zema21
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 619
- 251
Kwa sasa hivi nchi inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu wanaohitimu mafunzo yao mbalimbali, hakuna juhudi za dhati zinazochukuliwa kukabiliana na tatizo hilo; kama kawaida yetu ya kulalamika kila mmoja analalamika; lakini hakuna hatua za dhata kunusuru tatizo hilo!!
Ufisadi unaongezeka kila kukicha ukiacha matukio yaliyoripotiwa miaka iliyopita hv sasa kuna utoroshaji wa fedha kwenda nchi za nje!
Kama kawaida yetu linafanyiwa kazi na vyombo husika, watanzania tumebaki kulalamika huku tukiwa na hali ngumu za maisha, kiasi cha baadhi kukosa hata mlo mmoja wa siku!
Vijana na hawajui future yao, wengi wao ukiwauliza mipango yao katika miaka miwili ijayo hawajui wakujibu nini!
Wanaambiwa wakajiajiri huku wakiwa hawana mitaji, vifaa, wala hata elimu ya ujasiria mali bila kusahau ukosefu wa masoko! Watajiajiri vp! Jaribu kufuatilia watoto wa hao wanaowambia vijana wetu wakajiajiri uone kama wamejiajiri wao! Rasilimali za wananchi zinaliwa na wachache!
Ebu nyie mnaojiita nguvu ya umma tuambieni mtatatua vp haya mattizo yetu?
Manake siasa zimetuchosha! Hamna lolote tunalosaidika badala ya kuwa walalamishi tuuu! Pia tuzingatie kuwa na nyie mna matumbo kama hawa wengine waliopo sasa pia mna njaa kama wao! Nini kitawafanya msile kama hawa jamaa ile hali mna sifa zinazofanana za njaa na matumbo pia?
Naomba kuwasilisha
Ufisadi unaongezeka kila kukicha ukiacha matukio yaliyoripotiwa miaka iliyopita hv sasa kuna utoroshaji wa fedha kwenda nchi za nje!
Kama kawaida yetu linafanyiwa kazi na vyombo husika, watanzania tumebaki kulalamika huku tukiwa na hali ngumu za maisha, kiasi cha baadhi kukosa hata mlo mmoja wa siku!
Vijana na hawajui future yao, wengi wao ukiwauliza mipango yao katika miaka miwili ijayo hawajui wakujibu nini!
Wanaambiwa wakajiajiri huku wakiwa hawana mitaji, vifaa, wala hata elimu ya ujasiria mali bila kusahau ukosefu wa masoko! Watajiajiri vp! Jaribu kufuatilia watoto wa hao wanaowambia vijana wetu wakajiajiri uone kama wamejiajiri wao! Rasilimali za wananchi zinaliwa na wachache!
Ebu nyie mnaojiita nguvu ya umma tuambieni mtatatua vp haya mattizo yetu?
Manake siasa zimetuchosha! Hamna lolote tunalosaidika badala ya kuwa walalamishi tuuu! Pia tuzingatie kuwa na nyie mna matumbo kama hawa wengine waliopo sasa pia mna njaa kama wao! Nini kitawafanya msile kama hawa jamaa ile hali mna sifa zinazofanana za njaa na matumbo pia?
Naomba kuwasilisha