CHADEMA Iringa wamjia juu Pinda

Asha Abdala

JF-Expert Member
Mar 21, 2007
1,130
44
na Francis Godwin, Iringa




ZIKIWA zimepita siku chache tangu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kuifuta mahakamani kesi ya Diwani wa Kata ya Itunundu-Pawaga, Philipo Mkumbata, aliyekuwa akituhumiwa kuhujumu miundombinu, kwa madai kuwa kumfikisha mahakamani diwani huyo ni kuwapa nguvu wapinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kimeonyesha kulipinga agizo hilo kwa kumtaka kulifuta.

Akitoa tamko hilo kwa waandishi wa habari, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Iringa, Mwigongo Kapwani na Katibu Pascal Bella, walisema wamepokea kwa masikitiko makubwa agizo hilo la Waziri Mkuu na kuweka bayana kuwa jambo hilo ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Kapwani alisema wanaamini kuwa katika kushughulikia suala hilo Waziri Mkuu amedanganywa na baadhi ya watendaji waliokuwa na malengo ya kisiasa zaidi lakini pia agizo hilo limemdhalilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kwa kumfanya aonekane kiongozi asiye na mamlaka baada ya kuruhusu diwani huyo afikishwe mbele ya sheria.

“CHADEMA inaamini kuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho cha kutafsiri sheria na kwamba hakipaswi kuingiliwa utendaji wake kwa misingi ya ushabiki wa kisiasa, na kwamba diwani huyo ni mhalifu kama wahalifu wengine, hivyo Pinda hakupaswa kumtetea bali alitakiwa kuacha sheria ifanye kazi yake,” alisema Kapwani.

Kapwani alisema kuwa Waziri Pinda anataka kutoa tafsiri mbaya kwa wananchi ambao walianza kuwa na imani kubwa na utendaji kazi wake katika kushughulikia masuala mbali mbali ya nchi bila ubaguzi, ila kwa picha aliyoionyesha Iringa imemvurugia imani hiyo iliyoanza kujengeka.

Hata hivyo alisema kuwa bado Pinda ana nafasi kubwa ya kubatilisha uamuzi wake, kwa sababu suala lolote lililopo mahakamani halipaswi kuongelewa au kutolewa uamuzi nje ya mahakama.

“CHADEMA tunataka kesi hiyo namba 335/2008 iendelee kama ilivyoanzwa kusikilizwa na kwa sababu mali iliyoharibiwa ni ya Watanzania wote na si mali ya CCM,” alisema Kapwani.

Naye Katibu Pascal Bella, alisema wana tuhuma nyingi za diwani huyo na wapo tayari kuzitoa na hapaswi kupewa msamaha na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kama inavyofanyika hivi sasa.

Bella alisema wapo tayari kuwasiliana na uongozi wa taifa wa CHADEMA ili kuhakikisha suala hilo linakwenda kwa misingi ya sheria na kuondokana na mizengwe iliyoanzwa kufanywa hivi sasa kwa lengo la kupindisha sheria ili kulifanya liwe la kisiasa.

Alisema ni vema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akawa makini zaidi na matamshi yake anapofanya ziara mikoani ili kauli zake zisije zikamsababishia matatizo mbele ya jamii ambayo ina imani na utendaji wa kiongozi huyo.
 
Nyie CHADEMA mna nini na Pinda? Kila siku kumfuata fuata kuhusu kauli zake. Mara maalbino. Mshindwe na mlegee, Pinda ni waziri mkuu anayefuata misingi ya Nyerere. Pinda ni kama Sokoine

.....ndiyohiyo
 
“CHADEMA inaamini kuwa mahakama ndicho chombo cha mwisho cha kutafsiri sheria na kwamba hakipaswi kuingiliwa utendaji wake kwa misingi ya ushabiki wa kisiasa, na kwamba diwani huyo ni mhalifu kama wahalifu wengine, hivyo Pinda hakupaswa kumtetea bali alitakiwa kuacha sheria ifanye kazi yake,” alisema Kapwani.
CHADEMA nao hawakuwa makini katika kemeo lao hili, upinzani nchini kwetu kwa kweli umechoka. Pinda hakuingilia "tafsiri za sheria" za mahakama. Pinda hakuagiza hakimu aseme mtuhumiwa hakuvunja sheria. Ameagiza kesi iondolewe mahakamani. Ukigombana na ndugu yako halafu baba yenu akamwagiza mmoja akafute kesi mliyofunguliana mahakamani huyo mzazi atakuwa hajaingilia mahakama, ila ameingilia ugomvi wa hawa ndugu kwa kuwaagiza wakaondoe kesi mahakamani, isipokuwa kama Baba yao amemwagiza hakimu afute kesi.

Tatizo hapa, kosa la Pinda, ni kuonyesha kwamba hajali vitendo vya jinai iwapo vimetendwa na CCM mwenzake. Hajali uhujumu na uharamia wa mali ya umma, kwamba wavunja sheria wa CCM wasipelekwe mbele ya sheria. Hiyo sio "kuingilia utendaji...tafsiri ya sheria."

Upinzani wetu unalegalega kwa sababu wanashindwa kuelezea udhaifu wa CCM wakaeleweka na wananchi.
 
CHADEMA nao hawakuwa makini katika kemeo lao hili, upinzani nchini kwetu kwa kweli umechoka. Pinda hakuingilia "tafsiri za sheria" za mahakama. Pinda hakuagiza hakimu aseme mtuhumiwa hakuvunja sheria. Ameagiza kesi iondolewe mahakamani. Ukigombana na ndugu yako halafu baba yenu akamwagiza mmoja akafute kesi mliyofunguliana mahakamani huyo mzazi atakuwa hajaingilia mahakama, ila ameingilia ugomvi wa hawa ndugu kwa kuwaagiza wakaondoe kesi mahakamani, isipokuwa kama Baba yao amemwagiza hakimu afute kesi.

Tatizo hapa, kosa la Pinda, ni kuonyesha kwamba hajali vitendo vya jinai iwapo vimetendwa na CCM mwenzake. Hajali uhujumu na uharamia wa mali ya umma, kwamba wavunja sheria wa CCM wasipelekwe mbele ya sheria. Hiyo sio "kuingilia utendaji...tafsiri ya sheria."

Upinzani wetu unalegalega kwa sababu wanashindwa kuelezea udhaifu wa CCM wakaeleweka na wananchi.

Na wewe una statement kama za hao SISI Mafisadi. Umeanza maelezo yako vizuri tena ukiwa unaeleweka. Lakini hayo maandishi mekundu yamekuangusha kabisa kwa sababu husemi ukweli kwa kauli hiyo. Yamenitia kinyaa maana naweza tapika.
 
Nyie CHADEMA mna nini na Pinda? Kila siku kumfuata fuata kuhusu kauli zake. Mara maalbino. Mshindwe na mlegee, Pinda ni waziri mkuu anayefuata misingi ya Nyerere. Pinda ni kama Sokoine

.....ndiyohiyo


Pinda naona kama anachemka maana anadhani mali ni ya CCM kumbe ni mali ya wananchi .Huyo ni diwani wa watanzania wa eneo hilo kwa ticket ya CCM na si Diwani wa wana CCM pekee hadi aingiwe na hofu .Misingi ya mwalimu hapa ni ipi ?
 
Mkuu Asha,
Mimi bado ni kihiyo wa computer,naomba uweke pia maoni ya wasomaji yaliyopo chini ya habari hiyo kuongeza utamu wa mjadala huu.
 
habarindiyohiyo sijaelewa unachosema.PM anapokuwa anaongeaongea na kutoa maagizo yasiyo na mantinki i doubt about his capacity in making judgements before he spoke things
 
na Francis Godwin, Iringa




ZIKIWA zimepita siku chache tangu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kuifuta mahakamani kesi ya Diwani wa Kata ya Itunundu-Pawaga, Philipo Mkumbata, aliyekuwa akituhumiwa kuhujumu miundombinu, kwa madai kuwa kumfikisha mahakamani diwani huyo ni kuwapa nguvu wapinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kimeonyesha kulipinga agizo hilo kwa kumtaka kulifuta.
Haya hapo juu yalikuwa matamshi au kulikuwa na barua? Hapa JF.....?

Kapwani alisema wanaamini kuwa katika kushughulikia suala hilo Waziri Mkuu amedanganywa na baadhi ya watendaji waliokuwa na malengo ya kisiasa zaidi lakini pia agizo hilo limemdhalilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Said, kwa kumfanya aonekane kiongozi asiye na mamlaka baada ya kuruhusu diwani huyo afikishwe mbele ya sheria
.

Halafu hapa upinzani na una sua sua, wanaamini Waziri Mkuu mwenyewe hawezi kutoa maamuzi hayo bila kudanganywa:eek:

Sio jambo baya lakini linadhalilisha?



Hata hivyo alisema kuwa bado Pinda ana nafasi kubwa ya kubatilisha uamuzi wake, kwa sababu suala lolote lililopo mahakamani halipaswi kuongelewa au kutolewa uamuzi nje ya mahakama.

“CHADEMA tunataka kesi hiyo namba 335/2008 iendelee kama ilivyoanzwa kusikilizwa na kwa sababu mali iliyoharibiwa ni ya Watanzania wote na si mali ya CCM,” alisema Kapwani.

Siasa hizo hapo juu!

Naye Katibu Pascal Bella, alisema wana tuhuma nyingi za diwani huyo na wapo tayari kuzitoa na hapaswi kupewa msamaha na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kama inavyofanyika hivi sasa.

Nafikiri ingekuwa hivyo "kapewa msamaha" basi lazima awe amehukumiwa? au?

Kali nyingine hapo chini...mie mbavu sina...

Bella alisema wapo tayari kuwasiliana na uongozi wa taifa wa CHADEMA ili kuhakikisha suala hilo linakwenda kwa misingi ya sheria na kuondokana na mizengwe iliyoanzwa kufanywa hivi sasa kwa lengo la kupindisha sheria ili kulifanya liwe la kisiasa.:D


Alisema ni vema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akawa makini zaidi na matamshi yake anapofanya ziara mikoani ili kauli zake zisije zikamsababishia matatizo mbele ya jamii ambayo ina imani na utendaji wa kiongozi huyo.

Pale pale pa mwanzo Kwahiyo ina maana alitoa matamshi na hayaja tekelezeka?

Maoni yangu hii ita unfold kidogo...labda kuna mengine, only time will tell.

Na kama hayo yametekelezeka basi Waziri Mkuu ni cheo kizuri sana:D Yaani kama Yule jamaa anayeonekana nakutokuonekana (Invisible)akiamua anawadhalilisha ma mods wake halafu anawarudisha wale wanaopayuka!(Walio kuwa banned) Wapayukaji!

Kwa kweli Mh. Pinda atakuwa ndie yule tu wa kupindisha pindisha sheria!:D
 
Back
Top Bottom