CHADEMA waifungulia CUF njia…

CHADEMA waifungulia CUF njia…

Hamad Rashid mara nyingi tu ameshazungumzia masuala yanayohusu tanzania Bara.

Umeshawahi kusikia Mbowe anazungumzia swala la Pemba?

Kweli wewe na Uelewa wako PEMBA ina Wawakilishi; Wabunge Wengi ki Mraba zaidi ya Tanganyika sasa unataka na huyo MBOWE bado aizungumzie PEMBA? sasa huo sio UKIRITIMBA ni nini?

Kweli haujui kuwa Tanganyika ina matatizo mengi zaidi ya PEMBA? na ina Utajiri lakini unachotwa na VIONGOZI wakuu wabovu wasiojua jinsi gani ni bora kutunza na kulinda Maliasili; Madini; Malighafi za nchi...

Kweli umenishitua...
 
Attitude za watu kama ZeMarcopolo ndio zinaimaliza nchi yetu. Anapoandika thread zake unapata "tone" ya mtu ambaye ni arrogant,mbinafsi,mnafiki,mzandiki,mwenye uzoefu wa mipasho isiyo na tija kwa taifa bali kwa kundi la watu fulani, mtu aliyejengwa na propaganda zaidi kuliko umahiri wa kuandika mambo yenye kuleta tafari ya maslahi mapana ya Tanzania. Kuwa yeye ni yeye tu na yeye ndiye mwenye funguo za mlango wa chumba cha fikra sahihi za ni wapi Tanzania inakopaswa kwenda. Na kwamba kila mtu anayetaka kufikiri lazima aombe funguo toka kwake. Ukiangalia mabali zaidi kwa kutumia jicho la tatu unagundua kuwa aandikacho ZeMarcopolo na ile hali inayokuja na kile aandikacho ndio kitambulisho hasa cha watawala wetu tulionao madarakani ndani ya CCM na hata serikalini. Kwa hiyo ZeMarcopolo ndani ya JF ni kielelezo halisi na ushahidi wa fikra za watawala(sio viongozi)wetu na wale wanaofaidika kupitia watawala hao.
 
Kweli wewe na Uelewa wako PEMBA ina Wawakilishi; Wabunge Wengi ki Mraba zaidi ya Tanganyika sasa unataka na huyo MBOWE bado aizungumzie PEMBA? sasa huo sio UKIRITIMBA ni nini?

Kweli haujui kuwa Tanganyika ina matatizo mengi zaidi ya PEMBA? na ina Utajiri lakini unachotwa na VIONGOZI wakuu wabovu wasiojua jinsi gani ni bora kutunza na kulinda Maliasili; Madini; Malighafi za nchi...

Kweli umenishitua...

Kwahiyo ni wajibu wa mbunge wa Pemba kuzungumzia maswala ya Tanzania bara lakini mbungewa Tanzania Bara hapaswi kuzungumzia maswala ya Pemba?
Najua hiyo ni sehemu ya sera ya chadema ya majimbo lakini haiko sahihi kwenye hilo.
 
Attitude za watu kama ZeMarcopolo ndio zinaimaliza nchi yetu. Anapoandika thread zake unapata "tone" ya mtu ambaye ni arrogant,mbinafsi,mnafiki,mzandiki,mwenye uzoefu wa mipasho isiyo na tija kwa taifa bali kwa kundi la watu fulani, mtu aliyejengwa na propaganda zaidi kuliko umahiri wa kuandika mambo yenye kuleta tafari ya maslahi mapana ya Tanzania. Kuwa yeye ni yeye tu na yeye ndiye mwenye funguo za mlango wa chumba cha fikra sahihi za ni wapi Tanzania inakopaswa kwenda. Na kwamba kila mtu anayetaka kufikiri lazima aombe funguo toka kwake. Ukiangalia mabali zaidi kwa kutumia jicho la tatu unagundua kuwa aandikacho ZeMarcopolo na ile hali inayokuja na kile aandikacho ndio kitambulisho hasa cha watawala wetu tulionao madarakani ndani ya CCM na hata serikalini. Kwa hiyo ZeMarcopolo ndani ya JF ni kielelezo halisi na ushahidi wa fikra za watawala(sio viongozi)wetu na wale wanaofaidika kupitia watawala hao.

Mawazo yako yanavumiliwa kadri yanavyostahili.

Hata hiyo hoja ni jinsi vurugu za chadema bungeni zinavyoipa mwanya CUF kisiasa...
 
Kwahiyo kwa hiyo ni wajibu wa mbunge wa Pemba kuzungumzia maswala ya Tanzania bara lakini mbungewa Tanzania Bara hapaswi kuzungumzia maswala ya Pemba.
Najua hiyo ni sehemu ya sera ya chadema ya majimbo lakini haiko sahihi kwenye hilo.

Pemba ina BUNGE lake Baraza la Wawakilishi halafu Ina Wabunge BUNGE la Muungano... Sasa Unataka Kiongozi wa UPINZANI pia awe anatoa kipaumbele Mambo ya PEMBA kwanza na Wakati TANGANYIKA kuna issues kibao CHAMA TAWALA cha CCM kimeirudisha NCHI NYUMA' Nchi ni kama vile enzi za STONE AGE; Hakuna UMEME; Hakuna MAJI; Hakuna Malazi; Hakuna ELIMU; Hakuna KAZI ... wewe nadhani unaishi wa upendeleo au kwa MLO wa KIFISADI hauoni hayo matatizo hata kidogo unawaza matatizo ya PEMBA kweli tutafika? changes comes from within!!! kama unaogopa kujirekebisha mwenyewe kwa Maovu yako mwenyewe then U R DONE and finished!!! Don't throw out the blame to others just because you can...
 
Chama cha kuchana viongozi wa serikali kweli kinaongozwa na wala ganja wengi.
Suguuu sura kaa chuma
 
Anzisha mada yako kuhusu CUF. Hapa tunaijadili CHADEMA. Inaonekana shule ulikuwa unafeli sana wewe kwa ajili ya kushindwa ku concentrate kwenye kitu kimoja :smile-big:

Ni wewe uliyesema Chadema ni CCM B sasa inaonyesha jinsi ulivyofaulu shule hizo ulizokwenda... mimi ni wa kufeli nikataka kujua Je, CUF ni wapi ? Swali na ELIMU haina hasira...
 
chadema imeshindwa kuitumia vizuri nafasi yake kama chama kikuu cha upinzani kwa manufaa ya taifa.

Hali ilianza kuonekana tangu awali baada ya uchaguzi mkuu ambapo chadema ilikataa kushikisha vyama vingine kwenye uongozi wa upinzani bungeni. Uamuzi huu wa chadema uliwasikitisha wapenda mabadiliko wengi.

Hii ni tofauti na chama cha wananchi cuf ambacho kiliishirikisha chadema kwenye uongozi wa upinzani bungeni katika bunge liliopita. Manufaa yake kwa taifa tumeyaona, bunge la tisa liliweza kusimamia hoja nzito za kitaifa na kuitetemesha serikali mpaka waziri mkuu akajiuzuru. Bunge hili la 10 lina wabunge wengi zaidi wa upinzani lakini hakuna mafanikio yoyote katika kujenga hoja!

Zaidi ya hilo, mara kadhaa chadema wamekuwa wakikimbia mijadala kwa mtindo wa kususa ambao haujawahi kuleta manufaa yoyote. Jambo kama la kususia hotuba ya mkuu wa nchi halikuwahi kutokea bungeni wakati cuf ilipokuwa chama kikuu cha upinzani kwenye bunge la 9.

Kadri siku zinavyoenda wananchi wanazidi kushuhudia jinsi chadema inavyoshindwa kuwakilisha maslahi ya taifa bungeni. Jambo linalosikitisha zaidi ni kwamba siku hizi wabunge wa chadema wakiongea taarifa pekee inayoweza kutolewa ni kwamba “wamemchana kiongozi fulani”.

Anayeongoza katika tabia hii ya “kuchana” ni sugu ambaye jana ameelezewa kuwa alimchana mbunge wa iramba mashariki. Huo ndio ulikuwa mchango wake kwenye bajeti ya waziri mkuu!!!

Kwa kweli inasikitisha pale input ya speech ya mbunge katika kuchangia bajeti ya waziri mkuu inapokuwa ni kumchana kiongozi! Mambo haya hayakuwepo bungeni wakati cuf ilipokuwa chama kikuu cha upinzani bungeni. Hamad rashid wa cuf alikuwa maridadi zaidi katika kusimamia shughuli na hoja za upinzani bungeni kuliko anavyofanya kiongozi wa upinzani wa bunge hili la 10.

Picha inayowekwa na chadema ni kwamba upinzani ni vurugu. Wananchi wastaarabu wanaanza kuchukizwa na tabia za uvunjifu wa kanuni na kumkosea heshima spika zinazofanywa na wabunge wa chadema. Hamad rashid wa cuf hakuruhusu hili, lakini kiongozi wa sasa wa upinzani bungeni anaona vurugu na kubishana na spika kama burudani.
Nikumbushe tu kuwa taarifa zilizopo zinaonyesha hakuna mbunge hata mmoja wa chadema aliyeweza kutekeleza ahadi zake alizotoa kwa wananchi jimboni. Kwahiyo wananchi wanaweza kuwa na imani na wabunge wa chadema iwapo wataona angalau bungeni wana michango yenye tija.

Kwavile jimboni wabunge wa chadema hawatekelezi ahadi na bungeni wanaenda “kuchanana” wananchi watakuwa hawana sababu ya kuchagua chadema. Hasahasa ikizingatiwa kuwa chadema kimekuwa ni chama kinachoainisha matatizo bila kutoa jinsi yoyote ya utatuzi.

Vilevile cuf watakuwa na sababu ya kuwaambia wananchi kuwa chadema wameharibu image ya upinzani bungeni - jambo ambalo ni kweli. Jambo hilo litaiwezesha cuf kuchukua kura nyingi za wapenda upinzani ambazo zingeweza kuwa za chadema katika majimbo ya tanznia bara. Kwa vigezo hivyohivyo chadema itaendelea kukosa kura za zanzibar.

Bottomline: Chadema imeligeuza bunge kuwa jukwaa la kampeni. Cuf walipokuwa wanaongoza upinzani bungeni walisimamia hoja kwa maslahi ya taifa. Tabia ya vurugu na kumkosea heshima spika inayofanywa na chadema ni mtaji wa kisiasa kwa cuf.

Ushauri: Chadema ijiepushe na tabia za mipasho mbele ya tbc mkiwa bungeni. Sugu apewe mafunzo maaluma ya kuchagua maneno ya kuongea bungeni – itafaa zaidi iwapo hotuba zake zitapitiwa na mnyika kabla hajazisoma.

siasa za tanzania taabu sana, mijitu kama hii ambayo haina uchungu na nchi yetu ni janga la taifa, ccm imeongoza miaka 50 hakuna la maana badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma, angalia rwanda nchi ndogo ambayo uchumi wake unapaa kama ndege, sisi tumekalia kukomalia vitu visivyo na maana, ona kampuni za simu zinavyotuibia, mikataba mibovu, ona ufisadi , elimu kuporomoka, leo hii mtu anasimama na kuanza kuitetea ccm, shame on you. Maendeleo yeyote yanatokana na uongozi bora. Ccm wameshindwa kabisa. Lazima tuwe na uchungu wa nchi tuseme ukweli. Na bila chadema hali ingekuwa mbaya sana. Mungu ibariki tanzania
 
Upuuzi mtu!!

Wakati unalinganisha Bunge la 10 unakosa kulinganisha Makinda na Sitta, kulinganisha Hamad na Mbowe!! Unalinganisha vipindi na matukio, na havileti picha unayotaka kuieleza.

Kuhusu kutekeleza ahadi. Kila kona CCM inaendelea kusema yanayotendwa ni Ilani ya Uchaguzi ya CCM!! Kuna ahadi ngapi ambazo Rais wa Jamhuri kashindwa kutekeleza? Au na yeye ni Chadema??
 
Mawazo yako yanavumiliwa kadri yanavyostahili.

Hata hiyo hoja ni jinsi vurugu za chadema bungeni zinavyoipa mwanya CUF kisiasa...

Kuna vurugu gani Bungeni?? Hata Spika unasikia kafuta iliyodaiwa kuwa kesi dhidi ya wabunge wa Chadema na waliweka wazi kuwa hawatahojiwa. Usijifanye unasahau, Chadema wanafahamu tafsiri ya Sheria za Bunge kuliko unavodhani. Na hii ndio tofauti usiyoiona kati ya kambi za Upinzani za Bunge la 10 na 11!!!

Kwa taarifa yako tu, CUF inaweza kufanya vizuri Pemba na Zanzibar, sio Bara!! Uthibitisho wa hili ni nguvu inayotumiwa na CCM na serikali kudhibiti mafanikio ya kisiasa ya Chadema. Zamani ilisemwa Chadema iko mijini na kwamba mtaji wa CCM uko vijijini. Hatusikii msemo huu tena baada ya Chadema kuanza kushinda chaguzi kadhaa huko vijijini tena kwenye strongholds za CCM kama mkoa wa Tanga. Wakati CUF inafifia, Chadema inajipanua na CCM inafanya kazi ya kudhibiti upinzani kwa hila badala ya kuleta maendeleo au kutekeleza wanachoita Ilani ya Uchaguzi.

PS. Mimi si muumini wa vyama!!
 
Snoopy Doggy Doggy. Wewe na Chemba cha choo na Nepi inatakiwa muimbe bendi moja.
 
Mkuu umechambua hoja kwa umakini mkubwa Chadema inaelekea walipo UMD.
 
CHADEMA imechoka kiasi kwamba Mh. Sugu anachangia pumba bungeni na Mh. Nassari yeye hajui umuhimu wa Nyuki, kwa kweli 2015 CUF njia nyeupe kwao ya kuwa chama kikuu cha upinzani.
Na yule wa Nkasi anasema tulime bangi liwe zao la biashara...Bado yule wa Korogwe hajasema serikali itambue uchawi nk
 
hatuwezi kushirikiana na vibaraka wa ccm. bora tuwe wachache wanao elewana bila kuzungukana. wewe utashirikiana na mbatia, lyatonga au ccm b?. mia
 
hatuwezi kushirikiana na vibaraka wa ccm. bora tuwe wachache wanao elewana bila kuzungukana. wewe utashirikiana na mbatia, lyatonga au ccm b?. mia

Chadema ikiwa peke yake ni vurugu tupu kama unavyoona. Mijadala ya kitaifa inafeuzwa ngonjera!!!
 
Back
Top Bottom