CHADEMA ni chama kikubwa lakini hakina mipango makini

CHADEMA ni chama kikubwa lakini hakina mipango makini

MWONA MBALI

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
460
Reaction score
612
Ni katika uhuru wa mawazo natafakari hili, demokrasia katika Africa imekuwa na maigizo mengi sana, mara nyingi vyama tawala bila kujali kukubalika kwake na wananchi vimekuwa vikitumia dola na fursa ya utawala kujihakikishia utawala wa milele. uhuru wa kidemocrasia wa vyama pinzani umekuwa ukibanwa pasipo sababu za msingi.

Ili vyama vya upinzani viweze kwenda mbele vinahitaji watu makini wenye weledi na ujanja wa kisiasa kutumia fursa ndogo wanazozipata kujitangaza na kujenga hoja madhubuti na kufanya chama tawala "kihahe".

Ni miezi michache iliyopita shughuli za kisiasa za vyama ni kama ilikuwa imepigwa marufuku kabisa, sasa angalau mikutano ya ndani imeruhusiwa.

nilitegemea fursa hii ya kuruhusiwa mikusanyiko ya ndani kwa chama kikubwa kama CHADEMA ingeitumia vizuri ili kuhalalisha madai yao ya kubanwa kisiasa. na kwa kuwa chama kina mtandao wa nchi nzima pengine zingeibuliwa hoja mbalimbali zenye kuonyesha mapungufu ya kiutendaji ya serikali na pengine kushauri maeneo ya kuboresha, yote ni katika kuletea maendeleo taifa letu.

ACT wazalendo pengine ni chama kinacho onekana kidogo kilicho na mbunge mmoja tu, wao wameiona fursa hii jana walikuwa na mkutano wa kidemocrasia uliokuwa na waliikwa mbalimbali, sitajikita sana ya nini kilijadiliwa ila kitendo cha ACT kufanya mkutano ule wa ndani kwa ufanisi, kinafanikiwa zaidi kujitangaza na wameonesha kuwa wanaweza kutumia fursa ndogo zilizopo kufanya mambo makubwa.

Idara za uenezi/habari/na propaganda za vyama vya siasa hasa vya upinzani zinapaswa kuwekwa watu wenye akili nyingi na wanaojua kutumia kila fursa inayojitokeza ili kuimarisha uhai wa chama.

CHADEMA ni chama kikubwa zaidi ya ACT ila idara yao ya PROPAGANDA NA UENEZI ina watu wasio na AKILI KUBWA wakati ACT WAZALENDO ni chama kidogo kuliko CHADEMA ila idara yao ya PROPAGANDA NA UENEZI ina watu makini na wenye akili nyingi.

Najiuliza CHADEMA wana hoja gani kwa wananchi? je hiyo hoja yao itatoka kwa mikutano ya hadhara na maandamano pekee?
 
Nmeshangaa sana kuna uzi humu unahusu mkutano wa act wa jana, badala ya kujadili hoja alizotoa eti wao wanaanza kumzodoa,
 
Mkuu tokea Chadema iuzwe kwa Mafisadi, haina ajenda wala mvuto kwa watanzania.

Wild beast waliobakia nao wanaishirizia ufipa kutabaki kweupe.
 
Hivi act mpinzani wenu ni chadema ama chama tawala,,,hizo akili zenu kubwa ndo zimefanya muwe na ajenda ya kupinga ipinzani wenzenu???


Mna matatizo sana
 
Ni katika uhuru wa mawazo natafakari hili, demokrasia katika Africa imekuwa na maigizo mengi sana, mara nyingi vyama tawala bila kujali kukubalika kwake na wananchi vimekuwa vikitumia dola na fursa ya utawala kujihakikishia utawala wa milele. uhuru wa kidemocrasia wa vyama pinzani umekuwa ukibanwa pasipo sababu za msingi.

Ili vyama vya upinzani viweze kwenda mbele vinahitaji watu makini wenye weledi na ujanja wa kisiasa kutumia fursa ndogo wanazozipata kujitangaza na kujenga hoja madhubuti na kufanya chama tawala "kihahe".

Ni miezi michache iliyopita shughuli za kisiasa za vyama ni kama ilikuwa imepigwa marufuku kabisa, sasa angalau mikutano ya ndani imeruhusiwa.

nilitegemea fursa hii ya kuruhusiwa mikusanyiko ya ndani kwa chama kikubwa kama CHADEMA ingeitumia vizuri ili kuhalalisha madai yao ya kubanwa kisiasa. na kwa kuwa chama kina mtandao wa nchi nzima pengine zingeibuliwa hoja mbalimbali zenye kuonyesha mapungufu ya kiutendaji ya serikali na pengine kushauri maeneo ya kuboresha, yote ni katika kuletea maendeleo taifa letu.

ACT wazalendo pengine ni chama kinacho onekana kidogo kilicho na mbunge mmoja tu, wao wameiona fursa hii jana walikuwa na mkutano wa kidemocrasia uliokuwa na waliikwa mbalimbali, sitajikita sana ya nini kilijadiliwa ila kitendo cha ACT kufanya mkutano ule wa ndani kwa ufanisi, kinafanikiwa zaidi kujitangaza na wameonesha kuwa wanaweza kutumia fursa ndogo zilizopo kufanya mambo makubwa.

Idara za uenezi/habari/na propaganda za vyama vya siasa hasa vya upinzani zinapaswa kuwekwa watu wenye akili nyingi na wanaojua kutumia kila fursa inayojitokeza ili kuimarisha uhai wa chama.

CHADEMA ni chama kikubwa zaidi ya ACT ila idara yao ya PROPAGANDA NA UENEZI ina watu wasio na AKILI KUBWA wakati ACT WAZALENDO ni chama kidogo kuliko CHADEMA ila idara yao ya PROPAGANDA NA UENEZI ina watu makini na wenye akili nyingi.

Najiuliza CHADEMA wana hoja gani kwa wananchi? je hiyo hoja yao itatoka kwa mikutano ya hadhara na maandamano pekee?
Humu mtandaoni CDM wanamtegemea zwazwa mmoja hivi anaitwa Mmawia.....

Eti ndio think tank wao [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Kwani CHADEMA inatakiwa kufanya wanachofanya ACT au CCM,CHADEMA ni taasisi kubwa ina mipango yake kwa miaka 20 ijayo.Na hutakuja kuona "akili nyingi" ACT wakiilaza na viatu "akili nyingi" wenzao CCM,ila utaendelea kuona "akili ndogo" CHADEMA wakiendelea kuipigisha kwata CCM kila baada ya mwezi mmoja.NYIE PANGENI SISI TUNATENDA,MIPANGO SIYO MATUMIZI.
 
Kwahiyo ATC ni kama kichwa cha treni chenye taa moja kinavuta mabehewa kibao na Chadema ni meli yenye taa kibao lakini mwendopole.Mi nadhani TAA nyingi ndio ukubwa wa NURU teh....teh...teh
 
Mtoa post samahani ulitaka Chadema wafanye lini Mikutano ya ndani? Au ulitaka siku hio hio wameondoa zuio la mikutano na Chadema nao wafanye mkutano? . Ratiba za jirani yako kama una akili timamu huwezi kuhangaika nazo.
 
kumbe walitaka ruksa ndio wajipange hahahaaaaaaa
 
Mtoa post samahani ulitaka Chadema wafanye lini Mikutano ya ndani? Au ulitaka siku hio hio wameondoa zuio la mikutano na Chadema nao wafanye mkutano? . Ratiba za jirani yako kama una akili timamu huwezi kuhangaika nazo.
Hawana ratiba zozote, kazi yao imekuwa kumsakama profesa lipumba tuu.. mpaka wamesahau kilichowafanya waingie kwenye siasa.hata dovutwa kawadharau.
 
Hivi act mpinzani wenu ni chadema ama chama tawala,,,hizo akili zenu kubwa ndo zimefanya muwe na ajenda ya kupinga ipinzani wenzenu???


Mna matatizo sana
Hapa kwa mujibu wa Afande Sele unamsema Habib Mchange
 
Back
Top Bottom