CHADEMA Mkituangusha hatutawasamehe

CHADEMA Mkituangusha hatutawasamehe

Mtu huwezi kuwa 100% perfect, mpaka hapa CHADEMA kilipofikia kinahitaji PONGEZI za dhati kabisa, kwani kimepitia kwenye dhoruba nyingi sana mpaka kufikia hapo kilipo, lakini kama kuna mapungufu ambayo unayaona tafadhali usisite, toa ripoti mahala husika ili hatua zaidi zichukuliwe. Ahsante.
 
Chadema hawana sifa za kuongoza dola huo ndiyo ukweli.

Samahani RITZ kwani kuongoza dola kuna shule maalum ambayo viongozi wa CHADEMA wanatakiwa waende kama walivyokwenda viongozi wa CCM?
 
Miye yangu macho tu; lakini nani atalaumiwa kama wote tumeweka mayai yetu kwenye kikapu kimoja ambacho hakiachi kutikiswa, kurushwa rushwa na kugongwa gongwa? Do we need another credible alternative opposition? Tunaweza kujifunza chochote toka kikapu cha Raila?
 
Chadema amuwezi kushinda urais na wabunge 24.
 
Dola sio kichwa cha mwendawazimu. Huwezi kuwapa watu wafanyie majaribio.
 
Samahani RITZ kwani kuongoza dola kuna shule maalum ambayo viongozi wa CHADEMA wanatakiwa waende kama walivyokwenda viongozi wa CCM?

Kuongoza dola mpaka upate ridhaa ya wananchi na ukubalike Tanzania nzima siyo ukanda mmoja na tabaka moja.
 
Kuongoza dola mpaka upate ridhaa ya wananchi na ukubalike Tanzania nzima siyo ukanda mmoja na tabaka moja.

Kwahiyo unakubali kwa dhati kabisa muamuzi wa mwisho ni mwananchi kwenye sanduku la kupigia kura hiyo siku ya siku, basi tusubiri hiyo siku ya siku ili waamuzi waamue badala ya wewe kuwasemea.
 
Dola sio kichwa cha mwendawazimu. Huwezi kuwapa watu wafanyie majaribio.

Samahani sana tena sana sana ZeMarcopolo utueleweshe kuhusu Somo la uraia jinsi chama cha siasa kinavyopata ridhaa ya kuongoza DOLA. Narudia tena samahani kama nimekukwaza kwa lolote lile. No one is perfect... That's why pencils have erasers.
 
Chadema hawana sifa za kuongoza dola huo ndiyo ukweli.

...kwa sababu hata paka anaweza kuongoza TZ at this moment!

Kwani unahitaji nini kuweza kuongoza waswahili kama wewe? Wawekezaji tu! Wala hauhitaji kujua wanafanya nini au mkataba ni wa aina gani. You just trust them as long as hawakunyang'anyi ulaji wako.

Subirini tu, evolution is against you, people slowly have started to discover their power and what they can do with it.

Ipo siku tutajua mbivu na mbichi ni zipi kama wakenya, na nina uhakika hiyo siku itakapokuja mchuano hauta kuwa kati ya ccm na cdm, kwa sababu ccm haina future.
 
mzeluu Nara ferre.g Ruttashobolwa na wengine ni lazima tukubali kwamba kuna mahali CHADEMA wanakosea. Hebu tuambiane ukweli hata wale wanaojidai kwamba ni wapiganaji damudamu ni kwa nini thread zinazohusu ujenzi wa CHADEMA huwa hawazichangii?

Sidhani kama ni lazima wachangie, ila nina uhakika wapo humu wanacollect information.
 
2015 it's not who vote that count ... It's who count the votes... Bila tume Huru na ya Haki ... CDM itahesabu Maumivu ... Kazi Sasa iwe kuakikisha tume Huru inapatikana .. Mengine ni mbwembwe tu

Hakuna maumivu endapo wapiga kura wataamua, Angalia ushindi wa Ubungo, mbeya na pale kwa masha, Pamoja na kutumia mabomu mpaka ya moto, baada ya wapigakura kusimamia vilivyo jahazi halikuzama. ila angalia pale kibaha hali ilikuwa tofauti. Pia nakumbuka 2004 uchaguzi wa serikali za mitaa nikiwa vingunguti CUF walisimamia na wa CCM waliangushwa na kutaka kupindua hesabu walikwama na kukataa kusaini matokeo na siku ya Nne ilibidi Makamba asaini kwa niaba. Wakapora na ofisi wakadai ilikuwa ni ya chama sio serikali lakini vijana walipangisha kwingine na leo uaniona vingunguti iko tofauti. Hivyo hakuna kukata tamaa kwani CCM hawatokaa wakubali tume huru kwa kuwa ndio kisu chao.
 
hapo kweli pana kazi ila imani yangu kwa cdm ni kubwa tujitahidi kutoa ushauri ambao ni positive kwa chama
Ni kuongeza nguvu za M4C tu, na kuwaelimisha wapigakura kutoogopa mabomu ya machozi hata ya moto, na badala yake walinde kura zao na kuhakikisha zinasomwa kama zilivyo
 
Naunga mkono hoja za mtoa hoja,chama mzichukue na kuzifanyia kazi kadiri itakavyowezekana,lakini napenda kushindilia sehemu moja,nayo ni CHAMA KUANZISHA TELEVISION na GAZETI letu haraka,hii itakuwa ni nyenzo MUHIMU SANA,..WanaCDM tupo tayari,tunasubiri taarifa na jinsi ya kutekeleza,..fanyeni hima viongozi,na wala msiogope,nguvu ya umma hushinda yote,tuliweza suala la KATIBA,sembuse hili...
 
Back
Top Bottom