Chadema wampa Kikwete 'siku tisa'

Chadema wampa Kikwete 'siku tisa'

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
303
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kitampa rais Kikwete siku tisa baada ya kumaliza mzunguko wake wa kwanza wa kuwahamasisha wananchi mikoani.

"Rais Kikwete tunakwenda naye kwa stepu, tutawasha moto wa maandamano nchi nzima, tukimaliza tutaangalia kama atakuwa amechukua hatua. Tutampa siku tisa," alisema Mbowe na kushangiliwa.

Dk. Slaa aliyekuwa wa kwanza kuhutubia katika mkutano huo, alisisitiza sana msimamo wa chama hicho kumpa Rais Kikwete siku tisa za kuhakikisha anaondoa kodi kwenye maeneo yote yaliyosababisha bei za vyakula na bidhaa mbalimbali kupanda na kufanya maisha ya wananchi kuwa magumu.

My take: Is a 9-day strategy a coincidence, planned?, na je baada ya siku hizo tisa nini kitafuata. This is a serious note, wasiwasi wangu wasije kuwa wamekurupuka kusema siku tisa.
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.
 
kaka usiulize maisha sasa hivi magumu sana, after nine days tunaingia mtaani. mishahara haitoshi kabisa, kweli acha kwanza waangalie response ya wenzetu sehemu zingine kama ni nzuri kama ya jana then tunamtoa madarakani. Siumeona jamaa wameogopa sasa hivi wanashusha bei ya sukari? hii haijatokea kwa bahati mbaya ni wana-interejensia walijua nini kitaongelewa. kweli wasipotekeleza wanatoka madarakani.
 
Well, nadhani hilo liko wazi kuwa awamu ya kwanza ya maandamano itadumu kwa siku kumi. Maana yake ni siku ya tisa kuanzia leo. Baada ya hapo kitaendelea kingine kwa hiyo usitilie shaka hizo siku 9. Cha msingi ungejiuliza wewe mwenyewe kuwa utafanya nini baada ya hizo siku 9 kuisha wakati maisha yakiendelea kuwa magumu? Je, utaungana na watakachofanya wao au utakataa?

Pili, sijui kama kuna mtu au kiongozi CDM mwenye akili ya kukurupuka. Hakuna cha kuwa kurupusha kwani mipango ya maandamano haya ilianza tangu mwaka jana sasa kwa nini wafanye hivyo? Naomba tu mr. Luteni uwaze cha kuwafanyia watanzania wa leo na vizazi vijavyo kwani hatima ya nchi yetu hiko mikononi mwetu. Tushirikiane!!
 
Safi sana! Ni vyema wakifanya kazi na deadline badala ya kufanya tuuuu maandamano na mikutano. Kama wangekuwa wamekurupuka wangesema siku 3 au 5.. lkn nadhani wana ratiba ya kila siku. Baada ya siku 9, moto utawaka mkubwa zaidi kwani wananchi wengi zaidi watataka kujiunga na maandamano na kuhudhuria mikutano! Ni strategy nzuri, hebu tuone sasa strategy ya CCM na JK...
 
japo wanaashiria uvunjifu wa amani...serikali nayo iangalie madai kama ni ya msingi.....!
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

wewe ni mpuuuzi ambaye huna tv wala redio kwako maana hatua zilizochukuliwa nchi zingine wewe hujaziona unabaki kushangaa. angalia umati wa jana then ndo uulize hatua ambazo wanaweza kuzichukua. bado uko kwenye TANU??
 
Na kwa taarifa yako wameanza kutekeleza matakwa ya chadema sukari imeshuka bei wametoaagizo jana. harafu unauliza nini sasa?
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

wewe ni Topical
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

we majimshindo,,kama chadema hawatutakii mema ccm ndo inatutakia mema?
 
Good move CDM tumeanza kuona matunda ya maandamano wametangaza kushusha bei ya sukari bado umeme, cement, mabati na nondo, big up kwa pressure hiyo hata wanaobeza watafaidika.
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Kuna mema gani sasa Tanzania? Unaona bidhaa zilivyo panda bei na maisha yalivyo magumu wakati huyo mwizi wa kura yupo kwenye ndege nje ya nchi kutatua matatizo ya uongo huko Ivory Coast. Uache kuwa na maneno yasio na nyuma wala mbele. Nyie ndio mme fanya mama yangu na baba yangu kuendelea kupata shida. Unafikiri mimi nipo kusubiri ufisadi unimalize kama wewe....upotofu wa hali juu kukaa nyumbani na kufikiria Tanzania kuna "mema" na "amani" wakati wananchi hawana vyakula wala kazi. Unataka watanzania waishi vipi? Tuanze kuwa refegees Somalia au Ethiopia (AU)?
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Kumbe na wewe ni pimbi kichwani? Si lazima kuchangia vitu ambavyo ni juu ya uelewa wako.
 
Kama wamempa siku tisa they should take it on a serious note wasiishie kuongea tu.
 
japo wanaashiria uvunjifu wa amani...serikali nayo iangalie madai kama ni ya msingi.....!

Ina maana wewe hujui madai ya msingi ni yapi mpaka serikali iangalie? Duh! Tutafika kweli.
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Mbona hueleweki sema moja tukuelewe wachukuliwe hatua au wapuuzwe, unawaogopa wakati huo huo unajifanya mkali.
 
Chadema hawataitakii mema Tanzania yetu.

Kauli zao na vitendo vyao vyote vinaonesha kuashiria fujo, uvunjifu wa amani na uchu wa madaraka
.

Hivi wana ubavu gani wa kuitisha Serikali?

Mini naiasa Serikali ya Tanzania. Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Hawa viongozi wa Chadema wachululiwe hatua kali za kisheria kwa kauli zao za uvunjifu wa amani ili wasituletee fujo na uvunjifu wa amani.

Siku tisa? Wana maana gani siku tisa? Na kwa sasa, Serikali iwapuuze kwa hayo maneno yao, na ione baada ya hizo siku tisa wamekusudia nini? Wakianzisha uvunjifu wa amani au chokochoko zinazoashiria uvunjifu wa amani baada ya siku hizo tisa, basi wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Kwa hiyo uchu wa madaraka ni kwa CDM tu u sio, na hao waliokaa madarakani miaka 50 maendeleo hakuna na wanachakachua kura ili waendelee kutawala wana uchu wa nini? acha uvivu wa kufikiri.
 
Ina maana wewe hujui madai ya msingi ni yapi mpaka serikali iangalie? Duh! Tutafika kweli.
Kumbe na wewe umegundua, mijitu mingine haijui hata madai yao ya msingi yanasubiri hadi yaambiwe na Pinda.
 
kaka usiulize maisha sasa hivi magumu sana, after nine days tunaingia mtaani. mishahara haitoshi kabisa, kweli acha kwanza waangalie response ya wenzetu sehemu zingine kama ni nzuri kama ya jana then tunamtoa madarakani. Siumeona jamaa wameogopa sasa hivi wanashusha bei ya sukari? hii haijatokea kwa bahati mbaya ni wana-interejensia walijua nini kitaongelewa. kweli wasipotekeleza wanatoka madarakani.

Mishahara haitoshi? Hivi ushajiuliza wa Tanzania wangapi wanalipa kodi ipasavyo? Sasa chukuwa kodi inayolipwa kwa sasa halafu igawe kwenye hiyo mishahara uitakayo halafu uone zinabaki kiasi gani za kuliendesha taifa.

Nna uhakika njia mbadala zinazobuniwa na Serikali, kama vituo vya veta, kilimo kwanza, kuhamasisha ujasiriamali ndiko suluhisho la mishahara midogo.

Hivi hata ukiingia mitaani ndio mshahara utapanda? Unaweza ukapandishiwa mshahara wa kiini macho, yaani mshahara upande na thamani ya fedha ishuke sana na iwe afadhali ya huo mshahara mdogo kuliko kuwa na mipesa mingi isiyo na faida.

Hivi leo tunaona jitihada za Serikali kwa kuanzisha benki za wakulima, mortgage, pembejeo, mabara-bara, mashule, veta na kadhalika. Mambo hayo yote yanalenga kustimulate uchumi, na ndio njia ya kukuza kipato.

Usijidanganye kuwa kuingia mitaani ndio suluhisho, hasara zake ni kubwa kuliko unavyofikiria.
 


Kwa hiyo uchu wa madaraka ni kwa CDM tu u sio, na hao waliokaa madarakani miaka 50 maendeleo hakuna na wanachakachua kura ili waendelee kutawala wana uchu wa nini? acha uvivu wa kufikiri.


Hakuna kingozi aliekaa madarakani Tanzania kwa miaka hamsini. Maximum ni miaka kumi na ni kwa ridhaa ya wananchi.

Chadema, si wajipange na kuchukuwa madaraka kihalali kwa kupigiwa kura na asilimia kubwa ya wananchi?

Nani aliekaa madarakani Tanzania muda mrefu zaidi ya Nyerere? Nae alileta maendeleo yepi zaidi ya kutufanya masikini wa kutupwa?
 
Back
Top Bottom