatikana tafadhali tunauomba, ama mwenye nao please atuwekee ha jamvini tu-dowmload. Viva CDM tunakupenda.
 
Ccm ndio hopeless kabisa, siku moja nilishangaa sana baada ya baamedi mmoja kunionesha opena ya ccm ambayo kila ukifungua chupa ya soda au bia inaimba nyimbo za ccm (zile za capt. Komba)

kweli miongoni mwa siku ambayo niliwadharau ccm ni that day, maana niliona ni upuuzi mtupu kwa kweli, si bora wangenunua madaftari wakayapiga lebo ya ccm then wakagawa bure, kuliko kutengeneza opena zinazoimba vyimbo zetu tena mpaka uweke sikioni ndio utasikia.
 
Ccm ndio hopeless kabisa, siku moja nilishangaa sana baada ya baamedi mmoja kunionesha opena ya ccm ambayo kila ukifungua chupa ya soda au bia inaimba nyimbo za ccm (zile za capt. Komba)

kweli miongoni mwa siku ambayo niliwadharau ccm ni that day, maana niliona ni upuuzi mtupu kwa kweli, si bora wangenunua madaftari wakayapiga lebo ya ccm then wakagawa bure, kuliko kutengeneza opena zinazoimba vyimbo zetu tena mpaka uweke sikioni ndio utasikia.

Pamoja na kujitangaza nilitaka kujua kama chama, CDM wanafaidika vipi na charges ambazo vodaCom wanawatoza wateja wake. kwa wale wenye kuutaka huo wimbo wawapigie watu wenye wimbo huo kisha wabonyeze alama ya nyota basi kiurahisi kabisa wataupata. sasa sijui watakuwa wamewachangia CDM au watakuwa wamewaneemesha VodaCom ya kina RA na wenzie??
 
Back
Top Bottom