CHADEMA wamfungulia kesi Nape

Haki sawa

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2007
Posts
4,781
Reaction score
3,211
Kutokana na vyanzo vyangu vilivyopo Mahakama kuu ya Tanzania Leo Nape amefunguliwa kesi ya madai na imepewa namba 186 ya mwaka 2012.

Kesi hii ni kuhusiana na madai ya nnape kuwa CDM wana pokea pesa kutoka nje ya nchi.

Tuendelee kufuatilia


Updates.

Inaitwa civil case no.186 of 2012 ,board of registered trustees of chadema ... Plaintiff versus nnape nnauye defendant .

 
Aliyataka mwenyewe sasa athibitishe.Wapambe wake wote kama mchemba wataingia mitini.
 
Patamu hapo. Kazi kwake mropokaji.
 
Anasimama na Lissu Mahakamani pembeni kuna Prof.Safari au kuna kitu gani kwa upande wa Chadema ? Na hii ndiyo watanzania watajua kwamba Chadema wako serious sasa .Komesha kuropoka bila ushahidi .Marando am sure hatakosa hapa kuongoza kuutafuta ukweli .
 
Ni wakati wa Chadema kuumbuka. Nape atakuja na ushahidi wa kutosha.
 
Aisee hapa ndipo mahala sahihi wa yeye kuwaeleza waTZ ukweli kama alivyosema. Nape uwanja ni wako thibitisha tunakusubiri!!!
 
Tundu A. Lissu, Prof. Safari, Mabere Nyaucho Marandu etc. Je CCM watamlipia hizo Billion 3?
 
Ana udhibitisho, atatoa mahakamani kama alivyosema tusubiri
 
Mahakama ni yao, na hivi tena majaji wapya walioteuliwa na mwenyekiti wa ccm taifa na alishawapa maelekezo mpya ya maslahi ya ccm mbele! Uh!
 
Nape imefka wakat muafaka udhbitshe ukwel kama kesi imeshafunguliwa! Ukishndwa ujue wewe n full vuvuzela la nyinyiem
 
Hii kesi inaweza kuwa ngumu sana kwa upande wa Nape kwa sababu kwenye madai yake (yeye Nape) ni kwamba kuna nchi za nje zinazotoa fedha kwa CHADEMA kwa makubaliano ya kuuziwa/kupewa rasilimali za Tanzania. Hapa issue sio kupekea pesa, ila atatakiwa athibitishe beyond reasonable doubt kuwa kuna nchi zimetoa fedha kwa masharti wa kupewa rasilimali za Tanzania. Sasa itakuwaje kama hizo nchi zitakataa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…