CHADEMA na mbio za mwenge

CHADEMA na mbio za mwenge

Nao wengine waliovaa sare za CHADEMA wote hao ni wabunge wa Iringa Mjini hivyo walipaswa kuwepo uwanjani? Kwani wabunge wanapotoka nje ya bunge huwa hawahusiki na kikao cha bunge kinachokuwa kinaendelea?

Mkuu Kigarama usisahau kuwa leo ni kumbukumbu ya kifo cha baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na maadhimisho ya kitaifa yamefanyika Iringa.

Sasa kwakuwa serikali imechanganya matukio yote mawili ndio maana unawaona makamnda hapo uwanjani na kudhani kuwa wameenda kuadhimisha mwenge kitu ambacho si sahihi.
 
kwani wanaouza kitimoto wengi dar ni wakristo pekee?
nawajua weng tu wanaouza tena wenzangu wazuri tu wa swala...tuache hii
Unaamisha Msigwa hajiamini?
naona bado hatujaelewana philosofia yangu
Watamwekaje mtu asieutaka mwenge huo usio na faida kwa sasa aubebe?
Hata mimi sitaubeba wala kuuchangia ni upotevu wa hela na muda.
Ni Tanzania pekee bado tunaabudu litochi hili,,na wenye akili na wasomi bado wamo huko huko kusapoti ujinga.
liwekwe makumbusho ya taifa,
dhana nzima ya mwenge haipo tena wanaoubeba ndio hao hao wezi na mafisadi
sasa utammulika nani???


Vipi ukisikia kuna Sheikh anauza Kitimoto ingawa hali, wewe utamuelewaje? Jibu lake likiwa ni kwamba wanaouza ni watu wengine yeye anachukua hela tu, utamuonaje? self denial ni kitu kibaya sana. Leo kwenye Ratiba kulikuwa kunaonyesha kwamba Msigwa ataubeba Mwenge halafu yeye akakataa?
 
Mkuu Kigarama usisahau kuwa leo ni kumbukumbu ya kifo cha baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na maadhimisho ya kitaifa yamefanyika Iringa.

Sasa kwakuwa serikali imechanganya matukio yote mawili ndio maana unawaona makamnda hapo uwanjani na kudhani kuwa wameenda kuadhimisha mwenge kitu ambacho si sahihi.

Mkuu Mwita,
Hata mimi ningeamini hivyo ulivyonena bahati mbaya haikuwa hivyo kwa mheshimiwa huyu mchungaji. Msigwa kashiriki bega kwa bega kuanzia kukabidhiwa mwenge kwa Manispaa ya Iringa hadi Taifani.
 
labda tujiulize Msigwa kaenda kwa sababu ya kuzima mwenge
au kaenda kwa vile mwenge huo umezimwa katika jimbo lake?
ametumia busara kuwakilisha wananchi wake mbele ya rais.
Kuna mawili hapo kuukata mwenge na kuwakilisha wananchi mbele ya rais wao.
unaweza kuingia kanisani kwa heshima hata kama wewe sio mkristo wa dhehebu lile kama lengo ni uwakilisho wa jumuia yako.Haimaniishi kuwa pale anasapoti hilo litochi.
Well Stated.
 
Mkuu Mwita,
Hata mimi ningeamini hivyo ulivyonena bahati mbaya haikuwa hivyo kwa mheshimiwa huyu mchungaji. Msigwa kashiriki bega kwa bega kuanzia kukabidhiwa mwenge kwa Manispaa ya Iringa hadi Taifani.
Hacha uongo wewe! Weka picha yoyote ambayo Msigwa kashika mwenge. Yeye kaenda kuazimisha miaka 14 ya kifo cha mwl Nyerere na ndo maana hajavaa hizo pamba za Mwenge. CCM hacheni siasa za majitaka haziwasaidii
 
Chadema haikubaliani na mwenge na ndio maana nimeshangaa kumuona Mch. Msigwa kwenye hii shughuli.
Msigwa kaenda kuazimisha miaka 14 ya Mwl Nyerere siyo kwa ajiri ya ilo limoto sijui karabai
 
Mkuu Mwita,
Hata mimi ningeamini hivyo ulivyonena bahati mbaya haikuwa hivyo kwa mheshimiwa huyu mchungaji. Msigwa kashiriki bega kwa bega kuanzia kukabidhiwa mwenge kwa Manispaa ya Iringa hadi Taifani.
Msigwa hakuufata mwenge, mwenge umemfuata msigwa!
 
Vipi ukisikia kuna Sheikh anauza Kitimoto ingawa hali, wewe utamuelewaje? Jibu lake likiwa ni kwamba wanaouza ni watu wengine yeye anachukua hela tu, utamuonaje? self denial ni kitu kibaya sana. Leo kwenye Ratiba kulikuwa kunaonyesha kwamba Msigwa ataubeba Mwenge halafu yeye akakataa?
Sasahapa hoja yako ni ipi na unashangaa nini? Kakataa kuubeba kwasababu hausapoti FULL STOP. Yeye alienda pale kuazimisha miaka 14 ya kifo cha Mwalimu kama Mbunge na Kiongozi wa Chadema. Hacha uzandiki!
 
Mleta mada anastahili apimwe.akili kama ziko sawasawa maana mambo mengine yanahitaji fikira pevu. Mwenge wanaupinga ili uachwe.uache kumaliza pesa za walipa kodi wameona kasoro. Lakini Leo hii ado mwenge uko.kihalali na upo jimboni kwa.msigwa kuzimwa kufika kwake sinongwa yeye ni.kiongozi.wa.pale.

Hivi nani asiyejua kwamba vyama vya upinzani vingi vinapinga katiba iliyopo na tume ya uchaguzi. Hivi wangesema waache kugombea kwa vile katiba na tume havijabadilishwa wangekuwa wapi. Mambo mengine use common sense.
 
Kumbe ni " kuzima mwenge"? Yes alipaswa kuwepo kuhakikisha unazimwa kabisa, tena daima. Kama angekwenda kushangilia unapowashwa nisingemuelewa!!!!!!!
 
Vijana wa Chadema watakujibu mimi sina chama
ninaujua msimamo wa Msigwa na pia ni mtu anaejua umuhimu wa uwakilishi.
Kumsusia rais sio jambo jema akiwa jimboni mwake
yeye hana ugomvi na JK ana ugomvi na mwenge.
labda nikuulize kama huli kitomoto kisha nkakualika kwangu kwa mazungumzo hutakuja kwa vile nakula kitimoto??
utakuja tutaongea lakini kitimoto changu hutakigusa na hakitakuathiri ukiwepo...
Kama tungemuona Msigwa akiunyanyua mwenge huo ndio tungehoji uhalali wa kauli zake kama anasimamia anachosema

Mchungaji Msigwa ni kigeugeu tarehe 13.10.2013 alikuwepo maeneo ya Stand Kuu ya Mabasi pia kwa nyakati tofauti alienda kwenye kijiwe cha CDM maeneo ya Mashine za Mchele Mlandege,kwa mdomo wake aliwaambia VIjana wasusie kwenda kwenye Mwenge WAWEPO WATU WACHACHE kisha serikali itaona kuwa watu wa Iringa hawaupendi Mwenge,na aliwanunua kwa kuwapa Bendera mpya na kofia.Ameproove failure kwa kuwa vijana wengi ndo walikuwa mstari wa mbele hata wengine walidiriki kusema walikubali kwa kumbeza,kisha wakahudhuria na kumuomba kupiga naye picha huku wakimuuliza HAA MHESHIMIWA KUMBE ULIKUWEPO
 
kuna mambo mawili ya kutenganisha ni kuhudhuria na kutounga mkono mamabo ya mwenge kukimbizwa.mhe.msigwa kama mbunge wa eneo husika na kwa kuwa kulikuwa na wageni ilikuwa lazima kuhudhuria.Lakini maamuzi ya kuendeleza upuuzi wa kukimbiza mwenge hadi leo na kwa sababu malengo ya mwenge leo hii ni gheresha chadema ikiwa na uwezo wa kuamua mambo ya nchi kwa maana ya kuongoza dola mambo ya kwanza kabisa kuondoa ni pamoja na mwenge wa uhuru.huo ndio msimamo wa chama.kwa sasa kwa maeneo mbali mbali kila kiongozi anaweza kuhudhuria au kutohudhuria si lazima na ndio maana mhe msigwa hakutoa kauli ya kusifia mwenge kwa niaba ya chama.
 
uthibitisho wa ulichoandika tupatie? picha au documentary evidence akitoa hizo kauli na akihonga vvijana
la sivo huna tofauti na mashambenga wengine wasio na kazi
ya kufanya mitaani kazi yao kutunga maneno kutwa nzima

Mchungaji Msigwa ni kigeugeu tarehe 13.10.2013 alikuwepo maeneo ya Stand Kuu ya Mabasi pia kwa nyakati tofauti alienda kwenye kijiwe cha CDM maeneo ya Mashine za Mchele Mlandege,kwa mdomo wake aliwaambia VIjana wasusie kwenda kwenye Mwenge WAWEPO WATU WACHACHE kisha serikali itaona kuwa watu wa Iringa hawaupendi Mwenge,na aliwanunua kwa kuwapa Bendera mpya na kofia.Ameproove failure kwa kuwa vijana wengi ndo walikuwa mstari wa mbele hata wengine walidiriki kusema walikubali kwa kumbeza,kisha wakahudhuria na kumuomba kupiga naye picha huku wakimuuliza HAA MHESHIMIWA KUMBE ULIKUWEPO
 
Mchungaji Msigwa ni kigeugeu tarehe 13.10.2013 alikuwepo maeneo ya Stand Kuu ya Mabasi pia kwa nyakati tofauti alienda kwenye kijiwe cha CDM maeneo ya Mashine za Mchele Mlandege,kwa mdomo wake aliwaambia VIjana wasusie kwenda kwenye Mwenge WAWEPO WATU WACHACHE kisha serikali itaona kuwa watu wa Iringa hawaupendi Mwenge,na aliwanunua kwa kuwapa Bendera mpya na kofia.Ameproove failure kwa kuwa vijana wengi ndo walikuwa mstari wa mbele hata wengine walidiriki kusema walikubali kwa kumbeza,kisha wakahudhuria na kumuomba kupiga naye picha huku wakimuuliza HAA MHESHIMIWA KUMBE ULIKUWEPO

Bidyabalevya, mmesha ambiwa kulikua nashughuli mbili. ya uzimaji mwenge na kumbukumbu ya baba ww taifa serikari ilia muakufanyazote kwa pamoja. Mbona Wewe na mwenzako maboso mnalazimisha Kuwa Msigwa alienda kwaajili ya Mwenge wakati si kweli. Mnaanza kuonyesha Mnachuki tu ninyi.
 
labda tujiulize Msigwa kaenda kwa sababu ya kuzima mwenge
au kaenda kwa vile mwenge huo umezimwa katika jimbo lake?
ametumia busara kuwakilisha wananchi wake mbele ya rais.
Kuna mawili hapo kuukata mwenge na kuwakilisha wananchi mbele ya rais wao.
unaweza kuingia kanisani kwa heshima hata kama wewe sio mkristo wa dhehebu lile kama lengo ni uwakilisho wa jumuia yako.Haimaniishi kuwa pale anasapoti hilo litochi.
Khaa!! mnazungukazunguka tu na kutoa sababu nyingi juu ya huo mwenge. Mnadhani hatuna akili? Kitu chochote kisicho na ulaji kwako kinakuwa hakina maana kwako. Kiasili mwenge ulianza wakati wa mfumo wa chama kimoja, hivyo wahudumu wake wote walitoka ccm na hadi sasa bado wanaopata ulaji kwenye mradi huo wana sura za kiccm na hapa ndiyo tatizo cdm lilipo kwa sababu wao wamekosa nafasi za ulaji kwenye huu mradi. Labda ulaji kwenye mradi huu wa mwenge ungegawanywa kwenye vyama vyote ilitutoe ajira za kisiasa zaidi kama kawaida yetu ili kupunguza hizi kelele kelele 😎
 
Na kuitetea CHADEMA inatakiwa uwe na akili ya msukule!
Kuwa Chadema lazima uwe na akili kama ya funza

Khaa!!! 😎Statement kama hizi ni ujinga kuzileta kwa maGT:disapointed: akili ya funza ikoje??? Akili msukule ikoje ? Au huwa mnaandika kwa nguvu za viroba????zibaki hukohuko kwenye ushabiki wenu wa kivyama!
 
Back
Top Bottom