CHADEMA na Uchaguzi na Lowassa wanachanganya Wanachama

Si siri tena kuwa CHADEMA inajichanganya na imechanganyikiwa.

Uchaguzi mdogo wa Songea, Longido na Singida umesusiwa na CHADEMA. Uchaguzi wa Kinondoni na Siha wanakaa vikao vya kusimamisha wagombea. Unaweza uliza nini kimebadilika mpaka sasa?

Acha kuonekana ndumila kuwili. Ina maana viongozi wetu hawajui wapi washike?

Kuhusu Lowassa inachekesha sana. Lowassa alipokwenda Ikulu kila kiongozi alimpinga kwa uwazi sana. Lema, viongozi wa BAVICHA, Mbowe na Lissu walionyesha Lowassa kutofanya vema kwenda Ikulu.

baada ya siku mbili Mbowe anasema wote waliokejeli Lowassa wamuombe radhi kwa kumtukana hadharani huku ikisema chama kina wasemaji wake wanaojulikana. Kwani tumesema mara ngapi juu ya chama kukosa msemaji ambaye tunaweza sema chama kimesema?

Kwa maana nyingine Lowassa ameonyesha hakuna wa kumsimamia tena huko. Atafanya kama anavyotaka bila wa kumkemea tena.

Hebu chama kisema msimamo juu ya uchaguzi mdogo Kinondoni na Siha, nini kimebadilika mpaka sasa?

Updates:
View attachment 679645
Wewe na Chakubanga ndio mmechanyikiwa! Subirini muziki wa watu wenye hasira na fedha zao,mtajificha uvunguni!
 
Hahahaha! Kweli wewe una uwezo mkubwa sana. Unajua kufanya majadiliano, kujibu hoja kwa mpangilio una taarifa nyingi za kweli na sahihi.

Ukiendelea kuwa hivyo utaisaidia taasisi yako na wewe utafika mbali kama individual.

Hahahahaha!

Ww jichekekeshe hapa ukidhani unajadiliana na maboya. Hiyo taasisi unayoitumikia waambie wakuongezee mshahara maana umewadhibiti watu wa hiyo taasisi unayosema ni yangu kwa hoja.
 
Ww jichekekeshe hapa ukidhani unajadiliana na maboya. Hiyo taasisi unayoitumikia waambie wakuongezee mshahara maana umewadhibiti watu wa hiyo taasisi unayosema ni yangu kwa hoja.

Mwenye kufahamu hana hasira, mwenye hoja hapaniki, mwenye hoja hayumbiyumbi, humbana mtu katika hoja moja moja.

Mwenye kufahamu demokrasia anatambua utawala wa sheria, anatambua utaratibu unaolinda haki ya mtu na pia anatambua utaratibu was kufuata katika kudai haki na kufuatilia mambo mbalimbali.

Mwenye kufahamu kamwe hawezi kulitamka neno asilolohakika nalo kwenye mjadala asije akaulizwa akakosa la kujibu.

Mwebye kufahamu hamshambulii anayejadiliana nae kwa hisia zake, kumpachika uhusika ambao hana, kumuweka katika kundi ambalo hana hakika nalo ni mshiriki au sio mshiriki.

Mwenye maarifa ana kiu ya kupata maarifa zaidi, basi huwa mtulivu anapijadiliana na mtu kwa kuamini anaweza kupata moja au mawili mapya.

Wewe una sifa zote hizo. Hongera sana.
 
Mwenye kufahamu hana hasira, mwenye hoja hapaniki, mwenye hoja hayumbiyumbi, humbana mtu katika hoja moja moja.

Mwenye kufahamu demokrasia anatambua utawala wa sheria, anatambua utaratibu unaolinda haki ya mtu na pia anatambua utaratibu was kufuata katika kudai haki na kufuatilia mambo mbalimbali.

Mwenye kufahamu kamwe hawezi kulitamka neno asilolohakika nalo kwenye mjadala asije akaulizwa akakosa la kujibu.

Mwebye kufahamu hamshambulii anayejadiliana nae kwa hisia zake, kumpachika uhusika ambao hana, kumuweka katika kundi ambalo hana hakika nalo ni mshiriki au sio mshiriki.

Mwenye maarifa ana kiu ya kupata maarifa zaidi, basi huwa mtulivu anapijadiliana na mtu kwa kuamini anaweza kupata moja au mawili mapya.

Wewe una sifa zote hizo. Hongera sana.

Nimekuambia anzisha mada yako uongoje watu wajadili kwa utashi wako. Sio kupamia za wengine kisha kulazimisha tujadili kwa utashi wako. Hapa ni kwenye jukwaa huru na wala hatujadili unavyotaka au hao unaowawakilisha. Sisi sio watoto wadogo kwamba utatuvusha barabara umetushika mkono. Server ya jf ina nafasi ya kutosha, anzisha uzi wako na sio huu ulioupamia kisha ulazimishe watu wajadili kwa kuogopa uboss wako.

Ukiulizwa hili hutoi majibu yaliyonyooka, tukifunguka unasema sio mada husika. Nimekuambia weka mikataba mezani tujadili facts unasema najificha nyuma ya mikataba. Haya basi anzisha uzi wako tuujadili unalazimisha kwenye huu usioendana na tulichovutana. Jifunze kujadiliana na watu wasiokunyenyekea, beba ya kwetu ya kijinga, changanya na kwako bora utaelewa tatizo lilipo.
 
Nimekuambia anzisha mada yako uongoje watu wajadili kwa utashi wako. Sio kupamia za wengine kisha kulazimisha tujadili kwa utashi wako. Hapa ni kwenye jukwaa huru na wala hatujadili unavyotaka au hao unaowawakilisha. Sisi sio watoto wadogo kwamba utatuvusha barabara umetushika mkono. Server ya jf ina nafasi ya kutosha, anzisha uzi wako na sio huu ulioupamia kisha ulazimishe watu wajadili kwa kuogopa uboss wako.

Ukiulizwa hili hutoi majibu yaliyonyooka, tukifunguka unasema sio mada husika. Nimekuambia weka mikataba mezani tujadili facts unasema najificha nyuma ya mikataba. Haya basi anzisha uzi wako tuujadili unalazimisha kwenye huu usioendana na tulichovutana. Jifunze kujadiliana na watu wasiokunyenyekea, beba ya kwetu ya kijinga, changanya na kwako bora utaelewa tatizo lilipo.

Mikataba ijadiliwe jf, sawa kabisa. Hilo ndilo jambo la msingi ili kila mtu afahamu kilichomo si ndio? Mikataba ina usiri gani? Mikataba ya nchi yetu sio siri. Nimekuelewa.

Kwa hiyo nianzishe mada ya mikataba au uzi was hoja ambazo hazina majibu? Asante kwa kunikumbusha kuwa katika jukwaa huru la jf ni mwiko kujadili hoja na mawazo mengine ambayo ni tofauti na heading ya Uzi. Asante sana kwa uelewa wako na maelekezo yako
 
Wameshindwa kushiriki Songea na Loliondo kwa kukosa pesa harafu waje sahizi na pesa?

Kwani Lowassa ametoa zingine mkuu.
Wewe na Chakubanga ndio mmechanyikiwa! Subirini muziki wa watu wenye hasira na fedha zao,mtajificha uvunguni!
 
Si siri tena kuwa CHADEMA inajichanganya na imechanganyikiwa.

Uchaguzi mdogo wa Songea, Longido na Singida umesusiwa na CHADEMA. Uchaguzi wa Kinondoni na Siha wanakaa vikao vya kusimamisha wagombea. Unaweza uliza nini kimebadilika mpaka sasa?

Acha kuonekana ndumila kuwili. Ina maana viongozi wetu hawajui wapi washike?

Kuhusu Lowassa inachekesha sana. Lowassa alipokwenda Ikulu kila kiongozi alimpinga kwa uwazi sana. Lema, viongozi wa BAVICHA, Mbowe na Lissu walionyesha Lowassa kutofanya vema kwenda Ikulu.

baada ya siku mbili Mbowe anasema wote waliokejeli Lowassa wamuombe radhi kwa kumtukana hadharani huku ikisema chama kina wasemaji wake wanaojulikana. Kwani tumesema mara ngapi juu ya chama kukosa msemaji ambaye tunaweza sema chama kimesema?

Kwa maana nyingine Lowassa ameonyesha hakuna wa kumsimamia tena huko. Atafanya kama anavyotaka bila wa kumkemea tena.

Hebu chama kisema msimamo juu ya uchaguzi mdogo Kinondoni na Siha, nini kimebadilika mpaka sasa?

Updates:
View attachment 679645
Longido, na Songea sababu zake za marudio ya uchaguzi mdogo zipo kisheria! Death+Kutengeliwa kimahakama

Kinondoni na Siha zipo kisheria pia ila sababu zilizopelekea marudio hayo ni utashi tu wa (mtu) wabunge ambao hakuna tatizo la kimahakama wala death!! Sasa, ukiweka mgombea katika majimbo haya mwenye nguvu na ushawishi pamoja na hoja nzito kupambana na anaerudi kwa mara ya pili kuomba tena kura wakati alipewa mara ya kwanza, ni dhahiri ushindi wake ni wa kishindo kweli kweli, zingatia anaerudi mara ya pili akiulizwa tu swali na mpiga kura wa kawaida wakati wa kampeni kwa nn ulituacha na kwa nn unarudi hivi takuwa na jibu??? mbaya zaidi selection ndo tatizo, vyovyote itakvyokuwa angewekwa mtu tofauti na yule maelezo yake yapo wazi na yanaelezeka otherwise ushindi ni asubuhi kwa opposition
 
Wameshindwa kushiriki Songea na Loliondo kwa kukosa pesa harafu waje sahizi na pesa?

Kwani Lowassa ametoa zingine mkuu.
Wewe na Chakubanga ndio mmechanyikiwa! Subirini muziki wa watu wenye hasira na fedha zao,mtajificha uvunguni!
 
Mikataba ijadiliwe jf, sawa kabisa. Hilo ndilo jambo la msingi ili kila mtu afahamu kilichomo si ndio? Mikataba ina usiri gani? Mikataba ya nchi yetu sio siri. Nimekuelewa.

Kwa hiyo nianzishe mada ya mikataba au uzi was hoja ambazo hazina majibu? Asante kwa kunikumbusha kuwa katika jukwaa huru la jf ni mwiko kujadili hoja na mawazo mengine ambayo ni tofauti na heading ya Uzi. Asante sana kwa uelewa wako na maelekezo yako

Mura toka jana nilijua ww ni mwepesi japo ulitaka kujifanya ni mwerevu. Nimekufuatilia mtiririko wa hoja zako, ninahisi ww una kaelimu fulani aidha degree ama PhD, na huenda ni boss mahali fulani hivyo hata kwenye mijadala yako huko ulipo watu hujadili na ww kwa kukunyenyekea au kukubali kila usemacho hata kinafiki. Kwa sababu hiyo huwa huwa hukutani na challenge hivyo kujihisi ni mwerevu.

Sasa leo naona unajichanganya tu, jana ulisema tujadili mada iliyoko mezani na ukawa unanikebehi kwamba najadili mtu na ww unajadili hoja. Nikakuambia kama hoja ni hiyo tunayovutana sio hoja iliyopo kwenye maudhui ya mleta hoja. Nikakuambia unataka tubaki kwenye hoja moja bila kudadavua vizuri anzisha yakwako ulazimishe watu wajadili utakavyo. Saa hii unasema hujui kama ni kosa kujadili nje ya mada. Kipi ni kipi na ulikuwa unaniwekea mipaka jana ya nini. Humu jukwaani tunajidili randomly ili mradi ni siasa na kuboresha mjadala, ningejadili ufugaji wa samaki hapo ningekuwa niko nje.

Kutaka kukuonyesha kichwa chako kimetengana na kiwiliwili ni pale unaposema mikataba kijadiliwa humu jf. Jana uliniambia tujadili facts, nikakuambia facts ziko kwenye mikataba, kinyume na hapo tunajadili tulichoambiwa na watu kisha tunajiongeza. Ukalazimisha una facts nikakuambia hiyo mikataba ya siri ilipaswa kupelekwa bungeni, kisha wabunge watupe mrejesho. Sasa siri hata kwa wawakilishi wetu na bado unanirushia mate hapa jukwaani kwamba unajadili facts!?

Nikurahisishie, ww ni mwepesi kwenye mijadala huru japo una uelewa fulani wa mambo. Tatizo lako aidha una ulevi wa madaraka au kiburi cha elimu na vijihela vya kumalizia uzee vizuri, hivyo unaamini asiyejadili unavyotaka ni mjinga.
 
Vyama vya siasa ni mali ya watanzania wote. Chadema wa leo anaweza kuwa ccm wa kesho na kinyume chake. Hivyo basi in wajibu was kila mmoja wetu kuhakikisha ubora uimara was vyama hivi kwani ikitokea kimepata kiti au kimeshika dola kitakutawala na kukuongoza pasipo kujali kama wewe ni muumini au mwanachama wake
Sawa
 
Si siri tena kuwa CHADEMA inajichanganya na imechanganyikiwa.

Uchaguzi mdogo wa Songea, Longido na Singida umesusiwa na CHADEMA. Uchaguzi wa Kinondoni na Siha wanakaa vikao vya kusimamisha wagombea. Unaweza uliza nini kimebadilika mpaka sasa?

Acha kuonekana ndumila kuwili. Ina maana viongozi wetu hawajui wapi washike?

Kuhusu Lowassa inachekesha sana. Lowassa alipokwenda Ikulu kila kiongozi alimpinga kwa uwazi sana. Lema, viongozi wa BAVICHA, Mbowe na Lissu walionyesha Lowassa kutofanya vema kwenda Ikulu.

baada ya siku mbili Mbowe anasema wote waliokejeli Lowassa wamuombe radhi kwa kumtukana hadharani huku ikisema chama kina wasemaji wake wanaojulikana. Kwani tumesema mara ngapi juu ya chama kukosa msemaji ambaye tunaweza sema chama kimesema?

Kwa maana nyingine Lowassa ameonyesha hakuna wa kumsimamia tena huko. Atafanya kama anavyotaka bila wa kumkemea tena.

Hebu chama kisema msimamo juu ya uchaguzi mdogo Kinondoni na Siha, nini kimebadilika mpaka sasa?

Updates:
View attachment 679645
Shit hole
 
Ukisikia chama kile ni cha Kasi kazini usibishe. Kina wenyewe na wenyewe ndiyo hao. Singida na chadema wapi na wapi. Serikali imara itatokana na ccm. Wengine majanga tu
 
Mkuu hilo wenye akili wote walijua ni obvious.
Umesahau hata kumuunga mkono Kenyata alianza yeye kutoa tamko ndipo
baadaye kamati kuu ikakaa kupitisha?
kwenye chama siku zote kabla "mabadiliko" hajatubadilisha tulikuwa tukimuunga mkono Odinga.
Wewe ni msema kweli usiyeangalia uchama
Wengi wenu mngekuwa hivyo Chama chenu kisinheyumba km ilivyo sasa
 
Kwani Longodo ilikuwa kusini mkuu. Cha msingi ni maslahi gani yamekuwepo hapa hata kuachana na imani yao ya kuibiwa na kutokuwa na tume huru.
Ukisikia chama kile ni cha Kasi kazini usibishe. Kina wenyewe na wenyewe ndiyo hao. Singida na chadema wapi na wapi. Serikali imara itatokana na ccm. Wengine majanga tu
 

Maarifa ni nguvu, maarifa ni mamlaka. Mtu mwenye maarifa ana mamlaka.

Nimependa unavyotumia mamlaka yako yanayotokana na maarifa kujenga hoja zako makini.

Watu waso maarifa hawafahamu kabisa kuwa facts zipo kwenye mikataba tu. Watu wa namna hii wanahitajika wapewe mikataba waisome ili wapate facts, maana facts zipo kwenye mikataba. Asante kwa kunipa kitu kipya!
 
Back
Top Bottom