CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi

CHADEMA kuna Ombwe la Uongozi

Wewe Juliana Shonza huhitajiki Chadema, wewe ni kapi na endelea uliko mamluki wewe. Tuache wana mapinduzi na wazalendo tuendelee na kampeni zetu. Pandikizi mkubwa wewe.
 
Last edited by a moderator:
Juliana

Hujambo binti,

Nimesoma andishi lako, hakika lina sura mbili kuu

1. Ni andishi la kufikirika kama ulivyoanza mwanzo kwamba umekusudia kuwafikirisha tu makutano, hakika umefikirisha tu na huna uhakika na usemacho.

2. Umejitoa ufahamu na umang'amuzi wa nera katika kudurusu mambo mtambuka ya husuyo siasa na utawala, kwabahati mbaya kuyapuuza maonyo yangu lakini sitanyamaza kukuonya tena,

Kama akina Chahali na Mwanakijiji unawaamini kuwa ndio kipimo cha uthabiti wa Yericko bora Yericko awe na iq ndogo kwamaana kwa msaada na uthubutu wake taifa litapona,

Siamini kama wamekutuma uwasemee, lakini kama ndivyo basi nami naliwajua wangali hawajakutuma wewe,
Hao watu nikujuzi tu kuwa hawana msaada kwa taifa hili na ni wakimbizi ambao hata kura hawatapiga.

Chadema ni taasisi peke yakisiasa iliyoyashinda majaribu na hila chini ya Mbowe, hujiulizi kwanini?

Mbowe hana bei, bei yake ni ccm kutoka ikulu tu, Mbowe ni mwanasiasa aliyezaliwa kutoka uanaharakati. Msimamo na
Financial status ya Mbowe ndio mwiba mkali kwa ccm,
hilo Shonza unalitambua,

Jiulize kwanini wewe na akina Zitto mlinunulika na ccm lakini Mbowe hajanunulika na leo anatuongoza kwenda ikulu?

Nikutakie siku njema my ex honey, mwambie jamaa kuwa "aliyechonga mzinga hula asali mpaka mzinga uanguke"!

Mimi sijambo..nijuze juu ya hali yako..?

Katika andiko langu lililobeba HOJA ya msingi nimesema bayana kuwa IQ ya Yericko Nyerere ni 0.0001, na hauwezi kufananisha uwezo wake na mtu kama Mwanakijiji ama Chahali..sikuwa nimekosea, ulichoandika hapa kimeendelea kuthibitisha maneno hayo na hata kuonyesha ziada ya UMBUMBUMBU wako.

1. Umesema sina uhakika na nilichokisema.,naomba nikuhakikishie kuwa ninauhakika wa asilimia zaidi ya 100 juu ya kile nilichokisema..nitajinukuu;
YERICKO NYERERE, A man with 0.001 IQ, Anaishi katika uongo na uzushi, mpaka kila mmoja amemmpuuza, Mwanakijiji, Chahali na WATABE wengine wa maandishi yenye adili, wameikacha CHADEMA, bado CDM haijiulizi, inajivunia kuwa na YERICKO.
- Nikutakie siku njema my ex honey, UONGO na UZUSHI ndio maisha yako.

2. Hoja yako nyingine inasema kuwa nimekupima kwa mtazamo wa wanaCCM..
Haiingii akilini mwanaccm unayapima mapungufu ya Yericko kwakutumia kipimo cha mwanaccm,
Niambie ni wapi na lini Mwanakijiji ama Chahali walijiunga na CCM na kuwa wanaccm..?

3.
Chadema ni taasisi peke yakisiasa iliyoyashinda majaribu na hila chini ya Mbowe
Kama unadhani kuwa CHADEMA ya sasa imeshinda majaribu basi ni katika KUTHIBITISHA tu ukweli na uwezo wa IQ yako..,CHADEMA ambayo inaenda kwenye uchaguzi ikiwa na Mgombea asiyejua misingi, dhamira, vision na hata mission ya Chama, Chadema inayoenda kwenye uchaguzi ikiwa haina Katibu Mkuu na kawaida kwenye uchaguzi wowote katibu mkuu ndio mratibu wa shughuli hiyo..CHADEMA inaenda kwenye uchaguzi ikiwa defensive, inaanza kujitetea na kumpiga dodoki mgombea wake kisha ndio iombe kura..,CHADEMA ambayo imepoteza mandate na legitimacy ya KUKEMEA RUSHWA, na badala yake imekumbatia Rushwa na wala rushwa. Uchaguzi ni mwepesi sana kwa CCM kuliko chaguzi zake zote, CCM inasema na kuionyooshea CHADEMA na wapinzani vidole bado kwa UJINGA unasema CHADEMA imeshinda majaribu...wakati kila mmoja anajua kuwa LOWASSA kainunua CHADEMA kwa Bilioni 20...ni aibu.

4.
Financial status ya Mbowe ndio mwiba mkali kwa ccm,
Ndugu yangu kama haujui vitu ni vyema ukanyamaza kimya..financial status ya Mbowe ndio mwiba kwa CCM??? Kumbe kwenye miaka yote CCM wanaogopa financial status ya MBOWE na sio HOJA za wanachadema bungeni na katika majukwaa ya siasa..? Huu ni ujinga uliopevuka, nathubutu kuuita UMBUMBUMBU..Yericko wewe ni MBUMBUMBU.

Hivi kwa akili yako NDESAMBURO na MBOWE nani ana financial status nzuri..? kwanini asiogopwe ndesamburo.? Labda utueleze hapa jamvini, MBOWE anamiliki kiasi gani katika benki,na katika jumla ya vitu vyake (nyumba, mashamba n.k) ili tukubaliane na Hoja yako kuwa Financial status ya MBOWE ni Mwiba kwa CCM..

Bali ninachojua mimi, Mbowe ni mpiga dili, aliwahi kuiuzia CHADEMA magari mabovu kwa bei ya juu, aliwahi kudai fedha iliyotumika kwenye uchaguzi 2010 akidai ilikuwa ni ya kwake hali ya kuwa alipewa na wafadhili kwa ajili ya Chama, Mbowe ameiuza CHADEMA kwa Lowassa kwa bilioni 20 na taarifa nyingine ambayo hauijui ni kuwa KITEGA UCHUMI kikubwa cha mbowe, Club ya BILLICANS imefungwa baada ya watu kuweka mgomo baridi, watu wanakusanyika Maisha BAsement, HIGH SPIRIT. RHAPSOD na Club zingine za wajanga wakila ujana..Huyo mwenyekiti wenu amechacha..

Kimsingi hauna hoja yeyote ya msingi ambayo umekuja nayo zaidi ya kuja kutimiza wajibu wako uliotumwa wa kuitetea CHADEMA na MBOWE mitandaoni..shame on U..
 
Flasafa za vyama vya upunzani ni kweli zimepotea kutokana na kujiingiza katika siasa za umaarufu, hali hiyo inafanya vyama kukosa misingi imara ya hoja matokeo wamekuwa wakijibu hoja zinazo vumishwa juu yao.wameanguka wanatakiwa kujiuliza 2020
 
Inawezekana lakini
Yasemwayo ...............

Hizi ni siasa wenyewe ndio wanaozijua, wakishauriana washauriane,isitoshe huyo aliyetoa post alikuwa miuongoni mwao, basi, ila mimi napita tu
 
Tatizo kubwa wametawaliwa na uchu na urohoo wa madaraka Hakika dhambi hii itawaumiza sana
 
Acha umbea toka lini ccm ikawa mshauri wa CHADEMA:what::banghead:ama kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni nikuambie kitu hii nchi ni yetu sote tunajua baya na jema kwa hiyo usipoteze pumzi kutuambia hii nyeusi wakati ni nyeupe ni m.baya jully angalizo ukiwa mnafiki ujanani uzeeni utakuwa mchawi.

Kama ni hivyo basi lowassa mchawi maana ujana wake wote alikua CCM, vip na hapo una jipya la kuongea
 
Acha umbea toka lini ccm ikawa mshauri wa CHADEMA:what::banghead:ama kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni nikuambie kitu hii nchi ni yetu sote tunajua baya na jema kwa hiyo usipoteze pumzi kutuambia hii nyeusi wakati ni nyeupe ni m.baya jully angalizo ukiwa mnafiki ujanani uzeeni utakuwa mchawi.
Ni maoni tu, ila mtu ana uhru wa kuzungumza ila tu, azungumze ukweli, mwacheni aseme ukweli
 
tukiacha ushabiki , na kuweka pembeni nakusupport kwa asilimia 100, kwani hujaongea tu bali mambo yako wazi na yananonekana ni kweli, tatizo la ukawa hawapendi kuambiwa ukweli wanapenda uongo zaidi,, waswaili wanasema ambea hapendi kuambiwa maana , hajui maaana, fikra zao zimeshajikita sehemu moja hivyo utakavyowaambiwa watadhani unawasengenya , ila ukweli ndo huo kabisa!!
 
tukiacha ushabiki , na kuweka pembeni nakusupport kwa asilimia 100, kwani hujaongea tu bali mambo yako wazi na yananonekana ni kweli, tatizo la ukawa hawapendi kuambiwa ukweli wanapenda uongo zaidi,, waswaili wanasema ambea hapendi kuambiwa maana , hajui maaana, fikra zao zimeshajikita sehemu moja hivyo utakavyowaambiwa watadhani unawasengenya , ila ukweli ndo huo kabisa!!
 
CHADEMA kuna matatizo makubwa na ya msingi..moja ya tatizo lao KUBWA ni kupuuzia matatizo yao.
 
Wataanza kupoteana tuu wenyewe baada ya oct 25, sijui sasa watamwita nani msaliti au kanunuliwa.
 
Juliana wewe ni mwanaccm kwa sasa ya Chadema tuachie wenyewe.Umemsikia Mkapa ametuamgia kwamba sisi tu Wapumabavu na Malofa.Hakuachia hapo amemalizi juzi kwa kutuita mbumbu hakuna shida.

Maana Mpumbavu na Lofa ni vyema akaongozwa na Mpumbavu na Lofa mwenziwe.Na pia ni bora Mbumbu akaongozwa na mbumbu mwenziwe.

Fanya yako ya kwetu tuachie hayakuhusu.Ni wakati wa kampeni uza sera za chama chako.Cha kwetu tuachie.
 
Juliana wewe ni mwanaccm kwa sasa ya Chadema tuachie wenyewe.Umemsikia Mkapa ametuamgia kwamba sisi tu Wapumabavu na Malofa.Hakuachia hapo amemalizi juzi kwa kutuita mbumbu hakuna shida.

Maana Mpumbavu na Lofa ni vyema akaongozwa na Mpumbavu na Lofa mwenziwe.Na pia ni bora Mbumbu akaongozwa na mbumbu mwenziwe.

Fanya yako ya kwetu tuachie hayakuhusu.Ni wakati wa kampeni uza sera za chama chako.Cha kwetu tuachie.

Kuwa na Akili wewe Juliana alikuwa kiongozi wa Bavicha hivyo lazima afuatilie kama mwanasiasa na atoe ushauri ili kuleta changamoto katika siasa. NB Hizi ni siasa za Vyama vingi.
 
Back
Top Bottom