CHADEMA/UKAWA, mtawapokea Chenge na Rostam pia?

CHADEMA/UKAWA, mtawapokea Chenge na Rostam pia?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Inajulikana kuwa hawa ni marafiki walioshibana ndani ya CCM na hata katika maisha ya kawaida. Ikiwa swahiba wao Lowassa atahamia CHADEMA/UKAWA, wanaweza nao kumfuata rafiki yao.

Sasa ndugu zangu CHADEMA/UKAWA, mtakuwa radhi kuwapokea Andrew John Chenge na Rostam Aziz kuwa wanachama wenu?

Jibuni ili umma ufahamu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
VUTA-NKUVUTE

Kwani Rostam bado mwanachama wa CCM? nakumbuka wakati anajivua Ubunge kule Igunga alisema kuwa ANAACHANA NA SIASA ZA MAJI TAKA na kiuhalisia alimaanisha siasa ndani ya CCM ni za maji taka.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Tupa Tupa Wa Lumumba naona umefufuka na Laigwanan ulikua huonekani kabisa hapa Jukwaani baada ya Dhoruba kali kule Dodoma.

Karibu sana Ukawa.
 
Mzee Tupa Tupa Wa Lumumba naona umefufuka na Laigwanan ulikua huonekani kabisa hapa Jukwaani baada ya Dhoruba kali kule Dodoma.

Karibu sana Ukawa.

Mkuu,mimi sikuwahi kuwa team ya Lowassa. Ni mchafu mtu huyu

Mzee Tupatupa
 
Lowassa anakuja yeye kama yeye, mwanachama mwingine yoyote wa CCM atakayependa kujiunga na CDM basi atalazimika afuate taratibu zilizopo!!
 
Wakiamua kuacha ushetani wa Magamba nakufwata TORATI YA CHADEMA YA KUWATUMIKIA WANANCHI

NAKUKIRI MAKOSA YAO WATASAMEHEWA

ILIMAPAMBANO YAENDELEEE
 
Mkuu,mimi sikuwahi kuwa team ya Lowassa. Ni mchafu mtu huyu

Mzee Tupatupa

Mzee VUTA-NKUVUTE tafadhali sana kama wewe sio mnafiki hembu tuonyeshe hata mmoja tu CCM aliyemsafi ni nani??!!

Ruksa kutaja hata wake na watoto wa vibopa wa CCM kama Miraji na wengine,au hata Vimada kama vile Vick Kamata road na wengine!!

Chuki yako na Lowasa ni kama Ridhiwani na Mama Salma,kisa madaraka,mlikuwa na mgombea wenu kwenye kabati ambae hana mvuto na wala uwezo,mkapiga vita Lowassa cuz he was too big na the only potential candidate ili kibaraka wenu apite!!

Ni wewe uliyepiga Kambia wiki 3 kabla ya Lowassa kuongea Arusha,ni wewe uliyenadi hapa kuwa task force imeundwa na Mangula kuandaa file hasi ya Lowassa,Mbona hamsemi ya Membe??!! Mbona hamsemi ya Makamba??!!
I hope you have balls and guts,tuonyeshe msafi aliye CCM
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,mimi sikuwahi kuwa team ya Lowassa. Ni mchafu mtu huyu

Mzee Tupatupa
Uchafu wake ni nini kwa mfano? Naamini utakuja hapa na kutuambia uchafu wake ni Richmond, nasi tutasema uchafu wa Magufuli ni kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa huku akijua kuna upungufu mkubwa wa nyumba za watumishi. Baada ya hapo tunatafuta unafuu, kulikuwa na ulazima wowote wa kuuza nyumba? Na kwa upande mwingine wa Lowassa kulikuwa na ulazima sana wa kuingia mkataba na Richmond? Wote tutakubaliana kwamba kwa Lowassa nchi ilikuwa kwenye crisis kubwa ya umeme, lakini pia tutakubaliana kwamba Magufuli aliuza nyumba kwa interest yake tu, hakukuwa na any pressure ya kumpelekea kuuza nyumba. Kwa kuwa wote ni wachafu, basi mwenye unafuu ndiye tutakayempa kura.
 
Hata Osama Bin Laden (R.I.P), Angekuwa Hai Leo na Kutuakikishia Ushindi dhidi ya MaCCM Nadhani Angekaribishwa Kwa Mikono Miwili.

Malaria=CCM Havikubaliki Kwa Mstakabali wa Taifa.
 
VUTA-NKUVUTE

Waeshakuambia yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Sijui hawafahamu kwamba historia hujenga ya leo na ya leo hujenga ya kesho. Ama kweli hii ndio mtu kajigeuzia kibla mwenyewe na kujiwekea kisu shingoni.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,mimi sikuwahi kuwa team ya Lowassa. Ni mchafu mtu huyu

Mzee Tupatupa
Thibitisha uchafu wake mbona kama chuki binafsi hivi na kama mlikuwa mnashindwa kumshughulikia kwa sababu ya kichaka alichokuwepo sasa ni muda sahihi mwizi katoka kichakani yuko in plain site nadhani ni rahisi sasa kwa vyombo vya dola kula kichwa vinginevyo ni uzushi tu kusema mchafu.
 
Ni wakati sasa kuujua ukweli wa richmond na kupima nani mchafu
 
hao watabaki ili watumike kutupa taarifa zenu
 
Back
Top Bottom