CHADEMA Kumuondoa Lema Arusha

CHADEMA Kumuondoa Lema Arusha

MUSSA ALLAN

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2013
Posts
18,925
Reaction score
13,279
Wanajamvi! Amani idumu Tanzania!


Hizi ni habari zenye uhakika 100% nilizozipata kutoka ndani ya CHADEMA na zikathibitishwa na mmoja wa viongozi wakuu hapa mkoani.

CHADEMA kupitia mwenyekiti wao wameongea na Mbunge wa Arusha mjini Bw Godbless J Lema na kumuomba asigombee tena ubunge wa jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho.

Habari zaidi zinasema, CHADEMA wamefikia hatua hiyo baada ya kugundua kuwa wakazi wa Arusha mjini hawana tena Imani na Bw.Lema baada ya LEMA kushindwa kutimiza karibia asilimia 98 ya ahadi zake kwa wana Arusha, Kwahiyo kama angegombea angeshindwa vibaya na hivyo kuwa ni aibu kwa chama hicho, ukichukulia kuwa wameshatangaza kuwa Arusha mjini ni ngome yao.

Suala lingine lililosababisha CHADEMA kumuondoa LEMA ni hili la wanachama wengi wa CHADEMA ambao nao ni viongozi katika ngazi za chini kuonyesha wazi kupingana na uongozi wa Mbunge huyu! Kwa mfano kijana wa CHADEMA siku nyingi Bw.Noel Ole Veroya kutangaza Nia ya kumn'goa LEMA Arusha. Hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na siasa za fujo alizosiasisi Ndg.Lema.

Suala la Ukabila nalo Limechukua nafasi yake, kwani Bw.Noel ametajwa kuwa ni mzawa wa Arusha huku Godbless LEMA akishawishiwa akagombee Jimbo la HAI(Nyumbani kwao) kwani Mbowe anatarajiwa kuhamia jimbo la Moshi mjini.

Pia CHADEMA imemtoa wasiwasi Bw.LEMA kwamba iwapo atakosa nafasi ya Ubunge watampa cheo kama kile cha NAPE, kwahiyo hatakufa njaa hapa mjini.

Wapiga Kura wengi wa Arusha mjini wamefurahishwa na habari hizi kwani wengi wao wamechoshwa na vituko vya Mh.LEMA na sasa wanataka maendeleo.
 
MUSSA ALLAN

Naona sasa yale makarai ya kujengea yameanza kutumika waliowatumima wakishamaliza kazi zao mnakuwa delete hamna kazi tena ccm my foot kushinda arusha october ni jama Myahudi kumwozesha bint yake kwa Mpalestina.
 
Bado Lema ana miaka 50 ya kuongoza jimbo la Arusha...atawafirimba magamba mpaka basi.
Kazi uliyopewa ya kushinda huku JF na kuanza kumfukuzia Lema na Dr. Slaa naona Watanzania wameshakushtukia. Lakini upo kazini endelea kupiga mihela kwa kutunga uzushi humu bila hivyo wewe na familia yako hamuendi Msalani ng'o
 
Muache kiongozi wa taifa aingoze Arusha waliokutuma kawaambie Lema anakubarika nchi nzima si Arusha tu!
 
Bado Lema ana miaka 50 ya kuongoza jimbo la Arusha...atawafirimba magamba mpaka basi.
Kazi uliyopewa ya kushinda huku JF na kuanza kumfukuzia Lema na Dr. Slaa naona Watanzania wameshakushtukia. Lakini upo kazini endelea kupiga mihela kwa kutunga uzushi humu bila hivyo wewe na familia yako hamuendi Msalani ng'o

Wewe na MBOWE nani anayejua majaliwa ya LEMA?
 
MSALANI, hayo ndo maazimio ya kikao cha kisiwandui kule nchini Zanzibar, Naam wala hatushangai njooni na drama zote za kila aina ila tambueni mnachokifanya ni sawa na kupaka rangi hewa..!!!

Wananchi wanajua wanachokifanya na wanayemtaka. Lema ataamua mwenyewe lini asigombee ama astaafu kuwa mbunge wa Arusha yule Mch, nani sijui mtafutieni kata ya kugombea achaneni kabisa na habari ya Ubunge kwa Arusha.

BACK TANGANYIKA
 
Lema hatufai wana Arusha kama vipi kagombee kwa kina SOCIOLIGSTTZ Ndo wanataka matapeli wa Siasa
 
Wanachadema Arusha hovyo kabisa,

Hamjui hata habari za ndani za chama chenu?

Jana baada ya mkutano na wadau pale CORRIDOR SPRINGS Mbowe alifanya kikao cha siri na viongozi wa CHADEMA pale SAFARI Hotel na haya ndio yaliyojiri!
 
Kam humuamini hata mwenyekiti wa chama chako wewe si msukule tu!

Huwezi simulia mvua isiyokunyeshea na wewe utakuwa msukule mwenzangu huwa tunapishana usiku leo tripu za wapi msukule wa lumumba.
 
Huwezi simulia mvua isiyokunyeshea na wewe utakuwa msukule mwenzangu huwa tunapishana usiku leo tripu za wapi msukule wa lumumba.

LEMA kwa sasa ni Mbunge wa Arusha mjini, na mimi ni mkazi wa hapa, Mvua ipi unyozungumzia?
 
Back
Top Bottom