CHADEMA waipigia kura CCM

CHADEMA waipigia kura CCM

Mkuu OSOKONI hili suala kwenye nyanja ya upinzani si la kulichekelea na kulipuuza. CDM isidhani kwamba basi peke yake ndio inaweza kutwaa dola bila kuwashirikisha wapinzani wengine. Nchi za wenzetu wapinzani wanaungana dhidi ya vyama tawala lakini hapa kwetu inakuwa tofauti yaani mpinzani anaungana na chama tawala ili kumwangusha mpinzani mwenzake! Hii ni hatari kubwa.
Vyama haviwezi kuungana kama havina itikadi na manifesto angalau inayofanana! kuungana tu ili mradi kuondoa chama tawala madarakani hakuna maana mfano Raila aliungana na Mwai kibaki kuoindoa KANU then what followed? walitengana na uchaguzi uliofuata wakauana kuliko hata wakati wa KANU, so vyama viungane kama vinafanana itikadi na sera!!
 
Kimbunga itatuchukua muda sana kujua tufanye nini ili kuishinda CCM. leo watu wanadhani kuishinda CCM kwenye baadhi ya majimbo kunatosha. Kauli za viongozi wetu wa vyama vya upinzani dhidi ya vyama vingine vya upinzani yanakera zaidi kuliko yale wanayoyatoa dhidi ya CCM. Hawajifunzi kabisa kupingana bila kuwekeana hasira ili mbele ya safari washirikiane kwenye jambo jingine.
kila chama kina itikadi na sera zake huwezi kulazimisha vyama vya upinzani viungane kwa sake ya kuungana tu mwisho wakishakitoa chama tawala madarakani inafuata vurugu kama kenya kibaki na raila, chadema inaweza kuing,oa ccm bila msaada wa chama chochote kingine, mana hivi vyama vingine vimejaa mapandikizi ya ccm na ndio maana haviandamwi na dola kama chadema!
 
kila chama kina itikadi na sera zake huwezi kulazimisha vyama vya upinzani viungane kwa sake ya kuungana tu mwisho wakishakitoa chama tawala madarakani inafuata vurugu kama kenya kibaki na raila, chadema inaweza kuing,oa ccm bila msaada wa chama chochote kingine, mana hivi vyama vingine vimejaa mapandikizi ya ccm na ndio maana haviandamwi na dola kama chadema!
Kwani CDM ina itikadi moja na CCM?
Mbona mmewapigia kura? Si mngemsimamisha mgombea wenu regardless of the outcome?
Hamueleweki.
 
Mkuu OSOKONI hili suala kwenye nyanja ya upinzani si la kulichekelea na kulipuuza. CDM isidhani kwamba basi peke yake ndio inaweza kutwaa dola bila kuwashirikisha wapinzani wengine. Nchi za wenzetu wapinzani wanaungana dhidi ya vyama tawala lakini hapa kwetu inakuwa tofauti yaani mpinzani anaungana na chama tawala ili kumwangusha mpinzani mwenzake! Hii ni hatari kubwa.
Hivi ni mpinzani yupi aliye na afadhali kwa chadema? Tlp si ndo ya mrema, na mrema si ndo mpiga debe wa jk? Sï ndo hao wamewasaliti cdm? Vyama vingine vyote ni wapinzani wa cdm, huo ndo ukweli..
 
Last edited by a moderator:
Hivi vyama haviogopi UKIMWI !!!!
Angalia Mtandao

Mwaka 2000 CHADEMA alimuunga Mkono CUF....CHADEMA akawa CUF B na MKe wa CUF
Mwaka 2010 CUF akaamua Kumuacha Mkewe CHADEMA...CUF akaenda kuolewa na CCM akawa CCM B...
Naona sasa CHADEMA Ameamua Kuolewa na CCM huko Kaskazini ,
Tumieni Kinga!
 
Huna lolote gamba moyoni usoni unaoshea na gwanda,hiv ile kadi yako ya gamba namba ngapi vile? Yan nimesahau,samahan lakin
Kumbe hata huko nyumbani hawajajipanga vizuri. Wanakimbilia Arusha, na sijui kama 2015 Chama chetu cha Chadema kama kitakuwa hai. Tuungane tujenge Chama chetu. Siyo vizuri kufagia uchafu nje huku ndani hapakaliki.

Afande nashukru, aaaa samahani Kamanda pamoja sana
 
hivi hujanielewa kuwa sibishani na makapi??

Kumbe umekuja JF kubishana umeulizwa swali dogo tu CCM na Chadema wanaitikadi moja? Kwa nini mmeungana na CCM kuingusha TLP...tumieni kinga.
 
Punguza unazi wewe, simama kidete.

Mkuu Kobello,
Tanzania hakuna upinzani ni usanii tu, hawa Chadema ni waganga njaa si umeona wameongwa pombe wote wameipigia kura CCM na kuwatosa TLP.
 
Last edited by a moderator:
Ritz,

Ukitumikisha akili yako kidogo tu utagundua mambo mawili katika taarifa hii.
a) Kuwa haiko kamili. CCM kashinda kwa kura 24 kati ya 44 lakini TLP kapata kura 17. Kura 3 ziko wapi. Je unajua katika hizi kura 44 kila chama kina viti vingapi ili tuone hiyo defection ya CDM unayoizungumzia?? Huoni uwezekano kuwa TLP ndio wanaweza kuwa wameipigia CCM kura? Mbunge wao na CCM sote tunamjua!
b) Makubaliano ilikuwa ni kuiunga mkono CDM baadaye TLP wakaweka mgombea. Kwanini usidhani TLP siye mpinzani wa kweli na badala yake unadhani ni CDM?
c) Tuondoke kwenye siasa za chuki za vyama. Hata kama walimuunga mkono CCM. Yawezekana pia kuwa alikuwa na uwezo wa kutimiza mahitaji ya kazi anayogombea kuliko wa TLP.

Ukijifunza kufikiri kila mara kabla hujatoa comment a) comments zako zitapungua kwa idadi b) utazungumza mambo ya maana. Haitakuwa ni kurukia kila kitu unachokiona. Haiwezekani kuwa wewe una comments za kila jambo.

A jack of all trades is a master of none!!!
 
Kumbe hata huko nyumbani hawajajipanga vizuri. Wanakimbilia Arusha, na sijui kama 2015 Chama chetu cha Chadema kama kitakuwa hai. Tuungane tujenge Chama chetu. Siyo vizuri kufagia uchafu nje huku ndani hapakaliki.

Afande nashukru, aaaa samahani Kamanda pamoja sana
Kwani nyumbani kwa chama chenu CCM ni wapi? Unawaza ukabila tu!
 
tatizo hatujajua siasa za huko zikoje, ilikuaje wakakubaliana TLP asigombee ili hali alikuwa naibu mayor na kwa nini alikiuka makubaliano. binafsi naona hawa madiwani wamefanya vizuri kutumia njia ya mkato maana tungesikia CHADEMA waangukia pua

na hapa tujue kuwa hawa madiwani waliona ni bora ya mgombea wa CCM kuliko huyo wa TLP. Ila naumiza sana kichwa kwa nini mgombea wa CHADEMA alijitoa ???
 
Ritz,

Ukitumikisha akili yako kidogo tu utagundua mambo mawili katika taarifa hii.
a) Kuwa haiko kamili. CCM kashinda kwa kura 24 kati ya 44 lakini TLP kapata kura 17. Kura 3 ziko wapi. Je unajua katika hizi kura 44 kila chama kina viti vingapi ili tuone hiyo defection ya CDM unayoizungumzia?? Huoni uwezekano kuwa TLP ndio wanaweza kuwa wameipigia CCM kura? Mbunge wao na CCM sote tunamjua!
b) Makubaliano ilikuwa ni kuiunga mkono CDM baadaye TLP wakaweka mgombea. Kwanini usidhani TLP siye mpinzani wa kweli na badala yake unadhani ni CDM?
c) Tuondoke kwenye siasa za chuki za vyama. Hata kama walimuunga mkono CCM. Yawezekana pia kuwa alikuwa na uwezo wa kutimiza mahitaji ya kazi anayogombea kuliko wa TLP.

Ukijifunza kufikiri kila mara kabla hujatoa comment a) comments zako zitapungua kwa idadi b) utazungumza mambo ya maana. Haitakuwa ni kurukia kila kitu unachokiona. Haiwezekani kuwa wewe una comments za kila jambo.

A jack of all trades is a master of none!!!
after all kura ni za siri wamejuaje kuwa CHADEMA walipigia CCM ??
 
Kumbe hata huko nyumbani hawajajipanga vizuri. Wanakimbilia Arusha, na sijui kama 2015 Chama chetu cha Chadema kama kitakuwa hai. Tuungane tujenge Chama chetu. Siyo vizuri kufagia uchafu nje huku ndani hapakaliki.

Afande nashukru, aaaa samahani Kamanda pamoja sana

Nimeipenda hii. Wengi katika hii 'inji' wanamawazo kama yako kwamba kambi kuu ya CDM ni Mkoa wa K'Njaro. Kwa maoni yangu hili na liwe fundisho kwenu wote mnaosafiria gari la ukabila, udini na ujimbo!
 
Wanajipendekeza kwa ccm. Jamaa katuaibisha sana, kujitoa noma bora angeacha kujitoa baada ya kura tungesingizia wamechakachuwa matokeo kama kawaida yetu. Chadema huwa hatubali kushindwa huyu atakuwa ametumwa na C. c. m. Kisingizio hakina mshiko.'' Aise chali yangu kwa mimi nachota si ni pesa! kwa nini nihangaike na bahati na sibu na nikikosa?'' Bora nichukuwe haka kwanza ni imalishe kaduka kangu aiise.
 
Back
Top Bottom