CHADEMA na ubunge 2020


Lakini unajua nini Komredi...?

Vipi kuhusu kitu kama ile 'Arab spring'?

Mbona ilimng'oa yule Hosni Mubarak wa Misri na yule Ben Ali wa Tunisia...

Tatizo ninaloliona kuhusu hapa kwetu ni uoga.

Tulio wengi hatupo tayari kupoteza damu zetu, maisha yetu, au hata kutandikwa mijeredi na kupigwa virungu vya polisi katika kudai haki zetu.

Mimi naamini kabisa kuwa mwisho wa siku sisi wananchi tuna nguvu kuliko polisi, jeshi, Magufuli, na CCM.

Tukiamua kuwatoa watatoka tu ingawa pia watu watalipa gharama kubwa sana.

Hebu ona kwa mfano kule Zimbabwe...yaani kile kibabu kinawapeleka puta hadi watu wanaishia kukamata panya ili wamfanye kitoweo lakini cha kushangaza eti bado kipo madarakani!

Hivi kweli unadhani Wazimbabwe wakiamua na kusema sasa basi imetosha...kile kibabu unadhani kitaendelea kuwepo madarakani?

Tatizo letu sisi Waafrika wa huku kusini mwa Sahara wengi wetu tuko waoga sana.

Waarabu huwezi ukawafanyia huo ujinga ujinga aisee....watajilipua wenyewe na kukulipua wewe.

Unakumbuka jinsi UKUTA ulivyochimbiwa biti na hatimaye ukaishia kuporomoka wenyewe?

Kwa kweli saa ingine hata sisi wananchi ni wa kulaumiwa kwa kuwaendekeza hawa viongozi.

Sisi wananchi tupo wengi mno kushinda hayo majeshi yao, tupo wengi kushinda usalama wa taifa, tupo wengi kushinda CCM.....lakini tunavyopelekeshwa sasa....

Hata sisi kwa kiasi chetu tunastahili lawama....
 
Hata wakiweka mikakati mizuri naamini 2020 wataivuruga tena kwa tamaa za wachache. (gia ya angani)Tunakuwa nao pamoja kwenye kujenga lkn wakioneshwa pesa ni wepesi kututenga wajengaji na kuwakaribisha wabomoaji.
 
Hata chaguzi zilizopita walipata viti mahali na mahali ila walinyang'anywa ushindi the issue is watazuiaje Cruelness ya CCM kuiba kura na pia wajipange kuweka watu sahihi sio waliokatwa uko ndo waje uku au watu wasiojua hata wanapogombea ni wapi
 
Ewaaa... hapo umesema vema komredi.

Ila mwenzangu uko ughaibuni hii comment haiwezi kukuweka matatani.

Nachelea kusema naiunga mkono kwa maana kesho sichelewi kupelekwa ununio kule wakani-Roma Mkatoliki.

Ulichosema ndio ukweli mtupu. Bila njia hiyo, tutaendelea kubaki na sera zetu za zidumu fikra za mwenyekiti.

Miafrika Ndivyo Tulivyo: Source Usa Baby
 
Kuwa kweli na nafsi yako, unaona dalili au mkakati wowote wa CDM kuongeza majimbo 2020 ?
Ni wazi 2020 CDM wanaenda kupoteza majimbo mengi, na Dsm ndio watakaongoza kwa kupokonywa majimbo, visingizio vitakuwa lukuki ila ukweli ushajulikana.
Kuota ndoto ni haki yako ila usipoteze muda kulazimisha iaminiwe.
Wenzio wanaoogopa hata mikusanyiko yoyote ya upinzani, wanajua vizuri zaidi wanachokiogopa kuliko wewe. Ukienda kuwaeleza haya utanyimwa posho na kufukuzwa uanachama.
 

Mkuu ulivyobadilika inashangaza sana. Sijui kama yale uliyokuwa ukiyapigania miaka yote utayapata kwa utawala huu wa Magufuli hata kwa 10%. Nategemea utarudi tu kuwa mlalamikaji. Muda utaamua.
 
Ni matokeo ya utafiti au porojo za kutafutia posho? Weka hadharani BASI huo utafiti wako.
 
Boss Nyani Ngabu Pale Mwana CCM anaposhauri CHADEMA. Hii ina maana gani? Unaitakia mema Chadema? Umeichoka CCM? Unataka CCM wawe Wapinzani 2020. Bado sijakuelewa Boss.

Ungetaka kuwashauri, anza na Msingi mwenyewe. Washauri Upinzani wote Waungane. Den wasimamishe Mgombea mmoja kwa kila Kijiji, Kata, Mtaa, Wilaya, Mkoa. Kila Mahali ni Mgombea Mmoja tu Vs CCM.

Ukimaliza hapo pia washauri wawe na Mgombea mmoja tu wa Urais. Anayekubalika na kuuzika. Awe damu changa, anayeweza Mziki wa Ngosha. Anayeweza kupiga Push Up. Otherwise 2020 mambo ni yale yale.

 
sahihi sana inatakiwa chama kiangalie hili,kingine si kuokoteza ama kutegemea viongozi waliohama chama au kutoka chama tawala kuja kwao kwamba ndo wawe wagombea wakati CDM ina vijana wengi wanaweza kujenga hoja.so ni jukumu lao kwa pamoja kuliangalia na kutafuta viongozi wa ndani katika kila jimbo.
 

Mimi ni mwana CCM?

Unaumwa wewe!
 
Je,Tume huru ipo?
Yani mteule wa rais DED ndo anatangaza matokeo ya mwisho ya ubunge!!!


Tume huru idaiwe mapema ccm itoke vinginevyo watanzania mtapata tabu sana.
 

Hayo yote uliyosema cdm wanayajua vizur sana. Je unadhan ccm ni wajinga wayakuli hayo unayosema. Ivi unadhan kama Mungu angesimamia uchaguzi uliopita ccm wangekua madarakani leo?
 
Hiyo bidii yako ya ushawishi uitumie zaidi huko kwenu. Wingi wenu hauna faida kwa maendeleo ya taifa, mmekalia KUUTUMIA kutuletea sheria na mikataba mbofumbofu halafu kuunda kamati magumashi kuchunguza madhara mloleta wenyewe.
 
Hivi mshafukuza wangapi vile? Uchambuzi bado waendelea.
 
Hivi kwa nini kila siku hapa tunaongelea CHADEMA na jinsi itakavyoshindwa uchaguzi lakini hatuongelei sera za CCM na nini wanafanya kumkomboa Mtanzania. Kuna mtu hapa anaweza kunieleza sera za utawala wa Magufuli kwenye kilimo? Je ana mpango gani na hii sekta inayotoa ajira kwa zaidi ya 80 percent ya Watanzania? Kilimo sehemu nyingi duniani kinakuwa subdize na serikali...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…