CHADEMA na ACT Wazalendo fungueni kesi kupinga 15% kukatwa kwenye mishahara ya wafanyakazi wenye Mikopo HESLB

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Binafsi nashangazwa sana na ukimya wa watanzania kuhusu haya makato ambayo kwakweli ni makubwa mno kulinganisha na vipato halisi vya watanzania walio wengi.

Waajiriwa wengi wa nchi hii hasa watumishi wa umma wana mishahara midogo sana huku wakikabiliwa na msururu wa makato ya kisheria katika mishahara yao kuanzia PAYE, BIMA, makato kwa ajili ya mifuko ya hifadhi ya jamii,n.k.

Inasikitisha sana katika mlolongo huu mfanyakazi anaongezewa makato mengine ya kisheria ya asilimia 15 ya basic salary yake huku wengine teyari wakiwa na mikopo ya mabenki.

Kuna taasisi iliahidi kwenda mahakamani kupinga makato haya lakini mpaka sasa hatusiki chochote kinachoendelea huku watu wakiendelea kuumia na makato haya makubwa.

Mimi nawashsuri CHADEMA, ACT,na vyama vingine pamoja na wadau wengine kwenda mahakamani kupinga makato hayo iwapo kisheria inawezakana au kutoa mawakili kwa gharama za vyama kusimamia kesi hizi iwapo vyama vya siasa havina haki hiyo kisheria.

Japo Bodi inaruhusiwa kuongeza makato wakati wowote sidhani kama kisheria ni sahihi mabadiliko hayo kuathiri wale waliongia mkataba na Bodi kabla ya sheria kufanyiwa mabadilko.

Vile vile sidhani kama ni sahihi kubadili sheria bila kuhusisha wadau na kama sheria inairuhusu Bodi kubadili kiwango cha makato bila kushirikisha wanufaikaji na wadau wengine,basi sheria hii itakuwa ni sheria mbaya na inastahili kupingwa mahakani.

Mapungufu mengine ya wazi ya sheria hii

Grace period ya mwaka mmoja


Pia sheria hii inatoa grace period ya mwaka mmoja kwa mnufaika tangu amalize chuo na baada ya kipindi hicho kuisha, mnufaika huyu anatakiwa kuanza kulipa deni lake.

Lakini sheria hii haitambui ukweli kuwa kwa watumishi wa umma inaweza kuwachukua hata miaka miwili tangu wawasilishe vyeti kwa waajiri wao ndio wabadilishiwe mishahara yao(wapandishwe vyeo).

Sasa kumkata hiyo asilimia mtu mwenye mshahara wa Diploma kama ya ualimu sijui unategemea mtumishishi aishije na aweze kuleta tija mahala pake pa kazi..

Mimi nashauri grace period iwe ni angalau miaka miwili ilo hata makato yakianza basi mtumishi huyu awe na ahueni japo kidogo.

Utaratibu wa kuzingatia moja ya tatu ya mshahara.

Ni serikali yenyewe ndio iliweka utaratibu huu ili kumlinda mfanya kazi wake kuhakikisha anabaki na moja ya tatu ya mshahara wake baada ya makayo yote ya kisheria na yasiyo ya kisheriai lakini sina uhakika kama Bodi huu utaratibu unawahusu au laa .

Nachoshauri hapa ni kuwa,kama kweli huu utaratibu wa moja ya tatu Bodi hauwahusu au hawauzingati kama nilivyowa sikia(wenye uhakika watusaidie), basi ni wakati wa Bodi nao kuzingatia utaratibu huu ambao nao sijui kama uko kisheria au ni utaratibu tu usio na nguvu ya kisheria(sina uhakika kuhusu hili).


Wapinzani kama watu mnaotaka kushika madaraka ya nchi, nawashauri haya ndio mambo ya kupigania wananchi sambamba na mambo mengine kwani yanagusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Na hata muswaada wa kuunganisha mufiko ya hifadhi ya jamii nao kama utapitishwa kama ulivyo ni vizuri nao muupinge mahamani kama utathiri utoaji wa mafao na haki zingine za wanachama ambao walijunga na mifuko hii kabla ya mabadiliko yanayotarajiwa hayajafanywa.


Tatizo kubwa la sisi watanzania ni kuwa na reaction ya muda tu na baada ya hapo tunasahau wakati nchi za wenzetu hata bei tu ya mkate ikipanda ni maandamano nchi nzima.

Nachojiuliza hivi kesho na kesho kutwa wakiamua kuongeza asilimia na kufikia asilimia 20 tutakuwa na haki ya kulalamika au kuhoji kama leo hii hatujachukua hatua yoyote?

Binafsi niliwahi pendekeza vyanzo hivi vya mapato kwa Bodi hii ya Mikopo kupitia huu uzi hapa chini.

Hivi vinaweza kuwa vyanzo mahususi vya mapato kwa ajili ya Bodi ya Mikopo
 
Hii ni hoja ya kipinzani na ndio hoja zinazotakiwa kuuliziwa sio kelele zisizo na msingi.

Najiuliza wakati sheria inapitishwa wabunge wa Chadema kwa nini hawakutoka nje?
 
ukishaingiza siasa hamna litakalofanyika, kwanini usiombe mawakiki wasomi ambao pia ni wadaiwa wafanye hilo?
 
Hii ni hoja ya kipinzani na ndio hoja zinazotakiwa kuuliziwa sio kelele zisizo na msingi.

Najiuliza wakati sheria inapitishwa wabunge wa Chadema kwa nini hawakutoka nje?
You are a typical type of persons who were praising Idd Amin despite killing more than 500,000 or so fellow Ugandans! Hivi mmeshafikisha wangapi? ,,,100,000 or more!
 
Chadema Wana matatizo binafsi zaidi ya hayo ya mikopo,ruzuku ya kutosha nk shida za wananchi siyo kipaumbele.
 
Asanteni mods/Melo kwa kuona busara ya kurudisha huu uzi.

Haya makato jamani ni mateso na mzigo mkubwa na hapa JF ndio pa kusemea maana hakuna mahali pengine.
 
Wote mlio pata mikopo mlipe ili wengine wasome pia. Huu ulalamishi ni ubinafsi wa kishenzi
Hii Bodi inatakiwa itafutiwe vyanzo mahususi vya mapato kama ilivyo kwa mradi wa umeme vijijini na EWURA ambao wanapata mapato ya kujiendeshao kupitia tozo maalumu kwenyee manunuzi ya umeme na mafuta.

Itafika mahali hata hiyo asilimia 15 mnayokata sasa mtaona haitoshi mtataka kukata hata asilimia 30.

Wanufaika wa hii Bodi hawawezi kubeba mzigo wa kusomesha watanzania wenzao wanaoongezeka kila kukicha bali wanasaidia tu kubeba kiasi cha ghrama lakini sehemu kubwa inabidi itokane na vyanzo mahususi kwa ajili ya hii Bodi.

Niliwahi shauri hivi vinaweza kuwa ni vyanzo mahususi vya mapato kwa hii Bodi.

Soma kupitia hii link hapa chini.

Hivi vinaweza kuwa vyanzo mahususi vya mapato kwa ajili ya Bodi ya Mikopo
 
Hii ni hoja ya kipinzani na ndio hoja zinazotakiwa kuuliziwa sio kelele zisizo na msingi.

Najiuliza wakati sheria inapitishwa wabunge wa Chadema kwa nini hawakutoka nje?
Kinachonikera nchi hii ni watu kuishi kwa mihemko alafu jambo likpita linakuwa kawaida na si issue tena.

Tunatumia muda mwingi kupigana vijembe na tunatumia muda mchache sana kujadili suluhu ya matatizo yote.

Hili limeshapita na sasa si habari tena tunasubiri la kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii tupige makelele alafu turidhike na kusahau.

Tumekosa mikakati ya kutotua hapa tulipo na tutaendelea kuwa nchi ya watu masikini tu.
 
Hii nchi ina ushithole mwingi sana... Yani mtu analipwa mshahara laki tano. Anakwatwa bodi asilimia 15,paye 10, nssf, sijui nhif, narudi nyumbani na laki mbili na nusu. Afu vyama vya wafanyakazi, na wabunge ambao ndo wanapaswa kuwa sauti ya wananchi wamekaa kimya tuu kwenye kiyoyozi. Aliyetulaani ngozi nyeusi.......!!!
 
Hii Bodi inatakiwa itafutiwe vyanzo mahususi vya mapato kama ilivyo kwa mradi wa umeme vijijini na EWURA ambao wanapata mapato ya kujiendeshao kupitia tozo maalumu kwenyee manunuzi ya umeme na mafuta.

Itafika mahali hata hiyo asilimia 15 mnayokata sasa mtaona haitoshi mtataka kukata hata asilimia 30.

Wanufaika wa hii Bodi hawawezi kubeba mzigo wa kusomesha watanzania wenzao wanaoongezeka kila kukicha bali wanasaidia tu kubeba kiasi cha ghrama lakini sehemu kubwa inabidi itokane na vyanzo mahususi kwa ajili ya hii Bodi.

Niliwahi shauri hivi vinaweza kuwa ni vyanzo mahususi vya mapato kwa hii Bodi.

Soma kupitia hii link hapa chini.

Hivi vinaweza kuwa vyanzo mahususi vya mapato kwa ajili ya Bodi ya Mikopo
Hamuwasaidii bodi mkuu wala kutoa fadhila bali ni kulipa MKOPO mlio chukua.
 
Wanaoleta hizi sera wao sio ndio walisoma bure kabisa.

Nyerere angekuwa kama wao baadhi ya wangesoma na kuwa hapo walipo leo hii?
Mambo yabadilika na Sera zinabadilika. Kuanza kutamani kuishi kama miaka 50 iliyo pita ni kujidanganya wenyewe. Hizi fedha zikitolewa kama MKOPO halafu watu kuilipa wanaona shida.
 
Mambo yabadilika na Sera zinabadilika. Kuanza kutamani kuishi kama miaka 50 iliyo pita ni kujidanganya wenyewe. Hizi fedha zikitolewa kama MKOPO halafu watu kuilipa wanaona shida.
Hizo hela mlizoenda kujengea uwanja wa ndege huko Chato zingesomesha wanafunzi wangapi?

Hizi hela za uchaguzi wa marudio zingesomesha wanafunzi wangapi?

Tatizo lenu ni kukosa ubunifu,kuwa na sera mbovu na kushindwa kuwa na vipaumbele vya maana.

Mmebaki kupiga makelele tu.
 
Hizo hela mlizoenda kujengea uwanja wa ndege huko Chato zingesomesha wanafunzi wangapi?

Hizi hela za uchaguzi wa marudio zingesomesha wanafunzi wangapi?

Tatizo lenu ni kukosa ubunifu,kuwa na sera mbovu na kushindwa kuwa na vipaumbele vya maana.

Mmebaki kupiga makelele tu.
Tulizo enda kujengea Chato, Mimi na akina nani? Tatizo lako kila kitu unafikiria kwa mtazamo wa CCM na CHADEMA. Sijawahi kukubaliana kimsingi na utawala wa Magu kwa mfano, ila ukweli mchungu ni kwamba watanzania na waafrika tunapenda kukimbia wajibu. Yaani watoto uzae wewe halafu utegemee serikali ikusomeshee, ebo!!! Kimsingi, mzazi anawajibika kusomesha na kukuza wanawe, serikali sio baba au mama yako.
 
Back
Top Bottom