Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 4,367
- 2,407
- Thread starter
-
- #21
Unashindwa kuleta hoja za msingi unaleta huo upuuzi wako hapa eti cdm ni ya kikristo mtabaki kubwabwaja mapropaganga yasiyo na msingi badala ya kuleta mambo ya maendeleo kuna mambo ya kujadili na siyo huo ***** wako hapa mabilioni ya uswis ufisadi wa kutisha tanesco yote hayo huyaoni mpaka ulete umbea hapa?mwambie aliyekutuma akupe mshahara mana ndo kazi yenu nynyiemu kuleta masuala ya kijinga then mnabaki kumbwelambwela shame on you magamba
Ndio nia kuu kupeleka malalamiko kwa Tendwa. Lakini kabla sijafanya hivyo nahitaji umma uelewe kwanini napeleka malalamiko yangu kwa msajili wa vyama.
Nafikiri si makosa kuwajulisha wanachama wa CHADEMA na Watanzania wote kwa nini ninaamini kuwa hiki ni chama cha kidini. Nimechoshwa na wanasiasa kulalamika majukwaani tu kuwa CDM ina udini. Napenda kwenda mbali zaidi ya hapo.
Si siri kuwa CHADEMA inauhusiano wa karibu au ni mwanachama wa Christian Democratic Parties duniani. Kuhudhuria kwa mwenyekiti wa BAVICHA katika mkutano wa CDU kule Ujerumani ni moja ya uthibitisho wa ukaribu huo. Lakini si kuhudhuria tu bali hata wanachama wa CHADEMA wakati huo waliandika hapa JF kuthibitisha ushirikiano na uhusiano wa CHADEMA na Christian Democratic Union cha Ujerumani. Wanachama hawakutueleza kinaga ubaga hasa ni nini idiolojia ya Christian Democratic Parties. Niliahidi kuandika mada kuhusu hili, na
hii ni sehemu ya kwanza katika mfululizo wa sehemu 4.
Christian Democratic Parties DunianiChristian Democracy ni idiolojia ya kisiasa yenye lengo la kutumia misingi ya Kikristo katika tawala za jamii. Muundo huu ulizaliwa katika karne ya 19 huko Ulaya kwa ushawishi wa mafundisho ya Kikatoliki ya kijamaa pamoja na wale wenye mlengo wa kulia (Conservatism).
Kifupi, Christian democracy imekuwa na siasa kali zaidi katika maswala ya Tamaduni, jamii na moral issues pia inazingatia social markets economy katika upande wa uchumi.
Tukimnukuu Geoffrey K Robert na Patricia Hogwood wameandika " Christian Democracy has incorporated many of the views held by Liberals, conservatives and socialists within the wider framework of moral and Christian Principles". Aidha baadhi wanaenda mbali zaidi pale wanapoandika kuwa Vyama hivi vinaamini kuwa Serikali inaunda Mamlaka yake toka kwa Mungu na sio toka kwa watu.
Nguvu ya vyama vya kidemokrasia vya Kikristo Ulaya
Mtazamo wa kisiasa wa vyama vya Kidemokrasia vya Kikristo umetofautiana katika makali yake (conservatism) kutoka nchi moja hadi nyingine kutokana na umaarufu au uzito wa kanisa katika nchi husika.Kwa mfano vile vya Ulaya vina siasa za kati (moderate conservative), lakini nchi za Ujerumani, Uhispania na Belgium vyama hivi vina nguvu sana na ni conservative zaidi.Katika kipindi cha hivi karibuni (2000-2012) Vyama vingi vya kidemokrasia vya kikristo vimesota sana katika chaguzi kuu. Vingi vikiishia kupata 4-9% katika chaguzi kuu, vingine vikiishia kupata chini ya 3% na kushindwa kuingia Bungeni. Nchi ambazo vyama hivi vina nguvu na kushika madaraka katika miaka ya hivi karibuni ni Ujerumani (Christian Democratic Union- Bi Angela Merkel, kabla yake, Konrad Adenauer, Helmut Kohl), Italia- (Giulio Andreotti-PM, Giorgio La Pira, Aldo Moro-PM, Adone Zoli-PM.), Uhispania (Mariano Rajoy-PM).
Nafasi ya CHADEMA
Maswali mengi, watanzania tunapaswa kujiuliza, hivi CHADEMA inapokwwenda katika mikutano kama hiyo inakuwa na ajenda gani na inajifunza nini? Je ni idiolojia ya principles za kikristo ndio tuzitarajie itapochukua madaraka? Hivi ni makosa kukiita chama hicho kuwa ni cha kidini.
Waswahili wanasema niambie rafiki zako ni akina nani, nitakueleza wewe ni nani? Marafiki wa CHADEMA ndio hao nafikiri si vigumu kwa watanzania kukielezea kinaga ubaga kuwa hiki ni chama cha aina gani.
Sehemu ya pili itaelezea Historia ya chimbuko la vyama vya Kikristo.
Kimsingi, PROPAGANDA za kutumia UDINI kama njia ya kudhoofisha CHADEMA, zilisha prove failure,
Kuhusu suala la CHADEMA kuwa na uhusiano na chama cha kikristu cha Ujerumani, nakuja kutoa maelezo,
Kimsingi, PROPAGANDA za kutumia UDINI kama njia ya kudhoofisha CHADEMA, zilisha prove failure,
Kuhusu suala la CHADEMA kuwa na uhusiano na chama cha kikristu cha Ujerumani, nakuja kutoa maelezo,
Jakaya kikwete.....Mwislam
Philipo mangula....MKRISTO
Abdulahiman kinana.Mwislam
Mwigulu nchemba....Mwislam
Asha Rose migiro...Mwislam
Nape Mnauye........Mwislam
Do Mimi napita tu.
Rais ni Mwislam, Makamu wa rais ni Mwislam, Mkurugenzi mkuu wa TISS ni Mwislam, IGP ni Mwislam, Jaji mkuu ni Mwislam, Jaji kiongozi ni Mwislam, etc. Tukisema Alhaj Kikwete anaiongoza nchi Kiislam tutakuwa tunakosea??!!Una hakika kuwa Asha Migiro ni mwislam.
Hata hivyo point haikuwa mtu au watu bali muelekeo wa Chama. Walipoalikwa Ujerumani na Christian Democratic Union Party cha Bi Anggela Merkel walitamba sana. Nilwauliza hivi ni nini mnachofaidika au kujifunza toka kwa chama hicho? Mjibuji wa swali langu alijitahidi kujibu lakini alificha ukweli katika baadhi ya mambo muhimu sana, hasa kuhusu uhusiano wa kanisa na chama hicho. Ndipo nikaahidi kuja na mada itayohusu vyama vya kikristo duniani.
Ninachotarajia kwa wajibuji wa thread hii, ni kutetea idiolojia ya chama chao hasa wakizingatia kutoshawishika na idiolojia za wakubwa hao 'CDU'. Hii ni muhimu sana kwani tumeona vyama vingi viingiapo madarakani, vikiyumbishwa na malobies. Na kwa maana hiyo nilikichukua hicho chama cha Ujerumani 'CDU' au wanachama wake matajiri kuwezekana kuwa wachangiaji wakubwa wa pesa kwa CDM kwa intrest zao. Sasa hizi Intrest za nchi Magharibi ndizo zinazotuharibia nchi zetu, kama ilivyokuwa katika mauaji ya genocide ya Rwanda na uhusikaji wa kanisa.
Kuna wanaosema kwanini unakifuatafuata CHADEMA? Wanakosea sana, kwani wakichukua nchi nami nitaathirika kwanini nsijiulize leo kama hicho chama kinastahili. Tafadhali jibuni hoja!!!!!
Ungekuwa na legal grounds na ushahidi, na ungekuwa unauamini ushahidi huo wala usingepitia hapa ungeenda moja kwa moja kwa msajili. Nakushauri kwa moyo mmoja nenda na peleka ushahidi wako.Ndio nia kuu kupeleka malalamiko kwa Tendwa. Lakini kabla sijafanya hivyo nahitaji umma uelewe kwanini napeleka malalamiko yangu kwa msajili wa vyama.
Nafikiri si makosa kuwajulisha wanachama wa CHADEMA na Watanzania wote kwa nini ninaamini kuwa hiki ni chama cha kidini. Nimechoshwa na wanasiasa kulalamika majukwaani tu kuwa CDM ina udini. Napenda kwenda mbali zaidi ya hapo.
Christian ideology ndiyo inayoongoza dunia sasa, ndiyo maana kuna anguko la uislam. Nadhani CDM wapo sahihi kuwa nao.