Mbona mmesema makatibu wa ccm wengi wanatoka kusini? Huo ni nini kama sio ubaguzi.? Basi na cdm mmefilisika kisiasa.Mie ninadhani umri hauna maana sana juu ya uimara wa chama hasa ukizingatia historia ya TANU kabla na baada ya uhuru huku ukizingatia upigwaji marufuku wa vyama vingi baada ya uhuru.....kutolewa baadhi ya huduma za msingi kama pasi za kusafiria, masomo ya juu nje ya nchi nk. kwa wanachama wa SISIEM pekee hili lililazimisha wengi kuwa wanachama kadi. Kama mikwaruzano ya ndani ya chama ndiyo dalili ya kufa chama basi SISIEM hivi sasa ingekuwa historia.... ichukulia mfano wa kura za maoni ndani ya CCM ni nani asiyejua kuwa zoezi zima lilitawaliwa na uchu wa madaraka au urafiki??.......mapambano ya ufisadi..............hata kujivua gamba pia.......... "ukiona mtu anauingiza udini au ukabila basi ujue amefilisika kisiasa"- Mwalimu JKN
crap. Yani kujadili ccm sawa, bt cdm kikijadiliwa mnasema ni vitu visivyo na maana. Poleni!!!Nadhani kama sitakosea sana kwa mujibu wa makamu mwenyekiti wa CCM na katibu muenezi (Nape) walisema watawatuma vijana kwenye mitandao ya kijamii kujibu/kutoa hoja za chama chao na SI KULETA VITU VISIVYOKUWA NA MAANA... Tafadhali fanyeni kazi mliyotumwa......:der:
dua la kuku......!!!hizi ndizo busara za mwendawazimu. Ccm imeshahukumiwa na historia na sasa inasubiri anguko lake kuu, la kishindo cha kutisha na kuleta simanzi kwa wahalifu waliojificha kwenye chaka hilo. hapa nape anajaribu kutushawishi kwamba eti chadema ina uchu wa madaraka! Hivi ni nani asiye na uchu wa madaraka hapa nchini? Tatizo si uchu wa madaraka, bali ni madhumuni ya mtu kutaka madaraka. Nape ni mmoja wa wenye uchu mkubwa wa madaraka na ana rekodi ya kuhongwa na kutulizwa mzuka. Uchu wa namna hii ni sumu kwa taifa na hatari kabisa. Hebu tukumbushane kidogo jinsi kijana huyu alivyokuwa akihaha kama kuku anayetaka kutaga yai muda mfupi tu kabla ya uchaguzi uliopita, wengi tuliamini kwamba kijana alikuwa mpambanaji mzuri dhidi ya ufisadi haswa alipokuwa akilalamikia chama kutekwa na mafisadi huku akiwataja kwa majina! Hakuwa ameishia pale, alihangaika huku na kule hadi kutafuta "ulaji" chadema alipotaka kujiunga nacho ambapo walimtolea nje, alijishughulisha pia na harakati za kuanzisha chama cha ccj kama tunavyoelezwa. Lakini wenye werevu wa kifisadi walijua alichokuwa akitafuta na homa iliyokuwa ikimsumbua; walimtupia mfupa; cheo cha kishemeji cha ukuu wa wilaya (dc) ambapo akatulia kama maji mtungini! Na sasa baada ya kunogewa na "uheshimiwa" nape amesogezwa usoni kwa kubebeshwa furushi lisilobebeka ndani ya chama kinachougua kansa na ukimwi wa kifisadi. Kwa maoni yangu nape, kwa kukubali kuhongwa cheo cha udc na baadae hiki alicho nacho (kwa mujibu wa falsafa ya mwasisi wa ccm hayati mwl.nyerere) amepoteza kabisa sifa ya kuwa mpiganaji dhidi ya ufisadi na anachofanya sasa ni tamithiliya ya maigizo. Nyerere alitamka hadharani kwamba "hakuna kiongozi atayewekwa madarakani kifisadi anayeweza kupambana na ufisadi" kama atabisha nape atueleze vigezo vilivyotumika kwa yeye kuteuliwa kuwa dc na si watanzania kibao wanaomzidi kila hali kuanzia elimu, umri, uzoefu wa kisiasa na hata haiba. Kwangu mimi, niliyewahi kufanya kazi chini ya hayati baba yake nape ni msaliti mkubwa kwa umma na falsafa aliyokuwa akiisimamia baba yake. Nathubutu kusema kwamba kwa kadiri nilivyomfahamu mzee yule asingekubali uteuzi wa kirushwarushwa ule. Mungu ibariki tanzania, mungu ibariki afrika.
what the hell are talking about?? You mean politic or Politics?? Nenda shule.cheap popularity is not a part of politic?
mnaonaje huu muda mnaopoteza hapa mngeutumia kujadili namna ya kukiokoa chama chenu na mbinu za kuwaondoa wale mapacha watatu!!mbona ufisadi mnauangalia upande mmoja au mbowe kukiuzia chama mafuso 3 kwa 480m na slaa kulipwa 7.5m huo sio ufisadi?
GET LOST!!Chama (kinachojiita) cha Demokrasia na Maendeleo kiko mahututi (ICU) na huenda kikafa rasmi kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015.
Utafiti binafsi nilioufanya bila kushirikisha REDET wala SYNOVETE unaonesha chama hicho kukosa mwelekeo na hivyo huenda kikavurugika kabisa kutokana na uchu wa madaraka.
Hali inayoendelea Arusha ni kielelezo cha ninayoyasema.
Wiki iliyopita VUA GAMBA aliandika uhalisia wa kile alichokiona kwenye chama chake. Katika maelezo yake alidai yeye ni mwanachama wa chadema lakini HAKUBALIANI NA MUAFAKA ULIOFANYIKA ARUSHA.
Alitoa sababu zenye mashiko na kudhibitisha bila shaka yoyote kuwa kilichofanyika ARUSHA ni kwa maslahi ya wachache.
Lakini wafuasi wa chadema hapa JF walimtukana, kumpuuza na kumwita shushushu, bila hata kujaribu kutafakari ukweli wa kilichokuwemo kwenye thread. Ajabu hata Dr.KITILA MKUMBO nae akaangukia kwenye mkumbo huo wa wenzake.
Lakini mbaya zaidi MODS wakamburn.
Cha kushangaza ni kuona eti walewale waliotetea muafaka hapa jamvini wakiongozwa na TUKUTUKU eti ndio wanasimama kuungana na LEMA bila hata chembe ya aibu.
Mlisema chadema sio chama cha fujo na wanakubali muafaka, sasa mmetoka wapi leo kumtetea LEMA? Historia itawahukumu.
Tunaongelea mabilioni ya walipa kodi yanayosombwa na baba zako wa magamba wewe unatuletea mambo ya mbowe/slaa!mbona ufisadi mnauangalia upande mmoja au mbowe kukiuzia chama mafuso 3 kwa 480m na slaa kulipwa 7.5m huo sio ufisadi?
Just tell them, maana wamelewa mbege. Huyo mchagga anafanya ufisadi mkubwa sana kwny hicho chama chao lakini hawaoni. Wanakazana kukodoa macho kwny vyama vya wengine.Bible says toa kwanza boriti jichoni kwako, ndipo utakapoweza kuona kibanzi kwenye jicho la mwenzako.mbona ufisadi mnauangalia upande mmoja au mbowe kukiuzia chama mafuso 3 kwa 480m na slaa kulipwa 7.5m huo sio ufisadi?
Jamani wanaJF,nimeamua kuleta hii thread hapa ili nipate mawazo na mitazamo ya great thinkers kuhusu hili suala.
Baada ya kumsikia mh.Freeman Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa cdm akijiapiza kuwa ataachana na siasa endapo cdm haitachukua nchi kutoka mikononi mwa magamba/mafisadi pamoja na kuangalia mwenendo wa watu kama Zito anaye apa kuwa hatagombea ubunge(japo ndio saizi yake kwa sasa)na kuutaka urais (japo sio saizi yake kwa sasa na yeye analijua hilo fika)na sasa kila mwenye uwezo wa kufungua kinywa chake bila kujali hata kama anachokiongea ni makapi anajitangazia kugombea urais kupitia cdm.
Najiuliza nini kitatokea kwa cdm endapo hakitashinda 2015?
Note:siwakatishi tamaa wapambanaji wa mabadilikoM4C kuwa cdm haitashinda,No ila nahitaji tu tafakuri .
Naomba michango.