Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,065
- 136,448
Miezi miwili iliyopita niliwasihi CHADEMA wabadilishe kauli mbiu yao ya ‘no reforms, no elections’ na waache kusema [hususan mwenyekiti wao mpya] watauzuia uchaguzi kufanyika endapo hakutakuwepo mabadiliko ya namna chaguzi zetu zinavyofanyika.
www.jamiiforums.com
Kusema mtauzuia uchaguzi kufanyika endapo hakutakuwepo na mabadiliko ni rahisi sana kutafsiriwa kivingine na mtu yeyote yule. Na hicho ndo kimepelekea Lisu kukamatwa na kuwekwa kizuizini.
Kutoa kauli za namna hiyo [zenye kutafsirika kwa namna mbalimbali] kunairahisishia kazi CCM na serikali yake, ya kuwabana kuwa mnachochea vurugu.
Kwenye harakati kama hizi za kisiasa, moja ya kanuni kubwa zaidi ni kutokumrahisishia kazi mpinzani wako.
Kwa kutumia mfano wa mchezo wa mpira wa miguu, usijifunge magoli wewe mwenyewe au usicheze rafu kwenye eneo la penati au kwenye eneo la mita kumi na nane.
Sasa, CCM na serikali yake huwezi kuihusisha sana na matumizi ya akili kwa namna wanavyoiendesha nchi.
Lakini, hiyo isiwe sababu ya kuirahisishia kazi yao ya unyanyasaji.
Itakuwa vyema endapo huu uongozi mpya wa CHADEMA utaliangalia kwa maanani stahilifu hili suala la mawasiliano kwa umma.
Sijui idara yao ya mawasiliano ina watu gani na wenye sifa zipi.
Ila kwa kinachoendelea mpaka sasa naweza kusema idara hiyo bado ina nafasi kubwa na pana ya uboreshwaji.
Wataalamu wa mawasiliano kwa umma tupo. Just reach out and we’ll offer our helping hand in your messaging.
Happy Easter.
CHADEMA badilisheni hiyo kauli mbiu ya "No Reforms, No Elections"
My two cents from a distance. Siyo siri kwamba naunga mkono kutokushiriki chaguzi za maigizo zinazoendeshwa na CCM. Naunga mkono harakati karibu zote za mwenyekiti mpya wa CHADEMA za kuleta mabadiliko ya kweli. Yote anayofanya ni sahihi kasoro hili la kusema kuwa watazuia uchaguzi kufanyika...
Kusema mtauzuia uchaguzi kufanyika endapo hakutakuwepo na mabadiliko ni rahisi sana kutafsiriwa kivingine na mtu yeyote yule. Na hicho ndo kimepelekea Lisu kukamatwa na kuwekwa kizuizini.
Kutoa kauli za namna hiyo [zenye kutafsirika kwa namna mbalimbali] kunairahisishia kazi CCM na serikali yake, ya kuwabana kuwa mnachochea vurugu.
Kwenye harakati kama hizi za kisiasa, moja ya kanuni kubwa zaidi ni kutokumrahisishia kazi mpinzani wako.
Kwa kutumia mfano wa mchezo wa mpira wa miguu, usijifunge magoli wewe mwenyewe au usicheze rafu kwenye eneo la penati au kwenye eneo la mita kumi na nane.
Sasa, CCM na serikali yake huwezi kuihusisha sana na matumizi ya akili kwa namna wanavyoiendesha nchi.
Lakini, hiyo isiwe sababu ya kuirahisishia kazi yao ya unyanyasaji.
Itakuwa vyema endapo huu uongozi mpya wa CHADEMA utaliangalia kwa maanani stahilifu hili suala la mawasiliano kwa umma.
Sijui idara yao ya mawasiliano ina watu gani na wenye sifa zipi.
Ila kwa kinachoendelea mpaka sasa naweza kusema idara hiyo bado ina nafasi kubwa na pana ya uboreshwaji.
Wataalamu wa mawasiliano kwa umma tupo. Just reach out and we’ll offer our helping hand in your messaging.
Happy Easter.