CHADEMA jifanyieni tathmini

CHADEMA jifanyieni tathmini

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,091
Reaction score
136,650
Nyie CHADEMA sikilizeni....amkeni sasa.

Anzeni kuwa mnafikiria kwa hatua kadhaa mbele.

Hatua zenye manufaa kwa mustakabali wa chama chenu na viongozi wenu.

Hivi nyie mna idara ya usalama kweli? Kama mnayo, iweje suala la ulinzi kwa Tundu Lissu mlikuwa hamjaona umuhimu wake?

Kwa nini Lissu hakuwa na ulinzi imara wa watu wenye silaha za moto?

Kwa kweli hapo mmeudondosha mpira. Na kama mna watu wanaohusika na usalama ndani ya chama chenu basi hamna budi kufanya maamuzi magumu na kuwatimulia mbali.

Haiwezekani kiongozi mkubwa kwenye chama kama Lissu asiwe na usalama wa kueleweka.

Sijui mlikuwa mnaitegemea serikali kwenye hilo!

Kiongozi wa juu tena mwenye mbwembwe na cheche kama Lissu kutembea tembea bila ulinzi wa maana ni upumbavu.

Ni upumbavu kwa sababu tayari yeye atakuwa ni mlengwa wa mashambulizi toka kwa wabaya wake. Anapotembea bila ulinzi anakuwa ni shabaha iliyo rahisi sana kuilenga.

Haiingii akilini kwa nini hadi siku ya lile tukio mlikuwa hamjampatia ulinzi huyo mwanasheria wenu mkuu.

Shame on you.
 
Ya ccm yanawashinda unadhan ya chadema utayaweza? Pambanen na hal zenu za kwetu mtuachie wenyewe.

Ya ngoswe mwachie ngoswe

Sent using Jamii Forums mobile app

Mbona na nyie hampambani na hali yenu na mnaitegemea polisi iwakamate walohusika?

Nyie wafuasi hamna akili kabisa.

Mnachojua na mnachoweza ni kuzungusha mikono tu.
 
85ee72dfff91afa16bb78d787b3df31c.jpg
 
Nyie CHADEMA sikilizeni....amkeni sasa.

Anzeni kuwa mnafikiria kwa hatua kadhaa mbele.

Hatua zenye manufaa kwa mustakabali wa chama chenu na viongozi wenu.

Hivi nyie mna idara ya usalama kweli? Kama mnayo, iweje suala la ulinzi kwa Tundu Lissu mlikuwa hamjaona umuhimu wake?

Kwa nini Lissu hakuwa na ulinzi imara wa watu wenye silaha za moto?

Kwa kweli hapo mmeudondosha mpira. Na kama mna watu wanaohusika na usalama ndani ya chama chenu basi hamna budi kufanya maamuzi magumu na kuwatimulia mbali.

Haiwezekani kiongozi mkubwa kwenye chama kama Lissu asiwe na usalama wa kueleweka.

Sijui mlikuwa mnaitegemea serikali kwenye hilo!

Kiongozi wa juu tena mwenye mbwembwe na cheche kama Lissu kutembea tembea bila ulinzi wa maana ni upumbavu.

Ni upumbavu kwa sababu tayari yeye atakuwa ni mlengwa wa mashambulizi toka kwa wabaya wake. Anapotembea bila ulinzi anakuwa ni shabaha iliyo rahisi sana kuilenga.

Haiingii akilini kwa nini hadi siku ya lile tukio mlikuwa hamjampatia ulinzi huyo mwanasheria wenu mkuu.

Shame on you.


Una maana gani kusema shame on you?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mmmnh

inamaana viongozi wote/wabunge wote walindwe???

si wapo bungeni,wenye itikadi tofauti,

Mtu anayeongoza jimbo kwa ticket ya CCM,alindwe sababu katika jimbo lake,kuna walio na itikadi tofauti??ya ukawa kwa mfano
 
Kiongozi wa juu tena mwenye mbwembwe na cheche kama Lissu kutembea tembea bila ulinzi wa maana ni upumbavu
Usishangae, hili ni jambo dogo. Unaweza kuelewa kuwa Chama kilikodisha Choppa 4 kwa zaidi ya Tzs. bilioni 8 kuendesha kampeni za mgombea urais (2015) lakini wakashindwa kupata/kutenga bajeti ya Tzs. million 50 kulipa mawakala elfu 5 kusimamia kura za mgombea urais wao? Hawa jamaa hopeless kabisa. Mwenyekiti na sekretariat wao ni dili tu kila mahali, basi. Kwenye kukodisha choppa (hakuna accountability) kulikuwa na dili; bajeti ilipatikana, lakini kwenye kuwalipa mawakala (obvious accountability) bajeti hakuna! Halafu hao uwakabidhi dola, watakomba hadi nywele za VIKONGWE
 
Nadhani kuna tahadhari zilichukuliwa(ndo maana wakagunduwa kufuatiliwa mara kwa mara),however haikuhusisha security detail. Pia inaonyesha washambuliaji walifahamu kuwa mshambuliwaji asingekuwa na wasiwasi mwingi Dodoma ambapo ulinzi na usalama pengine ni wa juu zaidi kutokana na idadi za viongozi wanaokuwepo huko. Tena jirani na nyumba ya spika? Mtu wa tatu ama wa nne ki madaraka kama sikosei baada ya rais, na makamu wake?

Just my take.

However nakubaliana na hilo la chadema kutoa ulinzi.
 
..hili la ulinzi wa viongozi makini kama Lissu chadema ni la msingi mno....Na kweli chadema kwa hili walichemka mno....mi nlijua wanawatumia wale vijana wao wa red brigade...nashangaa Lissu hakuwa na ulinzi pamoja na kulalamika...

..kama watu kama kina gwajima wana security protocol za kufa mtu...sioni kwanini chadema wasifanye hivyo...ni uzembe kutegemea ulinzi wa serikali inayowaadhibu....badilikeni hakika....




 
Back
Top Bottom