Chadema: Kwanini vyuo vikuu

Chadema: Kwanini vyuo vikuu

elimukwanza

Senior Member
Joined
Dec 27, 2010
Posts
169
Reaction score
23
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.

Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana-take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la DOWANS.

Unajua tatizo aliko vyuo vikuu, tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.
 
Bahati mbaya huna elimu ya chuo kikuu, ungekuwa na elimu hiyo ingekupa uwezo wa kujuwa kwa nini wanafunzi wa vyuo vikuu ni muhimu na sio wale wa VETA.
 
Action And Reaction Are Equal And Opposite

(hiyo aya ya pili kuna mtu alikupokonya keyboard?)
 
Kwa sasa wanafunzi hao wa vyuo vikuu ni wa muhimu sana ili wasaidie kutoa elimu ya uraia kwa ndugu zao waliopo vijijini, kama ulivyosema kuwa wengi wa wanafunzi hao wamatoka vijijini.

CDM wamefanya vizuri kutumia mbinu hii na vyama vingine vya upinzani navyo vinatakiwa kuiga mfano huo wa CDM ili elimu ya uraia iwafikie watu wengi zaid.
 
Sasa wewe point yako ni ipi?
kwanini wanaenda vyuoni au kwanini wasiende?
Mbona una jichanganya mwenyewe tena?
 
Hilo ndilo tatizo la wabongo wanataka kusikia yale tu yanayowapendeza. Iilianzia CCM sasa CDM nalo inalinyemelea.

Point yangu: Siyo vibaya kutumia vyuo vikuu lakini wanatakiwa waende mbali zaidi, kama unakumbuka mkakati wa kutumia vyuo vikuu walianza NCCR baada ya uchaguzi wa 95, leo wamebakiwa na Mvungi tu na kusubiri watu yatakayowashinda CDM au CCM.

Kuna watu kama akina Waitara, Rugemalila na wengine wengi waliokuwa viongozi wa wanafunzi walinunuliwa CCM kwasababu ya njaa wakadhoofisha upinzani. Kule vijijini watu wako stable means siyo kama hawa wa vyuoni baada ya miaka 3 huwaoni tena.
 
Hebu tafuta hoja nyingine au rekebisha ili tuelewe unataka kutupa ujumbe gani.
Confusion!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
CHADEMA NI 'CHANDA CHEMA' HIVYO WANAFUNZI WA VYUO VIKUU
WAMEHIARI KUKIVISHA TU PETE WENYEWE

Katika swali lako hilo hapo juu wala usifikiri kwamba uko peke yako tu. Hata CCM, CUF na vikundi vingine wamepigwa butwaa hivo hivo usipime!!! Kwa bahati nzuri sana taarifa zinasema kwamba CHADEMA hualikwa na wanafunzi wenyewe na wala hawajipereki kwao.

Kwa mfano jana wapambanaji walivyokua Makumira Arusha, tayari humu ndani tuliona wachangiaji kibao kwenye THREAD fulani hivi wakiwaomba viongozi wa CHADEMA wawatembelee na wao kule Mkoa wa Iringa wakisema kwamba vyuo vyote mkoani humo vikiwemo Tumaini, Ruaha, Mkwawa, Klerruu, VETA na nyinginezo tayari wanafanya matayarisho ya kufanikisha jambo hilo.

Pamoja na yote mzee siku zote mtu yeyote anayependa kutambua, kuheshimu na kutetea maslahi ya taifa badala ya kutetea maslahi binafsi ya vijikundu vijikundi vidogo vidogo vya kifisadi, siku zote mtu huyo au chama hicho hupendwa sana na wananchi na mambo yake kwenda kiulaiiini kama hivyo unavyoionea gere sasa hivi CDM. Karibu kundini kabla hatujafunga milango ya mabadiliko ya kweli Tanzania!!

Wanafunzi wa vyuo vyote nchini vikiwemo UDSM, UDOM, MAKUMIRA na sasa Tumaini Iringa, Ruaha na Mkwawa, hongereni sana kwa kujitambulisha na upande wa siasa za 'Nguvu ya Umma' nchini ambayo falsafa yake ni UTAIFA MBELE KAMA TAI na kusema watetezi wa maslahi binasi ya vikundi kama CCM siku zao kupigwa chini ndio umewadia.
 
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.

Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana-take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la DOWANS.

Unajua tatizo aliko vyuo vikuu, tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.

Kuna kitu ulitaka kusema, embu soma vizuri post yako.
 
Hilo ndilo tatizo la wabongo wanataka kusikia yale tu yanayowapendeza. Iilianzia CCM sasa CDM nalo inalinyemelea.

Point yangu: Siyo vibaya kutumia vyuo vikuu lakini wanatakiwa waende mbali zaidi, kama unakumbuka mkakati wa kutumia vyuo vikuu walianza NCCR baada ya uchaguzi wa 95, leo wamebakiwa na Mvungi tu na kusubiri watu yatakayowashinda CDM au CCM.

Kuna watu kama akina Waitara, Rugemalila na wengine wengi waliokuwa viongozi wa wanafunzi walinunuliwa CCM kwasababu ya njaa wakadhoofisha upinzani. Kule vijijini watu wako stable means siyo kama hawa wa vyuoni baada ya miaka 3 huwaoni tena.
ElimuKwanza, pointi yako ni mzuri sana kwamba CDM kusirudie makosa bali tuwe makini zaidi katika kutumia hii strategy ya kuwakomba wasomi nchini.

Great Thinkers, tuwe tunasoma hoja kwa ukamilifu wake kwanza ndio tuweze kuchangia uzuri mawazo yetu.
 
Elimu ni Ukombozi.

Ni matarajio yetu kwamba wanafunzi wa Vyuo Vikuu ni kundi muhimu ndani ya jamii kutokana na namna wanavyopaswa kufahamu kuchambua matatizo ya jamii yao. Chuoni ni mahali pa kupika watu wanaohitaji kuisaidia nchi yao wenyewe.

CHADEMA kupitia kwa wanafunzi, ni mkakati imara na endelevu katika kuwaandaa na kukazia yale wanayojifunza kupambanua dhuluma zinazowakabili wananchi ndugu zao vijiijini. Ni mwanzo wa jamii nzima kujikomboa kifikra, kijamii, kisiasa na kiuchumi.
 
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.

Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana-take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la DOWANS.

Unajua tatizo aliko vyuo vikuu, tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.

Mkuu, unachanganya mambo. Wanafunzi wa vyuo vikuu wenyewe ndiyo waliwaalika viongozi wa Chadema kwenye kongamano lao wawahutubie. Chadema inaungwa mkono sana na wanafunzi wa vyuo, wasomi, wafanyakazi na watu wengine walioelimika. Hii ni kutokana na kuwa elimu yao imewafanya waweze kuchambua hoja za Chadema na kuzielewa na kuzikubali. Elimu yao pia imebaini kuwa CCM wametawala nchi hii kwa nusu karne (miaka 50) na kushindwa kuleta maendeleo hivyo ni muda sasa wa kuleta mabadiliko.

CCM bado inaendelea kuungwa mkono na baadhi ya wananchi wa vijijini kutokana na elimu yao duni. CCM wanatumia ujinga wa wananchi wake kuendelea kuwatawala kwa kuwatisha wasilinde kura vituoni, waogope wapinzani kuwa wataipeleka nchi iwe kama Rwanda au Somalia na wajigambe kuwa CCM ndiyo chama pekee cha kuleta amani na utilivu.

Kadri elimu inavyozidi kusambaa ndiyo jinsi CCM inavyozidi kuporomoka madarakani, watoto wa sasa wa primary na sekondari wakifikia umri wa kupiga kura 2015 wakaungana na wenzao wa vyuo ni kiama zaidi kwa CCM.
 
Back
Top Bottom