Chadema wampa Kikwete 'siku tisa'

Nguvu ya umma ilikuwa uchaguzi uliopita, ambapo aliyependwa na wananchi ndio amepewa ridhaa ya kuwaongoza watanzania. Sifa ya Tanzania na Rais JK nje ni kubwa kuliko ujuavyo. Ww hujiulizi kuna marais zaidi ya 54 Africa, kwa nn wachaguliwe 6 tu na JK yumo ? hapo ndipo utajua jamaa ni mashine nyingine kuliko fikra zako
Ni kweli heshima ya Tanzania na JK inawezekana iko juu lakini unalinganisha na rais yupi na Tanzania ya mwaka upi...heshima ya Tanzania ya mwaka 1990 ni sawa na ya sasa...? heshima ya Kikwete ya Mwaka 2005 ni sawa na ya sasa
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kitampa rais Kikwete siku tisa baada ya kumaliza mzunguko wake wa kwanza wa kuwahamasisha wananchi mikoani.

“Rais Kikwete tunakwenda naye kwa stepu, tutawasha moto wa maandamano nchi nzima, tukimaliza tutaangalia kama atakuwa amechukua hatua. Tutampa siku tisa,” alisema Mbowe na kushangiliwa.

Dk. Slaa aliyekuwa wa kwanza kuhutubia katika mkutano huo, alisisitiza sana msimamo wa chama hicho kumpa Rais Kikwete siku tisa za kuhakikisha anaondoa kodi kwenye maeneo yote yaliyosababisha bei za vyakula na bidhaa mbalimbali kupanda na kufanya maisha ya wananchi kuwa magumu.

My take: Is a 9-day strategy a coincidence, planned?, na je baada ya siku hizo tisa nini kitafuata. This is a serious note, wasiwasi wangu wasije kuwa wamekurupuka kusema siku tisa.

Ndugu wana JF hivi kuna ulazima wa kiongozi wa chama hasa nafasi ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa Keundelea kuvuta Bangi?
 
Ifikie kipindi Watanzania waelewe kuwa 'peace is more than the absence of war'
Tusidanganywe na amani na hali kuna njaa na umasikini wa kutupwa nchini huku hao wanaosema 'amani' wanakula keki ya Taifa wao na familia zao tuu.

Umejaribu kuelezea nini maana ya amani kwa mtizamo wako!
 
Ndugu wana JF hivi kuna ulazima wa kiongozi wa chama hasa nafasi ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa Keundelea kuvuta Bangi?
Hata Obama alivuta na ninaamini bado anavuta ingawa alisema ameacha. Ile kitu ukishaianza si rahisi kuiacha. Ni sawasawa na kula nyama ya mtu.
 
wewe ni mpuuuzi ambaye huna tv wala redio kwako maana hatua zilizochukuliwa nchi zingine wewe hujaziona unabaki kushangaa. angalia umati wa jana then ndo uulize hatua ambazo wanaweza kuzichukua. bado uko kwenye TANU??

Mkuu umeenda mbali sana, na watu kama wewe ndo wanatusumbua na 4sure hawana future nzuri na taifa. Kabla hujaandamana kudai mabadiliko jiangalie wewe mwenyewe how you have changed. Usidai mabadiliko hali ya kuwa wewe mwenyewe huna maadili hayo. Hao uliowaweka mbele kama viongozi wa kukuletea mabadiliko can you tell me how they have changed their atitude. Mtu mhuni siku zote mawazo yake yatakuwa ya kihuni.

Je wanasheria wetu sheria walikuwa wanazisoma kwa kuzielewa au kukariri? wakati wabunge wakiilazimisha serikali ivunje mkataba na DOWANS walikuwa hawajui madhara yake? Haifai kuangalia tulipoangukia tu bali tuangalie wapi tulipojikwaa.

Hii ni impact ya jamii kutokufundishwa maadili ndo maana yote haya yanajitokeza.
 
Mishahara haitoshi? Hivi ushajiuliza wa Tanzania wangapi wanalipa kodi ipasavyo? Sasa chukuwa kodi inayolipwa kwa sasa halafu igawe kwenye hiyo mishahara uitakayo halafu uone zinabaki kiasi gani za kuliendesha taifa.

Nna uhakika njia mbadala zinazobuniwa na Serikali, kama vituo vya veta, kilimo kwanza, kuhamasisha ujasiriamali ndiko suluhisho la mishahara midogo.

Hivi hata ukiingia mitaani ndio mshahara utapanda? Unaweza ukapandishiwa mshahara wa kiini macho, yaani mshahara upande na thamani ya fedha ishuke sana na iwe afadhali ya huo mshahara mdogo kuliko kuwa na mipesa mingi isiyo na faida.

Hivi leo tunaona jitihada za Serikali kwa kuanzisha benki za wakulima, mortgage, pembejeo, mabara-bara, mashule, veta na kadhalika. Mambo hayo yote yanalenga kustimulate uchumi, na ndio njia ya kukuza kipato.

Usijidanganye kuwa kuingia mitaani ndio suluhisho, hasara zake ni kubwa kuliko unavyofikiria.

Haya ni yakweli kabisa ambaye haoni basi ni ushabiki ndo utamponza, lakini pamoja na haya bado hasira ya wananchi raia wa kawaida kama mimi ni kuona wezi wa fedha za umma wanaendelea kustarehe mitaani na kupongezwa kama heroes. Kwangu mimi JK amejitahidi sana ku improve democracy na kuanzisha cash facilities kama microfinancing schemes ambazo zimepunguza kwa kiasi kikubwa shida ya hasa wafanyakazi wa serikali lakini matunda ya haya yote yanashindwa kuonekana kutokana na udhibiti wa wizi in various ways katika hizo hizo schemes. Angejitahidi sasa ili kuzima haya yote ambayo yako most likely kutokea kwa ku punish wote walilifikisha taifa katika ngazi hii ya kutokuwajibika kwa public.

Ugumu wa hili jambo ni kuwa elites wote wameingia katika huu mfumo wa wizi usio rasmi kwahiyo ukimwajibisha mmoja chain inamgusa mpaka yule wa chini, which is also dengerous kwa kiongozi wa nchi maana wenye genuine reasons za kumlaumu na wale ambao ndiyo main actors wata join hands kuenda against him....Swali kwa wote ambao tunaenda kwa ushabiki ingekuwa wewe ndo rais wa Tanzania ungefanyaje?

Elites acheni ushabiki na unafiki do your part, msaidieni Rais kusolve haya mambo you are the main actors hata kama mtamnyooshea yeye kidole kimoja vitatu vina rudi kwenu...Actually we are the most likely kuwa disgraced kuliko mtu yeyote if this country itafikia hatua ambayo wengi tunashabikia ifikie. Mpeni Rais good advice akikataa damu ya taifa hili itakuwa juu yake. Otherwise huu ni uonevu wa wazi kwa mtu ambaye dhamira yake ni njema kwa Taifa hili kwani ameonyesha mara kadhaa ku yield into your demands, wafanyakazi tulitishia kugoma, akaongeza mishahara mara mbili, sera zingine za CHADEMA amezi adopt, swala la katiba hata kama halikua ndani ya Ilani ya chama chake ame take risk na kulikubali...A president is not strong because of His strength but because of His people....the weakness we are now seing is in most of the case contributed by us elites....Mseme mtakachosema I will remain true to myself and to my God for I fear nobody but respect every humanity!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Hakuna kingozi aliekaa madarakani Tanzania kwa miaka hamsini. Maximum ni miaka kumi na ni kwa ridhaa ya wananchi.

Chadema, si wajipange na kuchukuwa madaraka kihalali kwa kupigiwa kura na asilimia kubwa ya wananchi?

Nani aliekaa madarakani Tanzania muda mrefu zaidi ya Nyerere? Nae alileta maendeleo yepi zaidi ya kutufanya masikini wa kutupwa?

We kweli maji MSHINDO kama N***E mshindo! CDM wachukue vipi madaraka kihalali wakati kura zinachakachuliwa??? madaraka aliechukua KJ mwezi octoba mwaka jana yalikuwa ya kihalali??????? Kaa kimya if you have nothing to say!
 
[watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifaQUOTE=Majimshindo;1665664]Ndio nini?[/QUOTE]
 
Haya ni yakweli kabisa ambaye haoni basi ni ushabiki ndo utamponza, lakini pamoja na haya bado hasira ya wananchi raia wa kawaida kama mimi ni kuona wezi wa fedha za umma wanaendelea kustarehe mitaani na kupongezwa kama heroes. Kwangu mimi JK amejitahidi sana ku improve democracy na kuanzisha cash facilities kama microfinancing schemes ambazo zimepunguza kwa kiasi kikubwa shida ya hasa wafanyakazi wa serikali lakini matunda ya haya yote yanashindwa kuonekana kutokana na udhibiti wa wizi in various ways katika hizo hizo schemes. Angejitahidi sasa ili kuzima haya yote ambayo yako most likely kutokea kwa ku punish wote walilifikisha taifa katika ngazi hii ya kutokuwajibika kwa public.

Ugumu wa hili jambo ni kuwa elites wote wameingia katika huu mfumo wa wizi usio rasmi kwahiyo ukimwajibisha mmoja chain inamgusa mpaka yule wa chini, which is also dengerous kwa kiongozi wa nchi maana wenye genuine reasons za kumlaumu na wale ambao ndiyo main actors wata join hands kuenda against him....Swali kwa wote ambao tunaenda kwa ushabiki ingekuwa wewe ndo rais wa Tanzania ungefanyaje?

Elites acheni ushabiki na unafiki do your part, msaidieni Rais kusolve haya mambo you are the main actors hata kama mtamnyooshea yeye kidole kimoja vitatu vina rudi kwenu...Actually we are the most likely kuwa disgraced kuliko mtu yeyote if this country itafikia hatua ambayo wengi tunashabikia ifikie. Mpeni Rais good advice akikataa damu ya taifa hili itakuwa juu yake. Otherwise huu ni uonevu wa wazi kwa mtu ambaye dhamira yake ni njema kwa Taifa hili kwani ameonyesha mara kadhaa ku yield into your demands, wafanyakazi tulitishia kugoma, akaongeza mishahara mara mbili, sera zingine za CHADEMA amezi adopt, swala la katiba hata kama halikua ndani ya Ilani ya chama chake ame take risk na kulikubali...A president is not strong because of His strength but because of His people....the weakness we are now seing is in most of the case contributed by us elites....Mseme mtakachosema I will remain true to myself and to my God for I fear nobody but respect every humanity!
Yaani umezungumza hadi nikaanza kumuonea huruma Kikwete lakini nilipojiuliza tena ni nani anayewaruhusu hao wanaomfanya aonekane hajui kazi jibu likawa ni weakness yake.
 
hakuna kingozi aliekaa madarakani tanzania kwa miaka hamsini. Maximum ni miaka kumi na ni kwa ridhaa ya wananchi.

Chadema, si wajipange na kuchukuwa madaraka kihalali kwa kupigiwa kura na asilimia kubwa ya wananchi?

Nani aliekaa madarakani tanzania muda mrefu zaidi ya nyerere? Nae alileta maendeleo yepi zaidi ya kutufanya masikini wa kutupwa?

kodi tu jamani:a s 13:
 
We kweli maji MSHINDO kama N***E mshindo! CDM wachukue vipi madaraka kihalali wakati kura zinachakachuliwa??? madaraka aliechukua KJ mwezi octoba mwaka jana yalikuwa ya kihalali??????? Kaa kimya if you have nothing to say!

Kama matokeo yalichakachuliwa Dr Slaa aliibiwa kura kiasi gani? Usilete stori za vijiweni!
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

unawashauri wenzio wakuze tatizo!? swala si cdm bali ni ukweli. dawa ya jino ni kulitoa na si kumeza panadol. wakizuia ndo wanakuza. conflict hazikwepeki na zipo kila siku. dawa yake ni kuzijadili kwa heshima na uwazi na si kudharau upande wowote. ccm ina tatizo la viongozi wake wengi kukariri nyakati za zamani. wanapaswa kubadilika na kwenda na wakati. watu wamebadilika na dunia imebadilika so the problem isnt cdm or watanzania. they are just showing that we have problem somewhere na wa kulimaliza ni ccm na uongoziwake kukubali kuheshimu mawazo ya wengi and so for. ccm hata kama ikishindwa but kwa heshima itakuwa na muda wa kujijenga na si kutumia mabavu then ikashindwa haitakuwa na wa kuiheshimu tena. kama kanu vile. the reason why baba wa taifa anaheshimika na hata mzee madiba ni uwezo wao wa kufikiri na kuona mbele na wakatoka kwa kuwa dunia ilichange na hawangeweza kugeuka majiwe. mtu unatakiwa ukamatilie unachoamini na ukiona wengi wako upande mwingine then waachie na ubaki na heshima yako. haya ni mawazo yangu. usiangalie cdm balh walioko nyuma yake. wanataka mabadiliko waachwe kwa amani then later wanaweza rudi. na ndo maana kwa wenzetu this time democrat next yaweza kuwa republican. kwa heshima.
 
japo wanaashiria uvunjifu wa amani...serikali nayo iangalie madai kama ni ya msingi.....!

siyo uvunjifu wa amani kuandamana jamani. mbona marekani watu huandamana hadi ikulu na hawapigwi mabomu ndugu zangu? watu wanapeleka meseji zao kwa amani waachwe na wasikilizwe na utekelezaji ufuatie. amani itoke wapi na njaa jamani? kila kitu juu. road license to kasheshe. mafuta ya magari usipime, sukari mchele na kila kitu juu. watu wakae kimya? tufumbue macho ndugu zangu. mimi nasikitika sana serikali kufumbia macho mfumuko wa bei kwani ndo tunazidi kuwa masikini. serikali itafute pa kupatia mapato na si kujisifu mapato yameongezeka kwa kuongeza bei ya vitu muhimu.
 
Mishahara haitoshi? Hivi ushajiuliza wa Tanzania wangapi wanalipa kodi ipasavyo? Sasa chukuwa kodi inayolipwa kwa sasa halafu igawe kwenye hiyo mishahara uitakayo halafu uone zinabaki kiasi gani za kuliendesha taifa.

Nna uhakika njia mbadala zinazobuniwa na Serikali, kama vituo vya veta, kilimo kwanza, kuhamasisha ujasiriamali ndiko suluhisho la mishahara midogo.

Hivi hata ukiingia mitaani ndio mshahara utapanda? Unaweza ukapandishiwa mshahara wa kiini macho, yaani mshahara upande na thamani ya fedha ishuke sana na iwe afadhali ya huo mshahara mdogo kuliko kuwa na mipesa mingi isiyo na faida.

Hivi leo tunaona jitihada za Serikali kwa kuanzisha benki za wakulima, mortgage, pembejeo, mabara-bara, mashule, veta na kadhalika. Mambo hayo yote yanalenga kustimulate uchumi, na ndio njia ya kukuza kipato.

Usijidanganye kuwa kuingia mitaani ndio suluhisho, hasara zake ni kubwa kuliko unavyofikiria.

To me jitihada hazipo ni ubabaishaji tu. nchi haina viongozi wenye macho yaliyo sahihi. kama wameacha wananchi wake wanakopa benki kama barclayz na wanalipa riba ya 23 to 25 pct wakati huko ilikotoka benki hiyo nadhani hata pcnt 10 ya riba haifiki na wako kimya unadhani tuna viongozi wenye kuona mbele? mfanyakazi akope m 10 alipe m 9. is i possible kumtoa kwenye umasikini?
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

The most amazing aspect of human thought processes is the ability to deliberately shut out reality!
 
Mi ningekuwa wao nisingesubiri kuaibika. ningewakabidhi nchi na kuona wanafanyaje. kulazimisha kuongoza nchi hii kwa sasa ni kujitafutia presha na kasheshe zisizo za lazima. labda kama una maslahi binafsi. ni kama kukimbiza mbio za vijiti. ukichoka mwenzio achukua na mwisho hulaumiwi sana kama kulazimisha mwenyewe na lawama zikawa zako pekee.
 
Its a god move! lets push on mpaka kieleweke, wameanza na sukari then umeme, gas, vyakula, cement nondo mabati and others will follow..!! Hii inflation ya sasa inatisha sijui hao wachumi wanaowashauri wamewakodi nini?? Im sure sio watanzania caz they dont wish us good..!! So dawa yao is to chase them out kwa speed mara mbili ya watunisia....!!:spider:
 
Huo umma unaousema wewe ndio kwa asilimia kubwa waliichaguwa simu kuendelea kuwaongoza, toka ngazi za udiwani mpaka wabunge, mpaka Rais.

Hebu nambie, madiwani na wabunge Tanzania wepi ni wengi? Jibu utalopata basi ujuwe bado mna kazi ya kufanya. Na hao wachache wanaowaunga mkono mtawakosa kabisa kwa siasa zenu zenu za uchokozi na uvunjifu wa amani. Na kama hamuijuwi peoples power ya kweli basi ngojeni siku wapenda amani tutapocharuka na kuwavamia mitaani, hapo ndio mtajuwa maana ya "peoples power".

Umma haukuichagua CCM, vyombo vya kusimamia uchaguzi vya CCM ndo vilivyoichagua. Huo umati wa watu wanaounga mkono maandamano ya kupinga wizi na udhalimu wa CCM unatuthibitishia hilo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom