CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

CHADEMA na polisi katika mtifuano mkali

THE COMMISSIONER

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2012
Posts
267
Reaction score
111
Huku Jeshi la polisi nchini likiamua kutumika vibaya na Chama cha Mapinduzi na Serikali yake kwa kupiga marufuku maandamano kwenye mikoa yote yalikopangwa kufanyika, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimeendelea kusisitiza na kulitaka jeshi la polisi kutambua hivyo kuwa maandamano yako pale pale.

Taarifa iliyotelewa kwa vyombo vya habari na jeshi la polisi kwa jiji la Dar es salaam zinadai kuwa haliwezi kuruhusu maandamano hayo kwa kuwa kuna ugeni wa rais wa China siku hiyo lakini CHADEMA wamedai kuwa Rais wa china yuko hapa nchini kwa maslahi ya nchi yake na wao CHADEMA wako kwenye shughuli zao kwa maslahi ya nchi ambazo hazina mausiano yoyote na rais huyo wa china.

Kwa upande wa Arusha Jeshi la polisi linadai kuwa haliwezi kuruhusu maandamano hayo kwa kuwa CCM nao wameomba kufanya maandamano siku hiyo kwenye barabara hizo hizo walizoomba CHADEMA kwa nia ya kuipinga CHADEMA na msimamo wao wa kumtaka waziri ajiuzulu. Taarifa zinaendela kusema kuwa CHADEMA wameliambia Jeshi la polis mkoani huo kuwa hakitatetereka katika msimamo wake na kwamba ni jukumu la jeshi la polisi kupanga barabara tofauti zitakazotumika na vyama hivyo na kwamba wao CHADEMA wataendelea na maandamano yao katika barabara zile walizozipanga na kama wanawahusudu sana CCM basi wawapangie barabara tofauti.

Jijini Mbeya hali insemekana kuwa tete kwani kila mmoja yaani polisi na CHADEMA wameonyesha misimamo mikali na tayari taarifa zinadai kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ameamua kufanya kikao na wachungaji na maaskofu ili kuwaomba wawatangazie watu kwenye ibada za kesho kuwa wasijitokeze kwenye maandamano hayo kwani yataatarisha amani. Kwa upande wa CHADEMA wameendelea kulieleza jeshi la polisi kuwa adhma ya maandamano ya kuomngo'oa Kawambwa iko pale pale iwe mvua ama jua.

Pia taarifa kutoka makao makuu zilizosambazwa kwa vyombo vya habari leo hii na zimeeonyesha vikosi vitakavyoongza maandamano hayo ambapo kwa upande a Jiji la Dar es Salaam, Mwenyekiti wa CHADEMA Tiafa Freeman Mbowe akisindikizwa na wabunge wote wa Dar es salaam watawaongoza wananchi kuelekea kwa waziri mkuu.

Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Slaa, Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi na Mbunge Sugu watakuwa jijini Mbeya, wakati Mwenyekiti wa BAVICHA Tifa John Heche, Tundu Lisu, na Godbless Lema watakuwa jijini Arusha na kwa upande wa Mwanza Mwenyekiti wa Wazee Taifa Nyangaki Shilungushela na Ezekeia Wenje Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Hata hivyo taarifa zinasema Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema anatarajia kukutana na uongozi wa CHADEMA Taifa ili kuwaangukia kusitisha nia yao hiyo kwa kuwa nchi iko kwenye ugeni mzito jambo ambalo linasemekana kuwa CHADEMA hawako tayari kusikia chochote juu ya hilo.​
 
Kamanda The Commissioner

Uko sawasawa kwa kiasi kikubwa mno. Waratibu wa maandamano na mgomo huo siku ya Jumatatu, BAVICHA kupitia kwa Katibu wa Baraza hilo taifa, Deo Munishi, wametuma taarifa kwa vyombo vya habari wakitoa tahadhari kwa Jeshi la Polisi kuacha kuwa kichocheo cha vurugu siku hiyo, badala yake litimize wajibu wake wa kulinda raia na mali zao.

Amesema kuwa uongozi wa chama katika kanda husika ambako watu wake watakutana kwenye centre moja kwa ajili ya shughuli hiyo, umeshafanya mawasiliano na Jeshi la Polisi kwa maana ya kutoa taarifa ili kuhakikisha uwepo wa ulinzi wa raia na mali zao.

Wamesisitiza siku zote CHADEMA kimekuwa kikiitisha maandamano ya amani, ambayo yamekuwa yakifanyika bila rabsha yoyote, isipokuwa pale ambapo Jeshi la Polisi linapotumwa au kutumika vibaya, kuvuruga na kusababisha fujo! Mifano iko hai.

Wamesisitiza pia kuwa, kama alivyosema Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe, maandamano hayo ni ya Watanzania wote wanaoipenda nchi yao. Itakumbukwa Mwenyekiti alisema yatamhusu kila mtu, waendesha daladala, bodaboda, mamantilie, walimu, wanafunzi (wote kuanzia msingi hadi vyuo vikuu), wasukuma mikokoteni, madaktari na wengine wote, watu wa kada zote nchini.
 
Hapa Magamba hawana ujanja,polisi wapeleke vifaa kumlinda Rais bandia wa china ama watumike kuwaua wazalendo wanaopaza sauti zao
 
Huo ugeni unaathiri nini?Rais wa China anakuja kwa maslahi ya Taifa lake.Hapa CHADEMA wanaongelea maslahi ya taifa letu na vizazi vijavyo

Watoto wamefeli na hatuwezi kuandaa mazingira ya wadogo Zetu na kuwa manamba ndani ya nchi yao watakapowekeza wageni anaokuja kuwatetea kwenye hiyo mikataba ya kinyonyaji watakayosaini na rais wa China

Ukipita Kariakoo utakutana na wamachinga wa kichina ambao wanaziba hata fursa kwa wamachinga na wadogo zetu waliofeli kidato cha nne kujipatia riziki yao.

Tuendeleze vuguvugu bila kurudi nyuma
 
Kamanda The Commissioner

Uko sawasawa kwa kiasi kikubwa mno. Waratibu wa maandamano na mgomo huo siku ya Jumatatu, BAVICHA kupitia kwa Katibu wa Baraza hilo taifa, Deo Munishi, wametuma taarifa kwa vyombo vya habari wakitoa tahadhari kwa Jeshi la Polisi kuacha kuwa kichocheo cha vurugu siku hiyo, badala yake litimize wajibu wake wa kulinda raia na mali zao.

Amesema kuwa uongozi wa chama katika kanda husika ambako watu wake watakutana kwenye centre moja kwa ajili ya shughuli hiyo, umeshafanya mawasiliano na Jeshi la Polisi kwa maana ya kutoa taarifa ili kuhakikisha uwepo wa ulinzi wa raia na mali zao.

Wamesisitiza siku zote CHADEMA kimekuwa kikiitisha maandamano ya amani, ambayo yamekuwa yakifanyika bila rabsha yoyote, isipokuwa pale ambapo Jeshi la Polisi linapotumwa au kutumika vibaya, kuvuruga na kusababisha fujo! Mifano iko hai.

Wamesisitiza pia kuwa, kama alivyosema Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe, maandamano hayo ni ya Watanzania wote wanaoipenda nchi yao. Itakumbukwa Mwenyekiti alisema yatamhusu kila mtu, waendesha daladala, bodaboda, mamantilie, walimu, wanafunzi (wote kuanzia msingi hadi vyuo vikuu), wasukuma mikokoteni, madaktari na wengine wote, watu wa kada zote nchini.

Kamanda Makene tunashukuru kwa ufafanuzi huo. Kwa kuwa ninyi mnawasiliana na wenzenu wa Mbeya na Meneo mengine tunaomba utupe update za maeneo hayo kwa tumearifiwa kwa Upande wa Mbeya poli na CHADEMA kila mtu anashilikia masimamo wake na kwamba polisi wamewakataza wenye magari ya vipaza sauti kutangaza maandamano hayo.
 
ziara ya china haina maslah yoyote kabisa,CHADEMA please move foward.
 
Huo ugeni unaathiri nini?Rais wa China anakuja kwa maslahi ya Taifa lake.Hapa CHADEMA wanaongelea maslahi ya taifa letu na vizazi vijavyo

Watoto wamefeli na hatuwezi kuandaa mazingira ya wadogo Zetu na kuwa manamba ndani ya nchi yao watakapowekeza wageni anaokuja kuwatetea kwenye hiyo mikataba ya kinyonyaji watakayosaini na rais wa China

Ukipita Kariakoo utakutana na wamachinga wa kichina ambao wanaziba hata fursa kwa wamachinga na wadogo zetu waliofeli kidato cha nne kujipatia riziki yao.

Tuendeleze vuguvugu bila kurudi nyuma
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii
 
Nchi za wenzetu mgeni wanapokelewa kwa maandamano.huku kwetu mkara kwenda mbele.

Sijui kama Kikwete anajifunzaga mambo kwenye hizo tripu anazoendaga Ulaya na America. Watu huandamana hata kama kuna malaika kutoka mbimguni ataitembelea nchi hiyo pale hao wanaoandamana wana sababu za kuandamana hata kama ni za kikumbavu kiasi gani na vyombo vya usalama vinakuwapo kuangaalia usalama tu.

Kwa sababu hii eti kuna ugeni wa RAIS WA CHINA kunadhihirisha jinsi Kkwete anavozururaga tu huko nje na hizo ziara hazimsaidii chochote.
 
Hongereni sana Chadema.Wananchi tuko pamoja na nyie.
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii

Hivi na wewe una la kusema ama unataka kujikomba tu.

Inaonekana akili yako fupi kama ya serikali ya chama chako ambao hawajui kutofautisha Maandamano ya Amani na ya vurugu. Wewe kama serikali yenu kwa akili zenu fupi mmeshindwa kuona ni kwa kiasi gani mlvyoathiri maisha ya watoto wa Watanzania kwa kuwafelisha. Wewe mwenyewe serikali yako imekufanya ukawa na akili fupi kwa kukufelesha. Mwenyewe uliambualia division ya aibu.

Unaandika hapa ukiwa Uingereza wakati wanaume CHADEMA wanapambana hapa nyumbani kupigania elimu ya wadogo zakouliowaacha hapa Tanzania ili wasije wakawa kilaza kama wewe.
 
Hivi unadhania nchi inaweza kuendelea bila wawekezaji?
Tatizo lenu nyie mnataka attention sana na mnaitafuta hii attention bila kujali waathirika wa haya maandamano na vurugu zenu, Wakipoteza maisha mnachofanya ni kuzunguka na picha zao kuonyesha huko waliko wawekezaji. mnataka nchi ionekane ina machafuko. Wewe unadhani nani mjinga atawekeza kwenye nchi yenye machafuko?
Hebu tafuteni kazi za kufanya manake sasa mmeanza kuwa kero kwa jamii

jiheshimu, umeingia choo cha kike!
 
Hivi na wewe una la kusema ama unataka kujikomba tu.

Inaonekana akili yako fupi kama ya serikali ya chama chako ambao hawajui kutofautisha Maandamano ya Amani na ya vurugu. Wewe kama serikali yenu kwa akili zenu fupi mmeshindwa kuona ni kwa kiasi gani mlvyoathiri maisha ya watoto wa Watanzania kwa kuwafelisha. Wewe mwenyewe serikali yako imekufanya ukawa na akili fupi kwa kukufelesha. Mwenyewe uliambualia division ya aibu.

Unaandika hapa ukiwa Uingereza wakati wanaume CHADEMA wanapambana hapa nyumbani kupigania elimu ya wadogo zakouliowaacha hapa Tanzania ili wasije wakawa kilaza kama wewe.
Nani alikuambia mie nilifeli?
Sio kuandika unatokwa povu tu bila kutumia akili.
Haya ukiandamana kesho halafu....
Au unadhani baada ya kuandamana ndio watabadilisha hiyo sifuri yako kuwa Division one?
Tatizo lenu mnakurupuka tu kufuata upepo bora DJ kasema muandamane basi woote mnaingia mitaani kama wale wafuasi wa ponda , matokeao yake mnaishia jela. Na ukiwa jela usidhani kama chadema watakuletea ndizi huko. muulize Ludovick
 
Huo ugeni unaathiri nini?Rais wa China anakuja kwa maslahi ya Taifa lake.Hapa CHADEMA wanaongelea maslahi ya taifa letu na vizazi vijavyo

Watoto wamefeli na hatuwezi kuandaa mazingira ya wadogo Zetu na kuwa manamba ndani ya nchi yao watakapowekeza wageni anaokuja kuwatetea kwenye hiyo mikataba ya kinyonyaji watakayosaini na rais wa China

Ukipita Kariakoo utakutana na wamachinga wa kichina ambao wanaziba hata fursa kwa wamachinga na wadogo zetu waliofeli kidato cha nne kujipatia riziki yao.

Tuendeleze vuguvugu bila kurudi nyuma
Hivi wewe bado upo uraiani?Hujaungana na mkurugenzi wako?Vipi utashiriki au utakuwa unaulizia UPDATE nyuma ya key board wakati wananchi wasio na hatia wakiumia?Familia yako itashiriki?Mkiti nasikia ameenda DUBAI!
 
Hii nchi hata wakichukuwa vyama vingine,hakuna ujanja ni lazima tufungue milango ili tuweze kupata wawekezaji ambao watasimamiwa vyema na kuifanya Tanzania isonge mbele.kwa dunia ya sasa bila kufungua milango huwezi kwenda mahali,bila kuwa na ushirikiano na nchi nyingine huwezi kusonga mbele,ufike wakati tukubali kuwa maendeleo ya sasa yanahitaji wawekezaji wawe wa ndani ama wa nje.
Nakubaliana na maandamano hayo,lakini ni vyema tuelewe kuwa Tanzania inahitaji wawekezaji wa kweli na kwa sasa wawekezaji wa kweli ni kutoka uchina na si ujerumani wala uingereza wala USA.
Cha msingi hapa ni kuwa makini ktk kile tukifanyacho,ktk swala la utaifa tusimame kwa pamoja na ktk maswala ya uvyama hainashida mkipambana maana kila chama kinataka kushika dola na hii ni kwa kila chama cha siasa ktk nchi yeyote ile.
 
Nani alikuambia mie nilifeli?
Sio kuandika unatokwa povu tu bila kutumia akili.
Haya ukiandamana kesho halafu....
Au unadhani baada ya kuandamana ndio watabadilisha hiyo sifuri yako kuwa Division one?
Tatizo lenu mnakurupuka tu kufuata upepo bora DJ kasema muandamane basi woote mnaingia mitaani kama wale wafuasi wa ponda , matokeao yake mnaishia jela. Na ukiwa jela usidhani kama chadema watakuletea ndizi huko. muulize Ludovick
Unafikiri CHADEMA wanafikiri kwa kutumia masaburi kama wewe na chama chako.
Utatumika saaana kwa kuwa ulinyimwa elimu ambayo ndio CHADEMA wanaipigania. Halafu wewe tulia mambo ya Tanzania hayakuusu kwa kuwa wewe si mtanzania. Ama unabisha?
 
Back
Top Bottom