CHADEMA ni Imara zaidi kuliko CCM

CHADEMA ni Imara zaidi kuliko CCM

Kuna siku niliuliza kama Mbowe anapaswa kuondoka kwenye nafasi yake ya Uenyekiti (itafika siku ataondoka tu) nani achukue nafasi yake. sijawahi kupata jibu. Lakini bado kila wakati likitoea jambo ndani ya CHADEMA lazima jina la Mbowe litajwe na kusemwa yanayotokea ni kwa kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA.

Lakini uimara wa kitu hupimwa kutokana na mashambulizi ama majaribu inachokumbana nayo. CHADEMA tangu baada ya kujiuhisha (Rebranding) mwaka 2006 kimekuwa ni chama kinachopanda na kuoenesha uimara wa kupambana na matatizo yanayosababishwa na CCM pamoja na dola dhidi yake!

Kila likitokea jambo wapinzani wa CHADEMA hulifanya jambo hilo kama ni jipya na litaisambaratisha CHADEMA. Kama viongozi wa chama kutoka CHADEMA na kujiunga CCM wameshatoka hadi viongozi wa kitaifa na bado CHADEMA inasonga mbele.

Kwa ulinganifu CHADEMA ni chama Imara sana kuliko CCM kwa kuwa chenyewe kinafanya siasa bila ya kutegemea dola dhidi ya CCM ambayo bila ya kutegemea dola ni chama dhaifu sana kuliko hata TLP ya Mrema.
Really?
Good job
 
Wenye uwezo na roho imara wasiyoyumba wapo wengi mno nawakati ukifika watapewa mikoba.
Vetting ya sasa ni imara sana kuliko awali. Yanayojiri sasa yanaiimarisha cdm kuliko ccm.
 
Hvi kuna watu bado wanaimani na chadema.....duh hii inanikumbusha vita ya US Vs Japan kule kwenye visiwa vya pacific... japan ilikuwa inachezea kichapo kizito pote katk visiwa vya Philippine, midway, guadiucanal, Saipan, Iwo jima na Okinawa lakn bado Japanese walijitoa ufahamu wakijiaminisha kuwa wanaweza kushinda mwisho wa Siku walijikuta wanapoteza roho za askar na raia wapato 2.5ml....ndo yatakayoikuta chadema

Ndugu yangu unakosea sana, unadhani CHADEMA ni viongozi, sio kweli chadema ni mbadala wa uongo na upofu. Watu bado wanaonewa, raslimali za nchi bado zinawasaidia wachache, elimu yetu ni ya kibaguzi, huduma zetu za afya halikadhalika. Waulize hao wakombozi wa wanyonge nani mwanae anasoma kwenye shule zetu? Walivyo na roho mbaya wameamua "hawatatoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kwa wale ambao wamesoma shule za binafsi". Matokeo yake, watoto wao waliosomea shule binafsi kuanzia chekechea hadi kitadato cha nne, wanawaingiza shule za kidato cha tano na sita shule za serikali. Kwa kuwa wameandaliwa vizuri wanafanya vizuri, wanapata mikopo na watoto wa wanyonge wanatupwa kwenye bahari ya sahau.

Kwa kuwa ubaya huu bado upo na unaendelea kuwepo, upinzani utaenedelea kuwapo hata kama si kwa jina la CHADEMA. Chadema ni ukweli, haki, upendo na ujasiri dhidi ya utawala kandamizi.
 
Back
Top Bottom