CHADEMA, kuweni makini na mtu huyu

CHADEMA, kuweni makini na mtu huyu

Inkognito

Member
Joined
Feb 13, 2011
Posts
86
Reaction score
108
Katika jitihada za kuhakikisha CHADEMA hawachukui jimbo la Morogoro mjini, Chama Cha Mapinduzi kimeweka mapandikizi wafuatao kama informer wao ndani ya CHADEMA Morogoro Manispaa.

Informer namba moja anayetumiwa sana na CCM ni Advocate Tarimo. Advocate Tarimo alikuwa ni mwanachama wa TLP na amewahi kugombea udiwani kwa tiketi ya TLP katika kata ya kichangani lakini hivi karibuni ameingia CHADEMA na kupewa nafasi ya kushiriki vikao vya chama kama mjumbe mwalikwa katika kamati tendaji ya CHADEMA wilaya ya morogoro mjini

Kujiingiza kwa Advocate Tarimo ni mkakati wa CCM kwakuwa habari za kuaminika ni kwamba advocate tarimo. Amekuwa akiwasiliana mara kwa mara na Katibu Mwenezi wa CCM kwa kutumia namba 0715972*** na kwamba mipango na mikakati yote ya CHADEMA kwa jimbo la Morogoro mjini huandaliwa na Advocate Tarimo ambaye anakingiwa kifua na uongozi wa CHADEMA wilaya.

Kimsingi, uelewa wa mambo kwa viongozi wa CHADEMA Moro mjini ni mdogo ukilinganisha na kasi ya CHADEMA kisiasa kwa sasa lakini viongozi hao kwa kutokujua wamekuwa wakiwashirikisha watu wasiowajua kwa sababu zao binafsi.

Habari kutoka kwa mmoja wa afisa usalama wa taifa ambaye ni mzalendo zinadokeza kuwa, Kwa sasa Advocate Tarimo analipwa fedha kwa ajili ya kazi hiyo ya CCM kiasi cha kumfanya muda wote awe bize na shughuli za CHADEMA, anahudhuria na kuandaa ripoti na nyaraka zote za chama ambapo nakala zake na taarifa huziwasilisha kwa CCM.
 
Watashindana nasi ila hawatashinda...Ikiwa Mungu yu upande wetu nani awezaye kutupinga...? Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu...

Kama habari hizi ni za kweli basi ni bora uongozi wa juu wa CDM uwe makini sana...

Ahsante kwa taarifa ...
 
Yani hizi jitihada CCM wanazofanya kupambana na CHADEMA.....
wangezitumia kukabiliana na matatizo ya nchi hii, tungekuwa mbali sana!!!
ugumu wa maisha ingekuwa ni msamiati!!!
 
Mleta taarifa wewe ni miongoni mwa wagombea wa Morogoro Mjini? Huyo ADvocate anajishughulisha na kesi za aina gani hapo moro, za wananchi wa kawaida, makampuni ama ni za aina gani?
 
Moro ipo ktk JIMBO LA Kati (Singida, Dodoma, Morogoro).
Hili suala linatakiwa kuchunguzwa na nafikiri TUNDU LISSU anapaswa kuliangalia hili kwa kuwa liko ndani ya kanda yake ingawa bado hajachaguliwa kiongozi atakayesimamia kanda hii.
 
Habari hizi kama zina ukweli fulani hivi, ngoja nizifanyie uchunguzi wa kina nitarudi kuwajuza.
 
tutakuja kuweka kambi! na wadau walio karibu na ofisi za chama mpeni taarifa hizi "heche"
 
Huu upuuzi wa kila mtu kuleta jambo analohisi litatokea iwe kwa kuota, kuhisi, kunusa au kwa namna yoyote toka chadema limegeuzwa kiofisi kufanyikia hapa Jf?
Au ndo kusema vijana wa chadema wanapenda sana umbea?
 
Unachonitatiza ni kimoja tu je hapa JF ndio ofisi za CDM? Hujajifunza kwa yaliyotokea? Sisi hapa ukileta habari za ndani ya chama humu jamvini tunakuona kama mnafiki maana sasa hapa unataarifu CDM au unataarifu na wabaya wake wajiweke tayyari. Hata siwaelewi nyie vijana na hii mitandao siku hizi
 
Kuita upuuzi jambo ambalo hujalijua ni utamaduni uliojengwa na ccm,wanapinga kabla ya kufanya utafiti.Hata ishu za epa zilianza kupingwa kama wewe upingavyo lakini baadae ukweli ukajulikana wote
 
Kuita upuuzi jambo ambalo
hujalijua ni utamaduni uliojengwa na ccm,wanapinga kabla ya kufanya
utafiti.Hata ishu za epa zilianza kupingwa kama wewe upingavyo lakini
baadae ukweli ukajulikana wote

Kamanda Ben Saa8 atumwe ili kuchunguza ukweli
 
Hizi ni fitina tu za kumchafua advocate Tarimo ambaye anajitolea muda wake mwingi kuiomarisha chadema.
 
Chanzo cha taarifa hizi ni kipi? Madai mazito kama haya ni muhimu yakatolewa huku yakiambatana na source ili usiwape watu makini wakati mgumu wa kukuamini..na kama una mapenzi ya dhati ya kuiona CHADEMA ikiimarika, basi uende ngazi ya chama inayohusika ukatoe taarifa hizi usiishie hapa tu..

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Hapa morogoro akika viongozi hawendi na kasi ya Chadema, Mfano kuna lile tawi la kilakala toka lifunguliwe kipindi cha Movt 4 Change adi leo sijawahi kuona imefunguliwa kiasi cha kufanya vijana kulalamika bila kujua nani wa kumlalamikia. Hivyo hata hilo si la kulidharau kamwe.
 
kina Yuda huwa hawakosekani,wapo kila kona cha muhimu ni kuwadhiti kitechnologia.
 
Moro ipo ktk KANDA ya Kati (Singida, Dodoma, Morogoro).
Hili suala linatakiwa kuchunguzwa na nafikiri TUNDU LISSU anapaswa kuliangalia hili kwa kuwa liko ndani ya kanda yake ingawa bado hajachaguliwa kiongozi atakayesimamia kanda hii.

sawa lakini sio kanda ya kati ni jimbo la kati mbona mnapotosha umma?
 
Back
Top Bottom