Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 44
na Francis Godwin, Iringa
ZIKIWA zimepita siku chache tangu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kuifuta mahakamani kesi ya Diwani wa Kata ya Itunundu-Pawaga, Philipo Mkumbata, aliyekuwa akituhumiwa kuhujumu miundombinu, kwa madai kuwa kumfikisha mahakamani diwani huyo ni kuwapa nguvu wapinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kimeonyesha kulipinga agizo hilo kwa kumtaka kulifuta.
Akitoa tamko hilo kwa waandishi wa habari, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Iringa, Mwigongo Kapwani na Katibu Pascal Bella, walisema wamepokea kwa masikitiko makubwa agizo hilo la Waziri Mkuu na kuweka bayana kuwa jambo hilo ni kuingilia uhuru wa mahakama.
Kapwani alisema wanaamini kuwa katika kushughulikia suala hilo Waziri Mkuu amedanganywa na baadhi ya watendaji waliokuwa na malengo ya kisiasa zaidi lakini pia agizo hilo limemdhalilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kwa kumfanya aonekane kiongozi asiye na mamlaka baada ya kuruhusu diwani huyo afikishwe mbele ya sheria.
CHADEMA inaamini kuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho cha kutafsiri sheria na kwamba hakipaswi kuingiliwa utendaji wake kwa misingi ya ushabiki wa kisiasa, na kwamba diwani huyo ni mhalifu kama wahalifu wengine, hivyo Pinda hakupaswa kumtetea bali alitakiwa kuacha sheria ifanye kazi yake, alisema Kapwani.
Kapwani alisema kuwa Waziri Pinda anataka kutoa tafsiri mbaya kwa wananchi ambao walianza kuwa na imani kubwa na utendaji kazi wake katika kushughulikia masuala mbali mbali ya nchi bila ubaguzi, ila kwa picha aliyoionyesha Iringa imemvurugia imani hiyo iliyoanza kujengeka.
Hata hivyo alisema kuwa bado Pinda ana nafasi kubwa ya kubatilisha uamuzi wake, kwa sababu suala lolote lililopo mahakamani halipaswi kuongelewa au kutolewa uamuzi nje ya mahakama.
CHADEMA tunataka kesi hiyo namba 335/2008 iendelee kama ilivyoanzwa kusikilizwa na kwa sababu mali iliyoharibiwa ni ya Watanzania wote na si mali ya CCM, alisema Kapwani.
Naye Katibu Pascal Bella, alisema wana tuhuma nyingi za diwani huyo na wapo tayari kuzitoa na hapaswi kupewa msamaha na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kama inavyofanyika hivi sasa.
Bella alisema wapo tayari kuwasiliana na uongozi wa taifa wa CHADEMA ili kuhakikisha suala hilo linakwenda kwa misingi ya sheria na kuondokana na mizengwe iliyoanzwa kufanywa hivi sasa kwa lengo la kupindisha sheria ili kulifanya liwe la kisiasa.
Alisema ni vema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akawa makini zaidi na matamshi yake anapofanya ziara mikoani ili kauli zake zisije zikamsababishia matatizo mbele ya jamii ambayo ina imani na utendaji wa kiongozi huyo.
ZIKIWA zimepita siku chache tangu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kuifuta mahakamani kesi ya Diwani wa Kata ya Itunundu-Pawaga, Philipo Mkumbata, aliyekuwa akituhumiwa kuhujumu miundombinu, kwa madai kuwa kumfikisha mahakamani diwani huyo ni kuwapa nguvu wapinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kimeonyesha kulipinga agizo hilo kwa kumtaka kulifuta.
Akitoa tamko hilo kwa waandishi wa habari, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Iringa, Mwigongo Kapwani na Katibu Pascal Bella, walisema wamepokea kwa masikitiko makubwa agizo hilo la Waziri Mkuu na kuweka bayana kuwa jambo hilo ni kuingilia uhuru wa mahakama.
Kapwani alisema wanaamini kuwa katika kushughulikia suala hilo Waziri Mkuu amedanganywa na baadhi ya watendaji waliokuwa na malengo ya kisiasa zaidi lakini pia agizo hilo limemdhalilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kwa kumfanya aonekane kiongozi asiye na mamlaka baada ya kuruhusu diwani huyo afikishwe mbele ya sheria.
CHADEMA inaamini kuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho cha kutafsiri sheria na kwamba hakipaswi kuingiliwa utendaji wake kwa misingi ya ushabiki wa kisiasa, na kwamba diwani huyo ni mhalifu kama wahalifu wengine, hivyo Pinda hakupaswa kumtetea bali alitakiwa kuacha sheria ifanye kazi yake, alisema Kapwani.
Kapwani alisema kuwa Waziri Pinda anataka kutoa tafsiri mbaya kwa wananchi ambao walianza kuwa na imani kubwa na utendaji kazi wake katika kushughulikia masuala mbali mbali ya nchi bila ubaguzi, ila kwa picha aliyoionyesha Iringa imemvurugia imani hiyo iliyoanza kujengeka.
Hata hivyo alisema kuwa bado Pinda ana nafasi kubwa ya kubatilisha uamuzi wake, kwa sababu suala lolote lililopo mahakamani halipaswi kuongelewa au kutolewa uamuzi nje ya mahakama.
CHADEMA tunataka kesi hiyo namba 335/2008 iendelee kama ilivyoanzwa kusikilizwa na kwa sababu mali iliyoharibiwa ni ya Watanzania wote na si mali ya CCM, alisema Kapwani.
Naye Katibu Pascal Bella, alisema wana tuhuma nyingi za diwani huyo na wapo tayari kuzitoa na hapaswi kupewa msamaha na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kama inavyofanyika hivi sasa.
Bella alisema wapo tayari kuwasiliana na uongozi wa taifa wa CHADEMA ili kuhakikisha suala hilo linakwenda kwa misingi ya sheria na kuondokana na mizengwe iliyoanzwa kufanywa hivi sasa kwa lengo la kupindisha sheria ili kulifanya liwe la kisiasa.
Alisema ni vema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akawa makini zaidi na matamshi yake anapofanya ziara mikoani ili kauli zake zisije zikamsababishia matatizo mbele ya jamii ambayo ina imani na utendaji wa kiongozi huyo.