MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 319
- 755
Katika hali ya kushangaza unajiuliza hivi wale Mawakili wanaojifanya kuwa ndiyo Mawakili bora Tanzania, imekuaje wameamua kukaidi agizo la Mahakama la kuitaka CHADEMA kutofanya shughuli yeyote ya kisiasa na kioparesheni.
Mtakumbuka Juni 10, 2025 CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilipigwa marufuku kufanya shughuli zozote zile za kiutendaji na oparesheni mpaka pale kesi ya msingi iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Saidi Issa Mohamed na wenzake wawili (2) dhidi ya Baraza la Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA itakaposikilizwa.
Jaji wa Mahakama Kuu Hamidu Mwanga alisema zuio hilo linakuja kufuatia maombi yaliyowasilishwa Mahakamani hapo na Mawakili wa waleta maombi wakiongozwa na Wakili Gido Thomas Simfukwe ambao waliiomba Mahakama kuweka zuio hilo hadi kesi ya msingi itakavyoanza kusikilizwa.
Wakati maamuzi hayo yanatolewa, upande wa utetezi (CHADEMA) haukuwa na mwakilishi yeyote Mahakamani, hiyo ni baada ya aliyekuwa Wakili wake Jebra Kambole kutangaza kujiondoa kwenye shauri hilo hatua iliyopelekea Mahakama kuendesha kesi kwa upande mmoja.
Hivyo Jeshi la Polisi liko sahihi kusimamia amri ya Mahakama ya kuwataka CHADEMA wasifanye shughuli yeyote, na kama CHADEMA wana malalamiko basi mtu wa kwanza wanayepaswa kumlaumu ni Jebra Kambole, ambaye alifanya uamuzi wa kijinga wa kujitoa kwenye kesi.
Mtakumbuka Juni 10, 2025 CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilipigwa marufuku kufanya shughuli zozote zile za kiutendaji na oparesheni mpaka pale kesi ya msingi iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Saidi Issa Mohamed na wenzake wawili (2) dhidi ya Baraza la Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA itakaposikilizwa.
Jaji wa Mahakama Kuu Hamidu Mwanga alisema zuio hilo linakuja kufuatia maombi yaliyowasilishwa Mahakamani hapo na Mawakili wa waleta maombi wakiongozwa na Wakili Gido Thomas Simfukwe ambao waliiomba Mahakama kuweka zuio hilo hadi kesi ya msingi itakavyoanza kusikilizwa.
Wakati maamuzi hayo yanatolewa, upande wa utetezi (CHADEMA) haukuwa na mwakilishi yeyote Mahakamani, hiyo ni baada ya aliyekuwa Wakili wake Jebra Kambole kutangaza kujiondoa kwenye shauri hilo hatua iliyopelekea Mahakama kuendesha kesi kwa upande mmoja.
Hivyo Jeshi la Polisi liko sahihi kusimamia amri ya Mahakama ya kuwataka CHADEMA wasifanye shughuli yeyote, na kama CHADEMA wana malalamiko basi mtu wa kwanza wanayepaswa kumlaumu ni Jebra Kambole, ambaye alifanya uamuzi wa kijinga wa kujitoa kwenye kesi.