CHADEMA Kutingisha Morogoro

CHADEMA Kutingisha Morogoro

Hakuna watu wabishi kama warugulu, na hakuna kitu kigumu kumbadilisha mawazo mrugulu. Kama Chadema wameweza kuwabalisha mawazo warugulu ambao walikuwa kipenzi kikubwa cha CCM na sasa wana support Chadema, basi nakubali kwamba sasa ni mwanzo wa mwisho wa CCM. Ila ninachohofia ni kwamba CCM haitakubali kuachia madaraka hata kama hawapendwi na wananchi. CCM wanaweza kutumia polisi, jeshi na usalama wa taifa ili kubaki madarakani kitu ambacho pia naona itakuwa ni ngumu sana.

Ushauri wangu kwa CCM na serikali yake ni kwamba wakubali matokeo kwamba hawapendwi na hawana mvuto tena kwa watanzania, hivyo wakae pembeni. Na kama kuna viongozi waliokwapua mali za Taifa ni hekima kuzirudisha mapema sana kabla Chadema haijachukua madaraka. Najua hilo ndilo litakalokuwa jukumu la kwanza la Chadema la kuwakamata wezi wa mali za Taifa wote na kuwafunga bila kusahau kurudisha mali hizo kwa watanzania. Sasa kwanini kuja kupata aibu na fedheha baadaye wakati unaweza kurudisha mali hizo sasa na ukasamehewa?. Na pia kuna uwezekano mkubwa sana viongozi wengi wa chama na serikali iliyo madarakani wakakimbia nchi pamoja na familia zao kukwepa matatizo yatakayo wakuta mara tu baada ya CCM kuangukia pua. Nakipenda chama cha mapinduzi lakini hakipendeki, na wala sioni matumaini ya kubadilika hivi karibuni. Tumepoteza lengo, maana, na sababu ya kuwepo madarakani. Na mwisho napendekeza kwamba kwenye bendera yetu ya CCM tubadili zile alama za jembe na nyundo. Kwa sasa CCM si chama cha wakulima na wafanyakazi bali ni chama cha walaji na mafisadi. Hivyo tuweke alama ya kisu, kijiko, paja la kuku na milango ya bank kuu ikiwa wazi kwa ajili yao.
 
Kwa sasa anatambukishwa mbunge mtarajiwa wa jimbo la Igunga kamanda Joseph Kashindye akie mfumua Peter Kafumu wa ccm kwenye kesi iliyotengua ubunge wa Magamba Igunga.
 
Hiyo ndiyo nchi ya UTULIVU NA AMANI ya Mh, J M Kikwete na wafuasi wake wa CCM. mkoloni hakuwafanya hivi watanganyika.tujionee wenyeweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee damu za watu wasio na hatia inamwagika bila sababu.
 
Kontena la silaha alilosema Dr. Slaa limeanza kufanya kazi. Range wanafanyia mjini badala ya Mzinga na Ngerengere?
 
Tungekuwa na karadio ketu, tungekuwa tunapata update ya kinachoendelee Moro saa ii!

Tusubiri, TBC I, watueleze wanachopenda.
 
Jamani mbona update zinasuasua toka moro? Hakuna jf members wengi huko?
 
Jamani mbona update zinasuasua toka moro? Hakuna jf members wengi huko?
Tulikaa kikazi zaidi, na mkutano wa ndani unaendela. Kama ulidhani neno hukuna kulala ni utani, leo Morogoro imeangukia CDM. Nitaweka picha kesho. Mabomu yamefanya macho yangu yasione vizuri kwa sasa. Lakini Tumepoteza kijana mmoja kwe uzembe wa FFU. Inaonekana kelengwa mu kichwa na risasi ya moto. Na alikuwa anasoma gazeti, na inasemekana alikuwa ni muuza gazeti. Njia niliyotumia kuingilia msamvu ilikuwa front line. FFU wapiga watu bila makosa.

Mkutana ulikuwa nyomi, kwa mujibu wa wenyeji wa Moro haijawahi kutokea, licha ya mbinu chafu cha makada wa CCM kujaribu kutumia polisi kuhujumu mkutano. Mida ya saa kumi shughuli nyingi za Moro zilisimama maana watu wengi walikuwa mkutanoni

Dk wa ukweli na timu yake wamemchana kiuhakika mbunge wa Moro, na Polisi wilaya. Kiasi cha waruguru kutupa hovyo kadi za CCM. Hotuba ilikuwa sio ya kawaida, ilikuwa ya kisayansi.
 
Tulikaa kikazi zaidi, na mkutano wa ndani unaendela. Kama ulidhani neno hukuna kulala ni utani, leo Morogoro imeangukia CDM. Nitaweka picha kesho. Mabomu yamefanya macho yangu yasione vizuri kwa sasa. Lakini Tumepoteza kijana mmoja kwe uzembe wa FFU. Inaonekana kelengwa mu kichwa na risasi ya moto. Na alikuwa anasoma gazeti, na inasemekana alikuwa ni muuza gazeti. Njia niliyotumia kuingilia msamvu ilikuwa front line. FFU wapiga watu bila makosa.

Mkutana ulikuwa nyomi, kwa mujibu wa wenyeji wa Moro haijawahi kutokea, licha ya mbinu chafu cha makada wa CCM kujaribu kutumia polisi kuhujumu mkutano. Mida ya saa kumi shughuli nyingi za Moro zilisimama maana watu wengi walikuwa mkutanoni

Dk wa ukweli na timu yake wamemchana kiuhakika mbunge wa Moro, na Polisi wilaya. Kiasi cha waruguru kutupa hovyo kadi za CCM. Hotuba ilikuwa sio ya kawaida, ilikuwa ya kisayansi.

Asante sana kamanda na pole sana.Lakini kumbuka ahadi ni deni.Kesho utuwekee picha kama ulivyoahidi.
 

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Slaa, akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Morogoro na vitongoji vyake, katika mkutano wa hadhara wa operesheni sangara, kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Uwanja wa Ndege


Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Morogoro waliojitokeza katika mkutano huo.

Makamu Mwenyekiti CHADEMA Zanzibar Said Issa Mohamed akifafanua jambo kwa wananchi hao.

Aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Igunda kupitia CHADEMA, Joseph Kashinde akizungumza na wananchi waliohudhuria katika mkutano huo


Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Morogoro na Mbunge wa viti Maalum CHADEMA Suzan Kiwanga akimwaga sera za chama hicho.


Mkurugenzi wa Habari na Uenezi CHADEMA na Mbunge wa jimbo la Ubungo Jijini Dar es Salaam John Mnyika akipanda jukwaani wakati akiwasili katika uwanja huo
 
Hapa zimeagiza risasi, mabomu ya machozi, hadi kuua lakini wapi. Hakuna rangi Ccm haitaona. Mluguru amegundua ilipo lulu hivyo shamba hauzi tena. Hongera sana CDM. Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu!
 
Risasi na mabomu yao yatajeruhi mwili lakini haziwezi kujeruhi fikra za kidemokrasia na Maendeleo zilizomo kwenye miili hiyo!
 
Back
Top Bottom