Chadema wampa Kikwete 'siku tisa'

Chadema wampa Kikwete 'siku tisa'

Mbona hueleweki sema moja tukuelewe wachukuliwe hatua au wapuuzwe, unawaogopa wakati huo huo unajifanya mkali.

Wapuuzwe kwa hizo siku tisa walizotowa, kwa sababu tu, ya kuona watafanya nini? Baada ya hizo siku tisa, wakileta uvunjifu wa amani, wachukuliwe hatua kali sana.
 
Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.
Msekwa yuko madarani nafikiri kabla Zitto hajazaliwa hivi yeye huoni kama ana uchu wa madaraka LOL!.
 
Well, nadhani hilo liko wazi kuwa awamu ya kwanza ya maandamano itadumu kwa siku kumi. Maana yake ni siku ya tisa kuanzia leo. Baada ya hapo kitaendelea kingine kwa hiyo usitilie shaka hizo siku 9. Cha msingi ungejiuliza wewe mwenyewe kuwa utafanya nini baada ya hizo siku 9 kuisha wakati maisha yakiendelea kuwa magumu? Je, utaungana na watakachofanya wao au utakataa?

Pili, sijui kama kuna mtu au kiongozi CDM mwenye akili ya kukurupuka. Hakuna cha kuwa kurupusha kwani mipango ya maandamano haya ilianza tangu mwaka jana sasa kwa nini wafanye hivyo? Naomba tu mr. Luteni uwaze cha kuwafanyia watanzania wa leo na vizazi vijavyo kwani hatima ya nchi yetu hiko mikononi mwetu. Tushirikiane!!

Maisha magumu wakati saa hizi upo kwenye mtandao una bofya? Unashangaza sana!
 
jana tu wameondoa kodi ya sukari na kuamuru sukari ishuke.......

chadema iko juuu
 
Hapa Chadema wame kurupuka na ndiyo maana mimi sikioni bado Chadema kama chama mbadala. Hiyo kauli ya "siku tisa" haionekani kama ili jadiliwa na uongozi wa chama. Inaelekea Mbowe alitoa kauli hiyo at the spur of the moment. Ndiyo hapo Chadema wanapo nipa wasi wasi. Mara nyingi wana achia hisia zichukue nafasi. Hisia wawaachie wananchi wap wafanye vitu kwa kupanga.

1. Siku tisa hazi toshi kuonyesha mafanikio ya sera fulani. Hata serikali ifute kodi hizo sasa hivi hatu wezi kuona unafuu baaada ya siku tisa tu. It's just not possible!

2. Chadema wame toa bluff ambayo they can not follow through. Mark my words baada ya siku tisa kita kacho tokea labda ni maendelezo ya maandamano tu.

3. Kabla hawaja tishia maandamano makubwa wapite kwanza nchi nzima na kuendelea kupata support ya wananchi. Inaelekea Chadema kina haraka sana. Sawa hali imekua mbaya zaidi ila kama chama cha siasa lazima wawe strategic.

Anyway pongezi kwa Chadema. Nadhani wakiendelea wata kuwa chombo kizuri cha kupressure serikali.
 
jana tu wameondoa kodi ya sukari na kuamuru sukari ishuke.......

chadema iko juuu

Halafu mnasema hawafanyi kitu? Au ndio unazuga kuwa imeshuka baada ya maandamano ya Chadema.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kitampa rais Kikwete siku tisa baada ya kumaliza mzunguko wake wa kwanza wa kuwahamasisha wananchi mikoani.

“Rais Kikwete tunakwenda naye kwa stepu, tutawasha moto wa maandamano nchi nzima, tukimaliza tutaangalia kama atakuwa amechukua hatua. Tutampa siku tisa,” alisema Mbowe na kushangiliwa.

Dk. Slaa aliyekuwa wa kwanza kuhutubia katika mkutano huo, alisisitiza sana msimamo wa chama hicho kumpa Rais Kikwete siku tisa za kuhakikisha anaondoa kodi kwenye maeneo yote yaliyosababisha bei za vyakula na bidhaa mbalimbali kupanda na kufanya maisha ya wananchi kuwa magumu.

My take: Is a 9-day strategy a coincidence, planned?, na je baada ya siku hizo tisa nini kitafuata. This is a serious note, wasiwasi wangu wasije kuwa wamekurupuka kusema siku tisa.
Hicho ndicho tulichokuwaq tunasubiria sasa ole wao ccm wasipotekeleza ndani ya hizo cku tisa nadhani umati wa jana wameuona
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Wacha kutoka mapovu wewe. Uandishi wako tu unaonesha tayari mnatishika wewe na ccm yako. Kama wewe una amani..mimi hiyo amani sina maana siwezi tena kumudu kilo ya sukari. Kama ni machafuko na yaje tumechoka amani kwenye dimbwi la umasikini. Si bora tuwe Somalia tu ili walimwengu wajue sisi ni masikini kwa sababu ya vita kuliko kuwa masikini ndani ya utulivu tele!

Miaka 50 ya kuwa na amani ccm wameshindwa kushinda umasikini naona tuwape miaka 100 ya vita labda wataweza!
 
Mishahara haitoshi? Hivi ushajiuliza wa Tanzania wangapi wanalipa kodi ipasavyo? Sasa chukuwa kodi inayolipwa kwa sasa halafu igawe kwenye hiyo mishahara uitakayo halafu uone zinabaki kiasi gani za kuliendesha taifa.

Nna uhakika njia mbadala zinazobuniwa na Serikali, kama vituo vya veta, kilimo kwanza, kuhamasisha ujasiriamali ndiko suluhisho la mishahara midogo.

Hivi hata ukiingia mitaani ndio mshahara utapanda? Unaweza ukapandishiwa mshahara wa kiini macho, yaani mshahara upande na thamani ya fedha ishuke sana na iwe afadhali ya huo mshahara mdogo kuliko kuwa na mipesa mingi isiyo na faida.

Hivi leo tunaona jitihada za Serikali kwa kuanzisha benki za wakulima, mortgage, pembejeo, mabara-bara, mashule, veta na kadhalika. Mambo hayo yote yanalenga kustimulate uchumi, na ndio njia ya kukuza kipato.

Usijidanganye kuwa kuingia mitaani ndio suluhisho, hasara zake ni kubwa kuliko unavyofikiria.

Hasara gani? wakati sasa hivi tunasumbuliwa na haya mafisadi na ni bora tuyaue maana yanatunyonya sasa hiyo hasara unayoizungumzia labda ni kwako unaokula na mafisadi mkuu! Sorry buddy!!
 
Hivi leo tunaona jitihada za Serikali kwa kuanzisha benki za wakulima, mortgage, pembejeo, mabara-bara, mashule, veta na kadhalika. Mambo hayo yote yanalenga kustimulate uchumi, na ndio njia ya kukuza kipato.
Kwa data zako nafikiri mwaka kesho UK watatusikia redioni, kwa taarifa yako hizo ni nyimbo tu za redioni eti kilimo kwanza kimemnufaisha nani, mortgage bila kuwa na raslimali benki gani itakuamini, tunachoongelea hapa ni mwananchi wa kijijini ambye hajui kesho atakula nini.
 
Wacha kutoka mapovu wewe. Uandishi wako tu unaonesha tayari mnatishika wewe na ccm yako. Kama wewe una amani..mimi hiyo amani sina maana siwezi tena kumudu kilo ya sukari. Kama ni machafuko na yaje tumechoka amani kwenye dimbwi la umasikini. Si bora tuwe Somalia tu ili walimwengu wajue sisi ni masikini kwa sababu ya vita kuliko kuwa masikini ndani ya utulivu tele!

Miaka 50 ya kuwa na amani ccm wameshindwa kushinda umasikini naona tuwape miaka 100 ya vita labda wataweza!

Umasikini wako ni ufinyu wa mawazo na ubunifu ulionao.

Hivi ni nini kinakuzuia kuondoka kwenye umasikini?

Kama huna ubunifu hata aje Mbowe hatoweza kukutowa kwenye umasikini huo. Yeye mwenyewe kashindwa kuendeleza mali za ufisadi alizorithi kwa babake, mpaka tunasikia zinazuiliwa kwa madeni, sasa huyo anaeshindwa kuendeleza mali ya urithi kweli ataweza kukuendeleza wewe masikini? Unashangaza sana.
 
Hata watoto wa Mubarak na Gadaffi waliuliza swali hili sembuse wewe usiye na jeshi kama Gamal Mubarak.

Nadhani huna hoja. Au kwa akili yako Chadema ndio italeta maajabu na kuwatoa watu kwenye umasikini kwa siku moja? Unadanganywa na unadanganyika.
 
Maisha magumu wakati saa hizi upo kwenye mtandao una bofya? Unashangaza sana!
Na wasiwasi na uelewa wako unafikiri maisha bora ni kukaa kwenye komputa hutofautiani na akili za rais wako eti foleni ni dalili za maisha bora.
 
Hebu soma kwenye red nafikiri utapata jibu.
3. Kabla hawaja tishia maandamano makubwa wapite kwanza nchi nzima na kuendelea kupata support ya wananchi. Inaelekea Chadema kina haraka sana. Sawa hali imekua mbaya zaidi ila kama chama cha siasa lazima wawe strategic.

Anyway pongezi kwa Chadema. Nadhani wakiendelea wata kuwa chombo kizuri cha kupressure serikali.


"Rais Kikwete tunakwenda naye kwa stepu, tutawasha moto wa maandamano nchi nzima, tukimaliza tutaangalia kama atakuwa amechukua hatua. Tutampa siku tisa," alisema Mbowe na kushangiliwa.
 
Umefika wakati tabia ya kuwabembeleza viongozi wa serikali hii ya kifisadi ikome. Tuwaambie specifically tunataka nini, uwezo wa kuyafanya hayo upo ila kwao si priority.

Sasa imefika mwisho, mifano tumeiona, Tunisia, Misri na sasa Libya. Nadhani sisi ndio tulitakiwa kuanza because we are not at all better than those countries. Wao wametuonyesha mifano halisi kuwa nguvu ya umma ni nguvu ya Mungu.

Kikwete na serikali yako amka usingizini (i am not sure about that), mkiendelea kulala na kutosoma alama za nyakati mjue kuwa wenye nchi yao (wananchi) wataitaka ili wajiletee maendeleo wanayoyahitaji.

Tumenyonywa vya kutosha, tumenyanyaswa vya kutosha, tumedhulumiwa vya kutosha sasa tunasema THIS MUST STOP NOW!!
 
Mishahara haitoshi? Hivi ushajiuliza wa Tanzania wangapi wanalipa kodi ipasavyo? Sasa chukuwa kodi inayolipwa kwa sasa halafu igawe kwenye hiyo mishahara uitakayo halafu uone zinabaki kiasi gani za kuliendesha taifa.

Nna uhakika njia mbadala zinazobuniwa na Serikali, kama vituo vya veta, kilimo kwanza, kuhamasisha ujasiriamali ndiko suluhisho la mishahara midogo.

Hivi hata ukiingia mitaani ndio mshahara utapanda? Unaweza ukapandishiwa mshahara wa kiini macho, yaani mshahara upande na thamani ya fedha ishuke sana na iwe afadhali ya huo mshahara mdogo kuliko kuwa na mipesa mingi isiyo na faida.

Hivi leo tunaona jitihada za Serikali kwa kuanzisha benki za wakulima, mortgage, pembejeo, mabara-bara, mashule, veta na kadhalika. Mambo hayo yote yanalenga kustimulate uchumi, na ndio njia ya kukuza kipato.

Usijidanganye kuwa kuingia mitaani ndio suluhisho, hasara zake ni kubwa kuliko unavyofikiria.

I'm convinced 100% kwamba majimshindo ni malaria sugu or from same blood line na si vinginevyo. Huu upupu unaoandika hapa please upeleke some place else. Mbona uko shallow hivyo? Kodi unayoijuwa wewe ni ile direct tax pekee ambayo ni sehemu ndogo sana ya real tax. Kwa taarifa yako watanzania wote wanalipa kodi tena kubwa sana kwani almost kila kitu kiko taxed. Unataka kusema huoni namna serikali hii ya nchi maskini duniani inavyoendeshwa kwa gharama kubwa zisizo na sababu? Na huoni ufisadi wa kutisha unaofanywa kila kona? Umejaribu kutafakari kwamba tungeziba hiyo mianya serikali ingeshindwa kutimiza majukumu yake ya kutoa huduma? Guys lets not waste our time responding to this nonsense.
 
Back
Top Bottom