Dola sio kichwa cha mwendawazimu. Huwezi kuwapa watu wafanyie majaribio.
Kamwe nchi haiwezi kuachwa kwenye mikono ya majangiri majambawazi,wadhalimu hawa miaka 54 inawatosha
Dola sio kichwa cha mwendawazimu. Huwezi kuwapa watu wafanyie majaribio.
In theory ambayo wengi wanaiamini ni wapiga kura.
In reality inategemeana na hali ya nchi.
Chadema hawana sifa za kuongoza dola huo ndiyo ukweli.
Kumnyang'anya CCM TONGE mdomoni si kazi rahisi yuko tayari kupigana ili asipokonywe TONGE au ulaji. CHADEMA inahitaji maarifa zaidi ili iweze fanikiwa katika hili. Nahisi harufu ya damu 2015.
Dola sio kichwa cha mwendawazimu. Huwezi kuwapa watu wafanyie majaribio.
Ni kuongeza nguvu za M4C tu, na kuwaelimisha wapigakura kutoogopa mabomu ya machozi hata ya moto, na badala yake walinde kura zao na kuhakikisha zinasomwa kama zilivyo
Mkuu Kigarama, nimekusoma na nimekuelewa.Ikifika mwaka 2015 itakuwa ni miaka 20 kamili imepita tangu kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza ulioshirikisha vyama vingi mwaka 1995 tangu kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi uliokuwa umepigwa marufuku miaka 30 kabla, yaani mwaka 1965. Kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 inaonekana mchuano utakuwa kati ya CHADEMA na CCM.
Kwenye mazoezi na mechi za utangulizi (Chaguzi ndogo) CCM inaonekana kuzidiwa kwa kupunguziwa viti ilivyokuwa inavishikilia kuanzia ngazi ya vitongoji hadi kwenye ubunge na CHADEMA ikiongeza idadi ya viti vyake sehemu mbalimbali za nchi.
Lakini kwenye uchaguzi wa mwakani ni uchaguzi ambao hautatoa nafasi kwa chama chochote kile kutumia viongozi wa kitaifa au maarufu kufanya kampeni nchi nzima. Uchaguzi wa serikali za mitaa kampeni zake hufanyika kwa siku saba tu. Na chaguzi hizo kwa uzowefu hukabiliwa na dosari nyingi (irregularities) sana na rafu (Rigging) za kutisha. Na ili kukabiliana na dosari na Rafu hizo CHADEMA inatakiwa kuwa na mtandao mpana wa chama ulio Imara.
Toka leo hadi uchaguzi wa mwakani inahitaji juhudi za ziada kujenga mtandao Imara wa chama. Na ujenzi wa mtandao huo huitaji sana fedha ambazo naamini CHADEMA hawanazo. Ule mpango wa kuichangia CHADEMA kwa njia ya simu sijui umeishia wapi? Ilitakiwa kila mwezi angalau wananchi wengejulishwa ni kiasi gani kimekusanywa ili kujenga hamasa na kufanya wanachama wenyewe wajitathimini ni kwa kiasi gani wanachangia chama chao. Bila fedha (Halali lakini) hakuna siasa endelevu kwa vyovyote vile.
CHADEMA inahitaji zaidi ya watu lakini moja kuwa wagombea kwa upande wake kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na maelfu mengine kwa ajili ya mawakala. Nguvu kazi hiyo na wagombea hao ni lazima wawe wametayarishwa tangu mwaka huu na wala si mwakani wakati wa uchaguzi.
Kuna kazi ya msingi ya kufanya kabla ya uchaguzi wa mwakani kama ndiyo msingi wa ushindi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA Msituangushe.
ni kweli mkuu, hakuna mtawala yoyote duniani aliyewahi kuachia madaraka na kumkabidhi mpinzani kirahisi na kama huyu basi ni kwa shinikizo; CDM lazima watumie mbinu za kisasa kuidhibiti CCM.Kumnyang'anya CCM TONGE mdomoni si kazi rahisi yuko tayari kupigana ili asipokonywe TONGE au ulaji. CHADEMA inahitaji maarifa zaidi ili iweze fanikiwa katika hili. Nahisi harufu ya damu 2015.
Mzee sauti yako inasikika kwamba mbali sana kama ya Pasco. Unaweza kuongeza sauti kidogo??Miye yangu macho tu; lakini nani atalaumiwa kama wote tumeweka mayai yetu kwenye kikapu kimoja ambacho hakiachi kutikiswa, kurushwa rushwa na kugongwa gongwa? Do we need another credible alternative opposition? Tunaweza kujifunza chochote toka kikapu cha Raila?
Mfano mjarabu kabisa kwa hali iliyopo!! Lakini wanaona?Mwanamke anayependwa na anajua anapendwa na kila mtu huringa; anajua kuwa bado anapendwa. Mwanamke wa namna hiyo na mwenye uzuri wake wa asili haitaji mapambo mengi kuvutia suitors; ana uhakika watakuja tu. Kama siyo mwenye hekima basi anaweza kutegemea uzuri wake kama mtaji wake wa pekee. Lakini atakapoanza kukongoroka na uzee ukaanza kujionesha ataanza kuona kuwa wadau wanapungua kwa kasi. Wakati huo ataanza kujitahidi kuukumbushia uzuri wake kwa mapambo, manukato na hata kujiachilia kirahisi. Hata hivyo, wale wale waliokuwa wanampenda zamani wanaweza kujikuta wamepata kigori mwingine. Hili pia laweza kusemwa kwa wanaume kwa namna yake.
CDM ni kama mwanamke anayependwa na anajua kuwa anapendwa...
Mkuu Kigarama, nimekusoma na nimekuelewa.
Kuhusu uwezekano wa Chadema kuchukua nchi, 2015, mimi binafsi nimeisha zungumza sana, baadhi ya ma great thinkers wetu humu, kina Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mchambuzi, Mag3 na wengine, pia wamesema sana!, I doubt kama Chadema wanamacho ya kuona, na masikio ya kusikia!.
Kwa vile wengi wetu humu ni watu wa "hopes" tuu (hope for the best) wana too great expectations kuwa Chadema "lazima" itachukua nchi 2015, hivyo ikitokea Chadema ikashindwa kuchukua nchi 2015, wataishia kwenye despair!, hivyo wengine wetu mimi nikiwemo sio watu wa just hopes bali ni ma "realist" kuhusu kuchukua nchi 2015!, Ikulu haitolewi kama "mana", it got to be earned!. Ili kuipata, lazima uonyeshe utayari wa kuingia ili wananchi wenye uamuzi wa mwisho, wakuaminie, wakukabidhi nchi yao!.
Sasa to be honest, hili la utayari kwa Chadema kuchukua nchi 2015, mimi bado sijaliana, ila naamini bado wanaendelea kujipanga!. Katika muda huu wanapojipanga, as a realist, nawaandaa watu wao kisaikolojia, "not only to hope for the best, but also to get prepared for the worst!, kuwa 2015, ni CCM Tena!. This is the very bitter pill they'll have to swallow kwa kutokujipanga kwao!.
Ukipata nafasi, unaweza kupitia nyuzi zangu hizi, kuona nilianza kulisemea hili lini, tulishauri Chadema ifanye nini, na kulinganisha ya kwa sasa Chadema inafanya nini, hivyo unaelewa 2015 kitatokea nini!.
Pasco.
Fanya Rejea on
Mkuu Mboko, kila kitu kimesemwa humuKama kweli tuna mapenzi na Nchi yetu ni kwa nini msitupe atleast,Chadema wajipange kivipi au wewe serious kivipi kama umeleta issue kama hii na umepoteza muda wako kuandika naona itakuwa vyema ukaweka nini Chadema wafanye na vipi wakabiliane na mapambano haya ya kuingia ikulu kama ulivyosema kwama ikulu haitolewi kama (Mana) tupe angalau hint na kumbuka kama ukitoa mchango wako wa ukweli tutakukumbuka maika ijayo kuwa oooh Pasco,Mzee mwanakijiji,Ritz walisema haya yatokeayo now kwa upande wangu mie namkubali Mchambuzi kwa jinsi anavyochambuua mambo yenye akili huyu jamaa hakunaga sio kama hao niliowataja maake wao hawaeleweki wako wa nchi gani!!Mchambuzi hayuko kichama japokuuwa ni mwanachama wa chama flani kama sikosei lakini yeye anasimamie ukweli na uwazi hakika ni Mpenda maendeleo anaweza kuwa kiongozi na sio mtawala.
Mkuu Kigarama, japo bandiko hili ni la zamani, lakini lina hoja za msingi sana kwa muktadha wa kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2020. Kama serikali za mitaa bila Chadema, what are the chances ya uchaguzi Mkuu wa 2020.CHADEMA inahitaji zaidi ya watu lakini moja kuwa wagombea kwa upande wake kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na maelfu mengine kwa ajili ya mawakala. Nguvu kazi hiyo na wagombea hao ni lazima wawe wametayarishwa tangu mwaka huu na wala si mwakani wakati wa uchaguzi.
Kuna kazi ya msingi ya kufanya kabla ya uchaguzi wa mwakani kama ndiyo msingi wa ushindi kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA Msituangushe.
Huu ndio ukweli wenyewe. Hebu tuchangie bila povu wajameni.