Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,280
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na ACT-Wazalendo, vimejitoa katika uchaguzi wa udiwani kata ya Igumbilo, Manispaa ya Iringa uliopangwa kufanyika Desemba 8, mwaka huu.
Kata hiyo haikufanya uchaguzi katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Oktoba 28, baada ya kifo cha mgombea wa CCM kutokea Oktoba 16, hivyo kusababisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuuahirisha.
Kutokana na kujitoa huko, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Iringa Mjini, Hamid Njovu, jana alimtangaza Boniface Kilave kuwa mshindi wa udiwani wa kata hiyo baada ya kupita bila kupingwa.
Novemba 13, NEC kupitia Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi, Gerald Mwanilwa, alitangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo kwenye kata tatu ikiwamo hiyo.
Kata nyingine ni Nyahanga iliyoko Halmashauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga na Kibosho Kati, kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, mkoa ni Kilimanjaro.
Katika kata hiyo ya Igumbilo, wagombea ambao ni Wilbert Kilave (CHADEMA) na Mahamad Rassa (ACT- Wazalendo), walitangaza kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho.
Njovu alisema wagombea hao waliwasilisha barua zao za kujitoa kugombea zikiambatanishwa na viapo vyao vya tamko la kujitoa vilivyotolewa mbele ya hakimu juzi.
Alisema barua hizo za kujiondoa zilizingatia kifungu cha 50 cha sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa, sura ya 292 ya mwaka 2015 na kanuni zake.
Alisema diwani mteule atapatiwa hati ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo ifikapo Desemba 8, ambayo ni siku iliyopangwa kufanyika uchaguzi huo.
IPPMedia
Kata hiyo haikufanya uchaguzi katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Oktoba 28, baada ya kifo cha mgombea wa CCM kutokea Oktoba 16, hivyo kusababisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuuahirisha.
Kutokana na kujitoa huko, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Iringa Mjini, Hamid Njovu, jana alimtangaza Boniface Kilave kuwa mshindi wa udiwani wa kata hiyo baada ya kupita bila kupingwa.
Novemba 13, NEC kupitia Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi, Gerald Mwanilwa, alitangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo kwenye kata tatu ikiwamo hiyo.
Kata nyingine ni Nyahanga iliyoko Halmashauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga na Kibosho Kati, kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, mkoa ni Kilimanjaro.
Katika kata hiyo ya Igumbilo, wagombea ambao ni Wilbert Kilave (CHADEMA) na Mahamad Rassa (ACT- Wazalendo), walitangaza kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho.
Njovu alisema wagombea hao waliwasilisha barua zao za kujitoa kugombea zikiambatanishwa na viapo vyao vya tamko la kujitoa vilivyotolewa mbele ya hakimu juzi.
Alisema barua hizo za kujiondoa zilizingatia kifungu cha 50 cha sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa, sura ya 292 ya mwaka 2015 na kanuni zake.
Alisema diwani mteule atapatiwa hati ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo ifikapo Desemba 8, ambayo ni siku iliyopangwa kufanyika uchaguzi huo.
IPPMedia