CHADEMA na CUF kipi mashuhuri??

CHADEMA na CUF kipi mashuhuri??

Kilichopata kura nyingi ndicho mashuhuri na kinachokua kwa kasi, kumbuka hakuna mbunge wa chadema aliyechaguliwa chini ya kura 10,000! Ila cuf ni wengi sana!
 
udikteta ni upi kati ya kula mali ya uma na tunashindwa kuongea kuogopa kuambia bomu la machozi limekupiga bahati mbaya au kutetea haki za wanyonge?

kutetea haki za wanyonge kwa kuhamasisha maandamano na kuchochea migomo ya madaktari mahospitalini ili wanyonge unaowatetea wakosa huduma bila kutueleza mipango yako na jinsi utakavyopata fedha za ku finance hiyo mipango yako ni uongo
 
Acha unafiki ndugu yangu, hivi sasa hivi unaweza kufananisha cuf na cdm kweli?, mbona chama hiki kinategemea fadhira za ccm, naomba unieleze nguvu ya cuf bara, kwani cdm haiwezi kuchukua nchi bila zanzibar?, kura za zanzibar ni majimbo 3 tu ya JJ Mnyika sasa ni zanzibar bwana?, acha propaganda zako humu Jforums, cuf imesambaratika, jana ccm wamewalipia mpaka Airtime TBCCCM, unasema cdm ni Namanga mpaka Himo, Je cuf inaanzia Pemba mpaka wapi?, naomba unijibu ww ccm b, mbona mna wabunge kutoka Pemba kuliko sehemu yoyote nipe jibu,lkn mbona mkutano weni ulijaa bagharashia je ina maanisha nini?.
 
CUF ni chama kisicho na sera kimebakia na bendera tu! Hakuna umaarufu hapo zaidi ya kufadhili UAMSHO

Na wao ukizungumza nao wanadai chadema hakuna zaidi ya kufadhili na kuchochea migomo mbali mbali,ndio mana tunataka kujua kipi mashuhuri kwa sababu vinafanana kwa mambo mengi sana
 
Ndio tumia njia hiyo hiyo, kuna tofauti kati ya umaarufu na kupendwa... Inawezekana CCM ni maarufu kuliko CDM lakn CDM ikawa inapendwa kuliko CCM..!!
Ha ha haaaa naona unajichanganya..kwa kigezo chako cha idadi ya wabunge ndio umaarufu na kupendwa kwa chama,sasa mbona hao wanaowapenda wamewapa safu nyembamba sana ya wabunge ukilinganisha na ambao hawapendwi kama chadema inavyopendwa??
 
Ni kwa nini una upeo mdogo wa kufikiri uliuliza kati ya Cuf na Cdm nimekupa jibu ushakimbilia ya CCM. Acha undumilakuwili stick to point.
ok kwa hiyo hiyo determinant ya idadi ya wabunge is applied mnaposhindanishwa na cuf tu basi kwa kuwa mnawazidi wabunge lakini kwa ccm inakua haifanyi kazi!hakuna ugonjwa mbaya duniani kama mapenzi nimeamini,ukipenda unakua kipofu
 
kwani Cuf ni chama cha siasa au taasisi ya dini? embu wanajamvi mnijuze maana niliona hijabu na balakhashia ndo zilijaa kwenye mkutano ule wa jana...

kuhusu cuf i have no idea zaidi ya kujua ni chama cha siasa ila chadema nilipata kusikia kwamba ni chagga delopment something nimesahau kidogo,je upo ukweli wa hilo??nomba wanajamvi wanaoijua chadema sawasawa wanijuze hili pia,naona limenijia wakati mzuri sana
 
Mada hii haujaitendea haki kabisa kwa sababu inajulikana kabisa kwamba CDM, ndicho chama mbadala kwa CCM, Na kinakubalika sana kwa sasa kuliko vyama vyote vya upinzani. Mambo mengi yako wazi kwa mfano unaweza kuangalia matokeo ya kura za uchaguzi wa Uraisi Mgombea wa CUF Aliachwa mbali sana na Dr Slaa wa CDM. Mbili CDM ni chama chenye Madiwani wengi Tanzania kuliko chama chochote cha Upinzani. Tatu CDM ni chama chenye wabunge wengi Tanzania kuliko chama chochote cha upinzani. Nne Cdm Ni chama kinachokubalika kwa sehemu kubwa ya Tanzania kuliko vyama vingine vya upinzani. CUF, ni chama chenye msomi mzuri sana Ndugu Prof Lipumba lakini kinakubalika sana PEMBA,LINDI,MTWARA, Na Katika baadhi ya maeneo fulani fulani.Unaweza kujiuliza Maeneo kama Kigoma ni CHADEMA NA NCCR Mageuzi.Na nafikili CUF wanahaja ya kujiuza zaidi ili waeleweke kwa jamii kubwa ya Tanzania. Hata Tabora CDM wako juu. Hata Dar Es Salaam, CDM wako juu ya CUF. Enzi za CUF kutamba zilikwisha ile miaka ya 2000, hadi 2005. Kuanzia 2010 ni CDM. CDM kwa taarifa yenu wana wabunge wengi zaidi mkoa wa Shinyanga kuliko hata Kilimanjaro. Kilimanjaro ina wabunge watatu wa CDM sawa na Mwanza. Kusema kwamba CDM inaishia Himo ni mzaa, utani,upuuzi,propaganda,ukipofu, ghiliba na ujinga uliopitiliza. Na nafikili watu wenye timamu hawawezi kusema hili, ni wale hamnazo tu. Kwa sababu vielelezo vyote vipo wazi. Na kama unabisha CDM NA CUF wapambanishwe katika majiji haya manne ya Tz kimikutano uone.

wabunge wa shinyanga umemhesabu na shibuda au?kweli baniani mbaya kiatu chake ni dawa!
 
Nataman kauchaguz ata cha ubunge kafanyike waumbuke watu .kama igunga ivi tuone nani atakuwa mbabe
kumbe lengo ni kuwa mbele ya cuf na sio kushinda ubunge!wapinzani wa bongo bwana,mnazingua sana,wananchi mjionee huu ndio aina ya upinzani tulionao ambao unakula kodi zetu bure tu kwa njia ya ruzuku
 
manake hawataki kuungana kila mmoja anajidai mkubwa na anajiweza kuliko mwenzie ndio mana nikaitisha kura ya maoni hii isiyo rasi ili tujue then tuwafahamishe,wnatakiwa kujipanga kuanzia sasa kwa ajili ya 2015
Wakiungana itakuwaje? Bwn CCM+Bi CUF best men and women, POLICCM,msajili wa vyama vya siasa,Sasa mbona wataka kumfundisha bintI ''UHUNI'' MWACHE ATULIE NA MTU WAKE CDM kama uijuavyo IMESIMAMA KI-KAMILIFU

 
kuhusu cuf i have no idea zaidi ya kujua ni chama cha siasa ila chadema nilipata kusikia kwamba ni chagga delopment something nimesahau kidogo,je upo ukweli wa hilo??nomba wanajamvi wanaoijua chadema sawasawa wanijuze hili pia,naona limenijia wakati mzuri sana

I thought you can argue .... from now I declare this post to be a foolish hoax
 
Wewe endelea na kutafuta CHAMA MASHUHURI wakati wajanja wanatafuta CHAMA KINACHOWAWEZESHA WANANCHI.
 
Ha ha haaaa naona unajichanganya..kwa kigezo chako cha idadi ya wabunge ndio umaarufu na kupendwa kwa chama,sasa mbona hao wanaowapenda wamewapa safu nyembamba sana ya wabunge ukilinganisha na ambao hawapendwi kama chadema inavyopendwa??

KK hivi umehesabiwa ktk sensa iliyomalizika juzi?
 
KK hivi umehesabiwa ktk sensa iliyomalizika juzi?
Ndio kaka nimehesabiwa,waislam ndio wakorofi wanapingana na serikali kwenye hili la sensa bila ya kuwa na hoja za msingi..lengo ni kuifanya serikali ishindwe kufanya kazi zake kitu ambacho hakikubaliki kwa serikali haina dini
 
mzazi shule inatakiwa hapa? nani kataja kuwa mbele ya cuf,ishu ni uchaguzi tuone mshindi nani kama cuf atafuatia no problem but cha muhimu ushindi wa ubunge kwa chadema acha kufikiri kwa makalio
 
UKISIKIA upuuzi wa kupotezea watu muda, basi upuuzi wenyewe ndo huu: MASHUHURI! Ungesema kati ya CDM & CUF kipi chenye sera nzuri za kukomboa mwananchi, ningekuelewa. LAKINI hicho ulichosema ni upuuzi tu ...
 
Back
Top Bottom