Sarya
Senior Member
- Nov 6, 2009
- 151
- 41
Jamani hili swala liko bayana, sehemu kubwa ya wapiga kura ni wazee na vijana wachache ambao walijiandikisha. Kumbukeni kwamba asilimia kubwa ya vijana walikuwa hawaoni umuhimu wa kujiandikisha na leo hii ndo wanaona umuhimu. Ndo maana ukiangalia idadi ya waliojiandikisha ni kubwa kuliko wapiga kura halisi maana yake ni kwamba hili daftari linahitaji kuwa updated na CCM wanaliogopa hilo maana hata kule kijijini vijana wengi waliomaliza shule za kata hawaiungi mkono CCM lakini hawaja andikishwa na dio wahudhuriaji wazuri mikutano ya kampeni za Chadema.
Nasema hivyo kwa maana kwamba wengi wetu tumechukua taswira ya wingi wa watu katika mikutano ya Chadema kuliko CCM lakini inapokuja kwenye uhalisia wa kura CCM wanawazidi Chadema.
Ndo maana Nape hakuyaongea anayoyasema kabla kwani alitarajia kupoteza kata nyingi kuliko ilivyotokea kumfanya aamini kuwa wameshinda. Kimsingi huwezi kusema umeshinda wakati umepoteza kile ulichokuwanacho.
Lingine ni kuwa Nape ameathirika kisaikolojia na vuguvuga la mabadiliko inayoendeshwa na Chadema na ndo maana hakuwa anavitaja vyama vingine kitu ambacho nadhani ni hatari zaidi kwa chama tawala kilichokaa madarakani mda mrefu kama CCM.
Hata kwenye kata ambazo upinzani umechukua, utakuta imetumika nguvu ya ziada na hata umwagaji damu ambao umesababishwa na chama tawala kutokukubali kushindwa au uonevu wa vyama vya upinzani hasa pale CCM inapozidiwa kete.....hayo yamejionyesha sana kwenye kampeni.
Nape anapaswa kupambana na umaskini wa watanzania kupitia ilani ya chama chake lakini kama ataendelea kuwaza M4C kama ndo adui namba moja kuna hatari kubwa kwa chama chake.
Nasema hivyo kwa maana kwamba wengi wetu tumechukua taswira ya wingi wa watu katika mikutano ya Chadema kuliko CCM lakini inapokuja kwenye uhalisia wa kura CCM wanawazidi Chadema.
Ndo maana Nape hakuyaongea anayoyasema kabla kwani alitarajia kupoteza kata nyingi kuliko ilivyotokea kumfanya aamini kuwa wameshinda. Kimsingi huwezi kusema umeshinda wakati umepoteza kile ulichokuwanacho.
Lingine ni kuwa Nape ameathirika kisaikolojia na vuguvuga la mabadiliko inayoendeshwa na Chadema na ndo maana hakuwa anavitaja vyama vingine kitu ambacho nadhani ni hatari zaidi kwa chama tawala kilichokaa madarakani mda mrefu kama CCM.
Hata kwenye kata ambazo upinzani umechukua, utakuta imetumika nguvu ya ziada na hata umwagaji damu ambao umesababishwa na chama tawala kutokukubali kushindwa au uonevu wa vyama vya upinzani hasa pale CCM inapozidiwa kete.....hayo yamejionyesha sana kwenye kampeni.
Nape anapaswa kupambana na umaskini wa watanzania kupitia ilani ya chama chake lakini kama ataendelea kuwaza M4C kama ndo adui namba moja kuna hatari kubwa kwa chama chake.