CHADEMA, uislam na waislam!

CHADEMA, uislam na waislam!

Status
Not open for further replies.

KIM KARDASH

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
5,139
Reaction score
1,149
kumekuwa na upotoshaji au propaganda kwamba chadema hakipikiki chungu kimoja na waislam walio wengi(sio wote),je suala hili ukweli wake ukoje?na je ni wapi hasa kama papo wanapotofautiana na kushindwa kuaminiana?je tatizo kama lipo kweli lipo upande gani,kwa waislam ama kwa jinsi chadema yenyewe ilivyojiweka na kuikalia kimya propaganda hii hatari.

ushauri wangu kama tatizo lipo kwa waislam kutokana na kulishwa tu propaganda basi tuwasaidie na kama tatizo lipo upande wa pili kwa maana ya chadema basi muda upo ijirekebishe na kuondoa sintofahamu hii kwa maslahi yake binafsi kama chama cha siasa chenye hamu ya kushika dola siku moja kwa kuwa ni ukweli ulio wazi bila kura za watanzania wote ambao kwa asilimia kubwa ni waislam na wakristo kwa umoja wao hakuna uwezekano wala njia ya mkato ya kushinda uchaguzi wa rais na kuunda serikali.

Nawasilisha.

DSC08501.JPG

Viongozi wa dini ya kiislamu mkoa wa Kilimanjaro.



DSC08536.JPG

mbunge wa jimbo la Moshi mjini Philemoni Ndesamburo akiteta jambo na viongozi wa dini ya kiislamu,huu ni mfano wa kuigwa




SDC10404.JPG


safi sana hii


Chadema+na+Idd+1..JPG



Chadema+na+Idd+3..JPG


Hii ni namna bora zaidi ya kujenga mahusiano na kuaminiana,iendelezwe na viongozi wa chadema mikoani na wilayani,kamwe chadema isidhani hii propaganda itaondoka yenyewe tu hapana they have to do something kujionyesha hawako upande wa kanisa na hawawachukii waislam kama waislam wengi wanavyoaminishwa na pia wana chadema mmoja mmoja pia mkisaidie chama kwa kuwa polite kwa waislam na wala msiwakejeli kwa namna yeyote ile bali muwasaidie kukielewa chama chenu,muwe mabalozi wazuri wa chama chenu,waislam watawaelewa na kuwakubali tu
 
Hakuna kitu kama hicho cha mgogoro kati ya chadema na uislamu hizo ni propaganda za CCM kikielekea kufa ni dalili tosha ya chama kilichokosa hoja na kinaelekea kufa, siyo hayo tu wanahubiri mpaka ukanda na ukabila ili waendelee kubaki madarakani lakini wananchi wameshawashtukia.
 
Hayo yaliletwa na sultani kikwete kuitenganisha chadema na Uislamu lakini sasa yameanza kumtokea puani Waislamu wa Mtwara wameshaligundua sasa wanampa za USO
 
Hayo yaliletwa na sultani kikwete kuitenganisha chadema na Uislamu lakini sasa yameanza kumtokea puani Waislamu wa Mtwara wameshaligundua sasa wanampa za USO
Kwani Kikwete ndie aliandika waraka au watu wa Mtwara wameanza kuichagua CCM baada JK kugombea urais? rudi kwenye mada kama una la kuchangia pumzika kwa amani.
 
Kwa mtazamo wangu Waislamu waumini wa kawaida wala hawana tatizo na Chadema na Chadema haina tatizo na waislamu, wakristo au dini yoyote ile. Tatizo ni wale vocal muslims, akina Sheikh Ponda na wenzake wa Annuur na Radio Iman.

Hawa wangependa chama cha siasa kitangaze from day one kwamba chama kitafanya hivi kitafanya vile kwa manufaa ya waislam ndipo wakiunge chama mkono. Sasa kwa chama cha siasa ni makosa makubwa kupandikiza mbegu za udini kwa namna hiyo.

Waislam yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni waislam, bali kwa kuwa ni Watanzania kwanza. Wakristo yapaswa wakiunge mkono Chadema si kwa vile wao ni wakristo, bali kwa kuwa ni watanzania kwanza.

Chadema wanalijua hilo na ndio maana namna zao za kujenga mahusiano na makundi mbalimbali zinawabeba wote kama watanzania. Kama wadini hawaitaki Chadema, basi ni tatizo la wadini. Si la Chama.
 
Llsemwalo lipo kwani mwananchi wa kawaida ni ngumu sana kumtoa ktk propaganda hiyo mfano mikoa kama ya tanga,pwani nk nivyema m4c ikajikita huko kutoa elimu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
CCM kila wanapoona chama cha upinzani kinapata nguvu hutumia propaganda kama hizi kujaribu kukipunguzia nguvu. Walianza na CUF na kuwaaminisha Wakristo kwamba chama hicho ni cha Waislamu. Baadaye wakauhamishia ujinga huo kwa Chadema wakidai ni cha kikabila na cha Wakristo. CUF walipuuza propaganda hizi lakini iliwaathiri kwa kiasi kikubwa sana na chama kikapoteza umaarufu kwa kiasi kikubwa. Lakini kwa Chadema ni tofauti kwa sababu tayari wananchi walio wengi wameamka sasa na wanajua uchafu wa CCM na propaganda zake. Ila ningewashauri Chadema wapambane waziwazi na propaganda hizi chafu na wawaeleze wananchi kutosikiliza ujinga huo wa majambazi wa CCM ambao lengo lao ni kulazimisha kuendelea kuwatawala watanzania licha ya kushindwa kuwaondoa kutoka kwenye dimbwi la umaskini.
 
Jambo la ajabu kuna diwani wa Chadema kwenye moja ya kata huko rufiji..Jambo jingine lakushangaza ni kuwa Zitto Kabwe ni muislamu..Ccm hawawezi kuongoza chi bila kuwagawa watu sasa viongozi wa kiislamu wale mashehe ubwabwa ndo wanaoharibiwa Ccm kama ilivyotokea kule Igunga mpaka leo Bakwata wameshindwa kuwaomba Watanzania radhi kwa ujinga wa matamko yao kule Tabora
 
Mliji changanya sana kumsimamisha Padri Mstaafu kuwa Mgombea Urais,na makanisa yakawa yanatoa approval kuwa hata kama Padri hajaoa sio tatizo kuongoza nchi! Na matamko ya Roman Catholic nayo kipindi yalizidi,siku hizi wameacha! Naona hapa ndipo mlipo jipambanua!
 
Hata nyerere alikuwa anavaa kibandiko aonekane anawapendea sana Waislaam. Matokeo?
 
Hakuna kitu kama hicho cha mgogoro kati ya chadema na uislamu hizo ni propaganda za CCM kikielekea kufa ni dalili tosha ya chama kilichokosa hoja na kinaelekea kufa, siyo hayo tu wanahubiri mpaka ukanda na ukabila ili waendelee kubaki madarakani lakini wananchi wameshawashtukia.

yah lakini hiyo strategy inaonekana kuisaidia ccm kwa kuwa hata kipindi cuf imeshika hatamu za upinzani hapa nchini hii kitu pia ilitumika kuichafua cuf mpaka ikakosa umaarufu miongoni mwa wakristo wakiaminishwa kwamba cuf ni chama cha waislam,chama cha wapenda n.k. lakini ukweli ni kwamba cuf ni chama cha siasa tu na kimeendelea kuwa hivyo,ndio mana nasema viongozi wa cdm wasilikalie kimya hili,they have to do something kuondosha propaganda hii,wakikaa kimya na kujifanya eti hamna kitu kama hicho waislam zaidi watazidi kujiunga katika kuichukia cdm bila sababu
 
Kabla ya uchaguzi mkuu wa 2010,iliibuka mipasuko mikubwa ya kidini ambayo itachukua miaka mingi kuiondoa.
CCM wakidhani ni kuikomoa CDM wakaeleza kwa mbinu mbalimbali kuwa CDM ni chama cha kikristo,na waislamu,bila kufikiri,wakameza propaganda hizo(na kuhimizana misikitini kuikataa CDM).
Hili limejenga pengo kubwa na chuki baina ya wakristo na waislamu.
Itatugharimu kama taifa kumaliza pengo hili!
 
Hayo yaliletwa na sultani kikwete kuitenganisha chadema na Uislamu lakini sasa yameanza kumtokea puani Waislamu wa Mtwara wameshaligundua sasa wanampa za USO

Wewe na kundi lako ndiyo mnawachafua Chadema kwa kuwakejeli Waislam.
 
Wewe na kundi lako ndiyo mnawachafua Chadema kwa kuwakejeli Waislam.
Nimewakejeli waislam wapi? Mkuu hizo ni propaganda mnazotumia nyinyi CCM nafikiri umeona ofisi zenu zinavyochomwa huko kusini lakini za CUF na CHADEMA hazijaguswa watu wameshawashtukia
 
Kuvaa kofia baraghashia na kupiga picha na waislam haitoshi hio cheap propaganda cha muhimu ni muhimu ni kufunguka ki sera na muelekeo
Bado kuna tatizo la kuamini malengo na nia ya CDM. Dhidi ya Waislam na uislam kwani hata zao ni za Mehemko kama ya kilokole so yaliyojificha ndani ya moyo zao ni makubwa kuliko yale wanayoengea wakivaa baraghashia kusanif waislam

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom