Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,209
Title ya thread yangu inaweza kunifanya nionekana masalia au buku saba group lakini si hivyo, mimi ni mwanachadema hai mwenye mapenzi ya dhati kabisa kwa chama changu na hili natoa kama angalizo kwa kuzingatia historia.
Kwa kawaida vyama vya upinzani hupata umaarufu mkubwa sana kutokana na utawala mbaya wa vyama tawala. Hapa nchini kwetu tayari tuna uzoefu wa nguvu ya NCCR mageuzi mwaka 1995 wakati nchi ilipokuwa chini ya utawala mbovu wa Ali Hassani Mwinyi. Katika utawala wa Mwinyi, nchi ilikuwa haina mwenyewe. Nchi ilikuwa inanuka rushwa, kazi zilikuwa hazilipi, ujambazi na mauaji ya kutisha vilikuwa ni vitu vya kawaida kabisa. Wakati huu Mrema alipata umaarufu wa kutisha, akaonekana ni chaguo na kimbilio la wale wasio na mtetezi. Kwa bahati mbaya wanyonge wakashindwa, wenye nazo wakashinda. Mkapa akaingia madarakani. Akaanza kurekebisha mambo, na kuirudisha nchi kwenye mstari. Ndani ya miaka mitano ya awali, watu wakajenga imani kubwa kwake, term ya pili ya uchaguzi mwaka 2000, Mkapa akapata ongezeko la kura kwa asilimia kumi ukilinganisha na zile za mwaka 1995. Watu wakarudisha imani kubwa kwa CCM. Kiasi cha kwamba ulipokuja uchaguzi wa mwaka 2005, hakuna aliyekuwa anawataka wapinzani. Watu walijiaminisha kwamba CCM yatosha. Kikwete akaingia madarakani kwa ushindi wa zaidi ya asilimia 80.
Hivi sasa Kikwete kavurugavuruga mambo, nchi ipoipo tu kama isiyo na mwenyewe. Inakwenda tu kama ndege isiyo na rubani. Hali ya maisha imezidi kuwa ngumu, mfumko wa bei umeongezeka mara dufu huku njia halali za utafutaji hela zikizidi kufungwa. Kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi ambapo watu walitozwa hadi kodi za baiskeli, hali inajirudia tena hivi sasa kwenye utawala wa Kikwete, watu sasa wanatozwa hadi kodi ya laini ya simu. Kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi ambapo wenye nacho walizidi kuwa nacho wakawepo matajiri wa kutisha na masikini wanaotia huruma hali ndiyo ilivyo wakati wa Kikwete. Kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi, wakati ambao ilikuwa ukilala hadi asubuhi na kuamka salama unamshukuru Mungu kwamba majambazi hawakupita kwako siku hiyo, ndivyo hali ilivyo sasa.
Watu wamejaribu kuonyesha hasira zao kwenye sanduku la kura mwaka 2010, ambapo kura zilishuka kwa karibu asilimia 20. Lakini hiyo haijatosha. Hali ya maisha imezidi kuwa mbaya na yenye kukatisha tamaa. Polisi wameacha kufanya kazi ya kushughulika na wahalifu na kuwalinda watu na mali zao, hivi sasa wanafanya kazi ya kubambikia watu kesi, wanaua na kuwashitaki watu wasio na hatia. Haya mambo yanawachosha na kuwakatisha tamaa sana wananchi dhidi ya CCM. Watu hivi sasa wanaichukia CCM kwa dhati, kiasi cha kwamba kama ambavyo Mrema alionekana kuwa mkombozi wa wanyonge kwa wakati ule, ndivyo ambavyo CHADEMA inaonekana kuwa ndiyo mkombozi wa hali za maisha ya sasa ya watanzania.
Watanzania wanaiona CHADEMA kama chama chenye uwezo wa kubadilisha hali ya mambo nchini kwa kuwa chama tawala kimekuwa chama mfu. Kimeiacha nchi iende kama ndege isiyo na rubani au meli isiyo na nahodha. Nchi inasombwa na mawimbi ya ujambazi, ufisadi, mauaji ya kutisha na umasikini mkubwa huku waliopewa mamlaka ya kuinusuru wakiwa wapo busy na mambo yao. Katika mazingira haya wananchi wataipa kura CHADEMA.
Huu ni wakati mhimu kwa CHADEMA kuchanga karata zao vema, wakishindwa tu kufanya hivyo, CCM inaweza kupata Rais makini mwaka 2015, na watu wakarudisha tena matumaini kwa CCM. Na ikifikia hatua hiyo, basi CHADEMA inaweza kuanza kupotea katika ramani ya siasa za Tanzania kama vile ambavyo NCCR na CUF vilipotea. Maana kitakachotokea hivi sasa ni kwamba CHADEMA itazoa kura nyingi sana 2015, lakini kisiposhinda akaingia Rais makini kutoka CCM, wananchi wakamwamini, inamaana mwaka 2020 wananchi wataipigia kura nyingi CCM na kuinyima kura CHADEMA. Na hivyo itawezekana kwa kuwa CHADEMA kitakuwa hakina serikali katika muda wa miaka mitano na hivyo kutokuwa na impact kubwa kama ambavyo chama tawala kitakuwa nayo chini ya Rais makini atakayeingia wakati huo.
Tufanye kazi usiku na mchana wanachadema wenzangu. Napendekeza tuanzishe vyombo vyetu vya habari vitakavyosaidia kukiuza chama. Ndani ya hii miaka miwili ya utawala dhaifu uliopo madarakani, tufanikiwe kuteka nyoyo za watanzania. Kwa hakika tutashinda. Failure of that, tuandike maumivu. Naamini CCM watamleta mtu wa tofauti, asiyetajwa tajwa kama alivyoletwa Mkapa, ili kuiokoa nchi na chama pia. Kwa sasa nchi ilipo si salama kabisa. Tunamuomba sana Mungu atusaidie tufike salama 2015. Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki CHADEMA.
Kwa kawaida vyama vya upinzani hupata umaarufu mkubwa sana kutokana na utawala mbaya wa vyama tawala. Hapa nchini kwetu tayari tuna uzoefu wa nguvu ya NCCR mageuzi mwaka 1995 wakati nchi ilipokuwa chini ya utawala mbovu wa Ali Hassani Mwinyi. Katika utawala wa Mwinyi, nchi ilikuwa haina mwenyewe. Nchi ilikuwa inanuka rushwa, kazi zilikuwa hazilipi, ujambazi na mauaji ya kutisha vilikuwa ni vitu vya kawaida kabisa. Wakati huu Mrema alipata umaarufu wa kutisha, akaonekana ni chaguo na kimbilio la wale wasio na mtetezi. Kwa bahati mbaya wanyonge wakashindwa, wenye nazo wakashinda. Mkapa akaingia madarakani. Akaanza kurekebisha mambo, na kuirudisha nchi kwenye mstari. Ndani ya miaka mitano ya awali, watu wakajenga imani kubwa kwake, term ya pili ya uchaguzi mwaka 2000, Mkapa akapata ongezeko la kura kwa asilimia kumi ukilinganisha na zile za mwaka 1995. Watu wakarudisha imani kubwa kwa CCM. Kiasi cha kwamba ulipokuja uchaguzi wa mwaka 2005, hakuna aliyekuwa anawataka wapinzani. Watu walijiaminisha kwamba CCM yatosha. Kikwete akaingia madarakani kwa ushindi wa zaidi ya asilimia 80.
Hivi sasa Kikwete kavurugavuruga mambo, nchi ipoipo tu kama isiyo na mwenyewe. Inakwenda tu kama ndege isiyo na rubani. Hali ya maisha imezidi kuwa ngumu, mfumko wa bei umeongezeka mara dufu huku njia halali za utafutaji hela zikizidi kufungwa. Kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi ambapo watu walitozwa hadi kodi za baiskeli, hali inajirudia tena hivi sasa kwenye utawala wa Kikwete, watu sasa wanatozwa hadi kodi ya laini ya simu. Kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi ambapo wenye nacho walizidi kuwa nacho wakawepo matajiri wa kutisha na masikini wanaotia huruma hali ndiyo ilivyo wakati wa Kikwete. Kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi, wakati ambao ilikuwa ukilala hadi asubuhi na kuamka salama unamshukuru Mungu kwamba majambazi hawakupita kwako siku hiyo, ndivyo hali ilivyo sasa.
Watu wamejaribu kuonyesha hasira zao kwenye sanduku la kura mwaka 2010, ambapo kura zilishuka kwa karibu asilimia 20. Lakini hiyo haijatosha. Hali ya maisha imezidi kuwa mbaya na yenye kukatisha tamaa. Polisi wameacha kufanya kazi ya kushughulika na wahalifu na kuwalinda watu na mali zao, hivi sasa wanafanya kazi ya kubambikia watu kesi, wanaua na kuwashitaki watu wasio na hatia. Haya mambo yanawachosha na kuwakatisha tamaa sana wananchi dhidi ya CCM. Watu hivi sasa wanaichukia CCM kwa dhati, kiasi cha kwamba kama ambavyo Mrema alionekana kuwa mkombozi wa wanyonge kwa wakati ule, ndivyo ambavyo CHADEMA inaonekana kuwa ndiyo mkombozi wa hali za maisha ya sasa ya watanzania.
Watanzania wanaiona CHADEMA kama chama chenye uwezo wa kubadilisha hali ya mambo nchini kwa kuwa chama tawala kimekuwa chama mfu. Kimeiacha nchi iende kama ndege isiyo na rubani au meli isiyo na nahodha. Nchi inasombwa na mawimbi ya ujambazi, ufisadi, mauaji ya kutisha na umasikini mkubwa huku waliopewa mamlaka ya kuinusuru wakiwa wapo busy na mambo yao. Katika mazingira haya wananchi wataipa kura CHADEMA.
Huu ni wakati mhimu kwa CHADEMA kuchanga karata zao vema, wakishindwa tu kufanya hivyo, CCM inaweza kupata Rais makini mwaka 2015, na watu wakarudisha tena matumaini kwa CCM. Na ikifikia hatua hiyo, basi CHADEMA inaweza kuanza kupotea katika ramani ya siasa za Tanzania kama vile ambavyo NCCR na CUF vilipotea. Maana kitakachotokea hivi sasa ni kwamba CHADEMA itazoa kura nyingi sana 2015, lakini kisiposhinda akaingia Rais makini kutoka CCM, wananchi wakamwamini, inamaana mwaka 2020 wananchi wataipigia kura nyingi CCM na kuinyima kura CHADEMA. Na hivyo itawezekana kwa kuwa CHADEMA kitakuwa hakina serikali katika muda wa miaka mitano na hivyo kutokuwa na impact kubwa kama ambavyo chama tawala kitakuwa nayo chini ya Rais makini atakayeingia wakati huo.
Tufanye kazi usiku na mchana wanachadema wenzangu. Napendekeza tuanzishe vyombo vyetu vya habari vitakavyosaidia kukiuza chama. Ndani ya hii miaka miwili ya utawala dhaifu uliopo madarakani, tufanikiwe kuteka nyoyo za watanzania. Kwa hakika tutashinda. Failure of that, tuandike maumivu. Naamini CCM watamleta mtu wa tofauti, asiyetajwa tajwa kama alivyoletwa Mkapa, ili kuiokoa nchi na chama pia. Kwa sasa nchi ilipo si salama kabisa. Tunamuomba sana Mungu atusaidie tufike salama 2015. Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki CHADEMA.