Ukisoma kitabu cha Mandela kinachoitwa "Long Walk to freedom" anasema 'the darkest hour of the night is dawn'. Anaelezea harakati zake za kutafuta ukombozi. katika vipindi vigumu kupita vyote anasema ni wakati ukombozi ulipokaribia. hapo PAC, Inkata Freedom, Makaburu na wengine walikisumbua sana ANC. Sasa chadema wana wakati mgumu sana katika harakati za ukombozi. Napenda kuwapa moyo kuwa hali ngumu mnayoiona inaashiria ukombozi upo karibu. Hii ni alfajiri karibia kunakucha na giza ndipo linakuwa nene zaidi.