CHADEMA 'imelidanganya Bunge'

CHADEMA 'imelidanganya Bunge'

Sasa nani atatuongelea ukweli ikiwa hadi upinzani nao unathubutu kusema uongo. Mungu tusaidie na balaa la wanasiasa waongo.
 
hii kampuni wanalitakiwa kukanusha kama hawajazoa ardhi kifisadi na kuwaacha wananchi watu,
iweje wao wanaona ni muhimu kumtetea JEET ambaye wanadai sio mmiliki wa kampuni?

yeye JEET ana wasemaji? kama wao wamekuja hadharani la kumiliki ardhi ni muhimu zaidi wangeongelea hiyo kwanza maana suhala kuu hapa ni hiyo kampuni kujichotea ardhi, hiyo patel anaweza kuikana hiyo kampuni kwa sababu imechafuka
 
Sasa nani atatuongelea ukweli ikiwa hadi upinzani nao unathubutu kusema uongo. Mungu tusaidie na balaa la wanasiasa waongo.

wewe la muhimu kwako ni lipi? kampuni kujichotea ardhi au umiliki wake? kama wamesema ukweli kwamba hiyo kampuni imechota ardhi hayo ya mmiliki ni nyongeza, Patel analo hata yakana yote
 
Ni kama ambavyo Rostam Azziz anavyomiliki makampuni zaidi ya kumi
lakini hakuna jina lake kwenye kampuni hizo, ndivyo ilivyo kwa Jeetu Patel
kuwa mmiliki kwenye kampuni hiyo bila kuwemo jina lake.
Kwani unafikiri janja yao haijulikani? Sidhani kama Chadema watakuwa
wamekurupuka kwa vyovyote wana evidence. Wapeleke kesi mahakamani
kama wanadhani wameonewa...
Kijana ukiitwa mahakamani utaweza kuithibitisha unachokisema JF, sio sehemu ya porojo
 
Always CHADEMA wanapotoa jambo wanakuwa na ushaidi wa kutosha....sio wazururaji...CDM LONG LIVE.
 
Huo muda walioutumia kuutangazia umma kuwa CDM wamedanganya wangetumia kwenda mahakani ili kuto somo/////////
 
Sasa nani atatuongelea ukweli ikiwa hadi upinzani nao unathubutu kusema uongo. Mungu tusaidie na balaa la wanasiasa waongo.
Kampuni ngapi umiliki wake ni wa siri? Nani asiyejua Kagoda inahusishwa na Rostam Aziz wakati jina lake halionekani mahali popote? Suala muhimu hapa kwa mkanushaji ilikuwa suala la umiliki wa ardhi ambalo hajaliongelea zaidi ya kumkingia kifua Jeetu Patel, Mwita zinduka hakuna wa kuzuia upepo unapovuma na hiki ndicho kinachoitesa ccm
 
Issue kubwa ni wananchi kunyang'anywa ardhi yao na kupewa walowezi. Umiliki ni maboresho tu ya taarifa.
 
Hata mmiliki wa Sea Cliff ukumtaja ataruka japo tunamjua.....na ilithibitika siku ilipoungua (au kuchomwa)....entourage iliyoenda pale mpaka makamu wa rais alikuwepo:

"We will be back. It will be bigger and better. We are yet to establish the extent of damage and loss but initial estimates are in billions of shillings," explained Patel.

He made the comments shortly after the Vice President, Dr Ali Mohamed Shein, toured the wreckage at what remains of the famed tourist hotel at Masaki Peninsula in Dar es Salaam.

Kinondoni Regional Commander (RPC), Mr Jamal Rwambow, who has been at the scene since the fire broke out, and the hotel's General Manager, Mr Kelvin Stender, could not establish cause of the fire.
 
Au Riz1 anavyomiliki mali kwa kutumia migingo ya watu kama ASAAS wa Iringa

ASAS ya Iring ilikuwepo kabla Ridhwan hajazaliwa, wacha kudanganya watu. Hao wenye ASAS tunawajua sana tena sana. Hao ni kina Bin Abri wa Iringa, ni matajiri wa huko kabla ya Nyerere kuwa Rais na hata wakati wake walikuwepo.

Na licha ya ASAS wana kampuni nyingine inaitwa Bin Abri Transport, kama wewe huwajui muulize baba'ko anaweza kuwajuwa kwani ni wa zamani sana hawa. Wacha uongo.

Ndio nyinyi mnawapoteza ma boss wenu halafu wanaenda kusema uongo bungeni!
 
ASAS ya Iring ilikuwepo kabla Ridhwan hajazaliwa, wacha kudanganya watu. Hao wenye ASAS tunawajua sana tena sana. Hao ni kina Bin Abri wa Iringa, ni matajiri wa huko kabla ya Nyerere kuwa Rais na hata wakati wake walikuwepo na licha ya ASAS wana kampuni nyingine inaitwa Bin Abri Transport. Kama wewe huwajui muulize baba'ko anaweza kuwajuwa kwani ni wa zamani sana hawa. Wacha uongo.

Ndio nyinyi mnawapoteza ma boss wenu halafu wanaenda kusema uongo bungeni!

Kumbe hujui kuwa biashara pia huuzwa kama nazi!......Kilimanjaro hoteli pia ilikuwapo mhata kabla ya mmiliki wake wa sasa kuzaliwa
 
Kumbe hujui kuwa biashara pia huuzwa kama nazi!......Kilimanjaro hoteli pia ilikuwapo mhata kabla ya mmiliki wake wa sasa kuzaliwa

Wacha uongo! wamiliki ndio walewale na haijauzwa hata siku moja.

Kilimanjaro Hotel ilikuwa ya "umma" na kama vilivyokufa 98% ya vilivyokuwa vya umma ndivyo ilivyokufa Kilimanjaro Hotel na ikatangazwa rasmi kutafuta atakae weza kuiendesha. Akatokea Mwarabu akajishindia tenda na unaiona sasa inavyopendeza? Na hiyo ASAS ni waarabu hao.
 
Kilimanjaro hotel si nasika ya Mengi

Hapana si ya Mengi. Alisindwa kwenye zabuni akawapeleka walioshinda mahakamani eti kwa kuwa sio wazawa. Mahakamani akashindwa kuwa hata kama ni mzawa lakini hukukidhi vigezo. Uchungu wake mpaka leo haingii Kempinski, anaona haya.
 
hii kampuni wanalitakiwa kukanusha kama hawajazoa ardhi kifisadi na kuwaacha wananchi watu,
iweje wao wanaona ni muhimu kumtetea JEET ambaye wanadai sio mmiliki wa kampuni?

yeye JEET ana wasemaji? kama wao wamekuja hadharani la kumiliki ardhi ni muhimu zaidi wangeongelea hiyo kwanza maana suhala kuu hapa ni hiyo kampuni kujichotea ardhi, hiyo patel anaweza kuikana hiyo kampuni kwa sababu imechafuka

Ujinga huo. Wao wanasema Jeetu sio kampuni yake, wewe kama una ushahidi weka hapa. Jeetu ajitetee nini na kupayuka mnapayuka nyinyi? ukimtuhumu mtu, ni wewe unaetakiwa ulete ushahidi si unaemtuhumu.
 
Hapana si ya Mengi. Alisindwa kwenye zabuni akawapeleka walioshinda mahakamani eti kwa kuwa sio wazawa. Mahakamani akashindwa kuwa hata kama ni mzawa lakini hukukidhi vigezo. Uchungu wake mpaka leo haingii Kempinski, anaona haya.
Nimekumbuka alishindwa bei mpaka leo aongei na Masilingi.
Ndio anadai alisababisha kuikosa hiyo hotel
 
rais mwenyewe kadanganywa ,soma magazeti ya leo.nchi ya uongo inawatu waongo wanaozungumza uongo tuuuuuuuu
 
Kijana ukiitwa mahakamani utaweza kuithibitisha unachokisema JF, sio sehemu ya porojo

...fisadi gani atajaribu kumpeleka mtu mahakamani? kawaulize karamagi, Mkono, na Mgonja wakumegee siri kwa nini hawakumpeleka Dr Slaa mahakamani alipowataja hadharani kuwa ni mafisadi, pamoja na mikwara yote waliyoitoa na nguvu kubwa ya pesa waliyonayo.

Kumbuka Kubenea alitaja majina kibao ya Rostam yenyetofauti za spelling mojamoja tu. e.g. Rustam, Rastam, Azziz, Aziz nk, kwenye makampuni kadhaa. hadi leo Rostam kala jiwe hathubutu kisogelea mahakama.
 
ASAS ya Iring ilikuwepo kabla Ridhwan hajazaliwa, wacha kudanganya watu. Hao wenye ASAS tunawajua sana tena sana. Hao ni kina Bin Abri wa Iringa, ni matajiri wa huko kabla ya Nyerere kuwa Rais na hata wakati wake walikuwepo na licha ya ASAS wana kampuni nyingine inaitwa Bin Abri Transport. Kama wewe huwajui muulize baba'ko anaweza kuwajuwa kwani ni wa zamani sana hawa. Wacha uongo.

Ndio nyinyi mnawapoteza ma boss wenu halafu wanaenda kusema uongo bungeni!

We Zoba, hata NBC ilikuwepo kabla hujazaliwa lakini leo ni ya wa South. makampuni mengi tu yalikuwepo tangu zamani lakini leo mafisadi wameingia na wanyatumia kukamua wanaTZ. tafuta hoja nyingine lakini sio uzamani wa kampuni kufanya ndio kificho cha ufisadi wenu
 
...fisadi gani atajaribu kumpeleka mtu mahakamani? kawaulize karamagi, Mkono, na Mgonja wakumegee siri kwa nini hawakumpeleka Dr Slaa mahakamani alipowataja hadharani kuwa ni mafisadi, pamoja na mikwara yote waliyoitoa na nguvu kubwa ya pesa waliyonayo. <br />
Kumbuka Kubenea alitaja majina kibao ya Rostam yenyetofauti za spelling mojamoja tu. e.g. Rustam, Rastam, Azziz, Aziz nk, kwenye makampuni kadhaa. hadi leo Rostam kala jiwe hathubutu kisogelea mahakama.
Naomba unitajie makampuni matano ya Rostam hata ukiitwa mahakamani unaweza kuyataja
 
Back
Top Bottom