CHADEMA: Kujipanga kwa Ukombozi hakuna Ukomo

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,823
35,819
Ikumbukwe ipo tofauti kubwa kati ya Chadema na mashabiki mitandaoni.

Ni muhimu kukawa na focus ya hoja ipi inamhusu nani katika wawili hao.

Kumekuwa na maangalizo mengi ambapo kwa hakika Chadema kama chama kinapaswa kufikiria kuyafanyia kazi:

1.Lwaitama, Heche, Kigaila na wa namna hiyo katika kipindi hiki (ambacho Mbowe yuko gerezani na Lissu yuko nje ya nchi) ni muhimu wasiwe mbali na hatamu za uongozi wa chama.

2. Agenda za chama ni muhimu zikaeleweka, na viongozi wakachukua jukumu la kuhakikisha wanachama na wafuasi wanazielewa.

3. Ni muhimu ikaeleweka kuwa kama chama cha ukombozi kupigania mageuzi makubwa yenye kuhitaji katiba mpya hakuwezi kutenganishwa na uanaharakati.

4. Kama chama cha harakati ni muhimu wasiokuwa tayari kuwa sehemu ya kuchukua hatua wakapisha, wakapiga kimya au hata kufikiria kujiunga ACT, TLP, nk huko kunako bata.

Msingi mzima wa kuyafikia malengo ukiwa uelewa wa wazi kuwa:

a) Minyukano ndani ya CCM haitusaidii kwenye madai yetu ya katiba mpya.
b) Mwendazake hayupo tena, makando kando yake tuhangaike nayo kwenye "haki na maridhiano" baada ya katiba mpya.
c) Agenda zetu ni za kudumu si marafiki.

Ni muhimu kutambua, Lissu na walioko uhamishoni kuja kwao kunategemea sana hali ya mapambano ardhini ilivyo.
 
Kwanza kabisa ijulikane hakuna siasa isiyo na harakati, na miongoni mwa harakati za kwenye siasa ni maandamano na mikutano ya hadhara, hivi vinatambulika kisheria. Hivyo asitokee kipofu yeyote akawaambia Chadema waache harakati kwani kusema hivyo ni sawa na kuwataka wapotee kwenye uso wa ramani za siasa za Tanzania.

Lakini pia, nimekusoma kwenye hoja yako namba moja hao jamaa watatu uliowataja Heche, Kigaila, Lwaitama (tatizo umri), hao wawili wa mwanzo wanaonekana wako vizuri kwenye harakati, ni wapambanaji by nature, muhimu pawepo na wengine wa kuwapa support watu wapo.

Kinachohitajika sasa kwa upande wa Chadema kama chama ni namna ya ku-recover their political platform, warudi majukwaani na kwingineko, Sasa kama wata negotiate na polisi au CCM kupata hii haki yao i don't know, though kuna msemo "haki haiombwi", but wakilazimisha wanaweza kuishia kupewa vilema na hawa polisi wasiojitambua.

Hapa inahitahika akili nini kifanyike, kuhudhuria uke mkutano wa msajili ingeweza kuwa njia mojawapo, tatizo msajiki kama mtumishi wa serikali ya CCM angeweza kuwapa vile tu ambavyo vingempendeza yeye na mabosi wake.
 
Kwanza kabisa ijulikane hakuna siasa isiyo na harakati, na miongoni mwa harakati za kwenye siasa ni maandamano na mikutano ya hadhara, hivi vinatambulika kisheria. Hivyo asitokee kipofu yeyote akawaambia Chadema waache harakati kwani kusema hivyo ni sawa na kuwataka wapotee kwenye uso wa ramani za siasa za Tanzania.

Lakini pia, nimekusoma kwenye hoja yako namba moja hao jamaa watatu uliowataja Heche, Kigaila, Lwaitama (tatizo umri), hao wawili wa mwanzo wanaonekana wako vizuri kwenye harakati, ni wapambanaji by nature, muhimu pawepo na wengine wa kuwapa support watu wapo.

Kinachohitajika sasa kwa upande wa Chadema kama chama ni namna ya ku-recover their political platform, warudi majukwaani na kwingineko, Sasa kama wata negotiate na polisi au CCM kupata hii haki yao i don't know, though kuna msemo "haki haiombwi", but wakilazimisha wanaweza kuishia kupewa vilema na hawa polisi wasiojitambua.

Hapa inahitahika akili nini kifanyike, kuhudhuria uke mkutano wa msajili ingeweza kuwa njia mojawapo, tatizo msajiki kama mtumishi wa serikali ya CCM angeweza kuwapa vile tu ambavyo vingempendeza yeye na mabosi wake.

Kwenye harakati ongezea pia "infiltration" kwenye vyama hasimu.

Kama ni halali kwa kina katambi kuwekezwa kwetu, kwa nini iwe haramu kwa akina Mdee, Silinde au wowote kuwekezwa kwao?

Kabla ya KANU kuanguka Raila alijiunga nao.

Hivyo makamanda kuhamia kwao kimkakati isiwe uhaini. Ndiyo harakati zenyewe hizo.

Uwezekano wa hatari, kufa au hata kupata vilema ni pale tunapokuwa hatujadhamiria kikamilifu. Idadi ya watu kwenye shughuli inapokuwa kubwa hamasa yao kwenye kuumiza watu hupungua.

Aina za akina Lwaitama, Kigaila, Heche ni wengi. Ndiyo maana ya neno "akina." Wanasema waswahili wavumao baharini Papa, lakini na wengine wapo.

Watu wenye uthubutu uliotukuka wapewe nafasi. Ikumbukwe sote hatuwezi kuwa sawa kwenye nyanja zote.

Wengine wanaweza kuwa na mchango zaidi kwenye maeneo mengine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom