CHADEMA imekuwa CCM, CCM imekuwa CHADEMA!

CHADEMA imekuwa CCM, CCM imekuwa CHADEMA!

Hizi ni hoja zinazotumiwa na wanasiasa ili waendeleze ulaghai wao kwa wananchi.

Siasa ina misingi ambayo ukiiacha inaondoa uhalali wako kama mwanasiasa kwa kile unachokisimamia.

Mwanasiasa kuwa kigeugeu ni kupoteza uhalali wa kuaminiwa
mbele ya jamii.

Chama hakiwezi kuwa na sera ya kubadili gia angani, halafu kipewe uhalali wa kuongoza nchi.!
 
CCM ndio imekuwa mtetezi wa wanyonge dhidi ya makabaila.
Tibaijuka wa ESCROW yuko CHADEMA?

Chenge aliyeihalifu katiba ya wananchi na kukwiba mabilioni ya ESCROW yuko CHADEMA?

Akina Ngeleja, Zitto na washiriki wengine wa ESCROW wako CHADEMA?

KIKWETE ambaye anatajwa kama mshiriki mkuu wa RICHMOND yuko CHADEMA?

hebu acheni kusumbua akili za wananchi! Kila mtu anafahamu, bila CCM hakuna UFISADI!

na mwaka huu lazima muondoke! Washenzi nyie!!!
 
Siasa haina adui wa kudumu wala haina rafiki wa kudumu.
Stukaaaaaa!!

kwenye msemo huo walimaanisha watu, sio sera! Sera zinabaki kama zilivyo, watu ndo hawana uadui au urafiki wa kudumu, walichofanya chadema ni kubadili hata sera zao!
 
CDM wanatetea ufisadi? Una wazimu sana wewe. CDM ndio inapinga ufisadi. Shida yenu ni maisha ya kukariri, Lowassa kawashika pabaya. Ufisadi haukemewi kwa mdomo.
Kama ningekuwa wazimu nadhani usingejisumbua kujenga hoja kwa wazimu!

Chadema ya miezi minne iliyopita ilikuwa inapinga ufisadi kwa maneno na vitendo.

Suala la Lowassa kutushika pabaya kama unavyojiaminisha linahusu nini katika hoja yangu hii? Ni watu nimetaja jina la Lowassa? Au ndiyo yale yale ya guilty conscience.
 
Kama wewe fisadi ukitaka uwe salama nenda Chadema, watakukodia na TV kukusafisha.!
Watakupa pia nafasi yoyote ya kiungozi ndani ya chama na kupitia chama. Wanasema, mtu yoyote akishakabidhiwa kadi ya uanachama anakuwa sawa na mwanachama yoyote. Ndiyo maana tumeona kuna baadhi ya watu wanapewa kadi leo na kesho wanateuliwa kuwa wagombea wa nafasi mbali mbali.

Haya ndiyo mabadiliko!
 
wtcoj.jpg


CDM-TV
Copyright 2010
Hii picha ndiyo inasadifu hoja yangu.
 
ccm ilitumia mbinu hizo ikashinda 2010,nao ukawa wanatumia mbinu hizo hizo kuona kama ni imara kwa ushindi
 
ccm ilitumia mbinu hizo ikashinda 2010,nao ukawa wanatumia mbinu hizo hizo kuona kama ni imara kwa ushindi

Very poor reasoning capacity, mkuu! 2010 CCM haikushinda urais kwa sababu ya campaign techniques bali kwa sababu ya incumbency. Unaelewa hata kidogo hili? Sidhani! So usitake kujitwisha kazi ya political strategist wakati hata basic concepts hujui!
 
njaa mbaya sasa, ewe lowassa njoo okoa kizazi hiki mana wanafanya si kwa mapenzi bali njaa
 
Na hivi sasa mkuu anajiandaa na trip ya US akirudi anakuta Magufuli amehamia Ukawa!
 
Chadema ya leo inapinga ufisadi? Chadema ya leo inasema ufisadi haukemewi kwa mdomo? Kwakwakwakwakwa
Huwezi kuamini kama hizi ni kauli za viongozi wa CHADEMA ambao miezi mitatu iliyopita walikuwa wanapiga kelele kwenye majukwaa ya nje na ndani kuhusu athari za ufisadi.
 
Hapa unadhibitisha bandiko kuwa ni ukweli mtupu.!
Huyu naamini hakuelewa mantiki ya thread. Hili siyo kosa lake pekee.

Wengi wa vijana wanaotetea CHADEMA ya sasa hawana fikra pana na mbaya zaidi, wanaanza kutoa comment kabla ya kusoma thread na kuielewa vizuri.
 
Tunaambiwa siasa zinabadilika (Political dynamics).

Mabadiliko ya siasa za Tanzania yanafanya watu wenye fikra pana wajiulize kuhusu hatima ya taifa na misingi ya vyama vya siasa.

Kwa kifupi, kile ambacho CHADEMA walikitetea, kwa sasa wanakipinga na kile ambacho CCM walikipinga kwa sasa wanakitetea!

Uchaguzi Mkuu uliopita, CCM walikuwa wanatetea sana ufisadi na mafisadi, kwa sasa kazi hiyo wameichukua CHADEMA.

Uchaguzi Mkuu uliopita, CCM ilikuwa inapinga sana midahalo ya wagombea Urais, kwa sasa kazi hiyo wameichukua CHADEMA.

Uchaguzi Mkuu uliopita, CCM walikuwa wanajitetea sana kuhusu uwezo wa mgombea Urais akiwa jukwaani, kwa sasa kazi hiyo wameichukua CHADEMA.

Uchaguzi Mkuu uliopita, CCM walidaiwa kuwa na wataalam wa kuiba kura, kwa sasa tunaambiwa CHADEMA pia wamesajiri watu wenye utaalamu wa kuiba kura.

Uchaguzi Mkuu uliopita, Mgombea Urais wa CCM alidaiwa ni mgonjwa baada ya kuanguka katika mkutano wa hadhara, kwa sasa CHADEMA wanadaiwa kuwa na mgombea Urais mgonjwa kutokana na afya yake kudhoofu ukilinganisha na miaka minane iliyopita.

Haya ndiyo mabadiliko ya siasa za Tanzania ambayo kwa sasa yanapigiwa upatu na vyama vya CCM na CHADEMA.

Kweli siasa ni mabadiliko!


Nazombi ndio waliwao
 
Tatizo la wanaccm ni kuishiwa sera na kukwama kwa kila proganda waliyodhani ingesambaratisha upinzani

ufisadi wa ccm uko pale pale wala ccm haipigi vita ufisadi maana wangeshawafikisha mahakamani wale wote waliohusika na escrow, epa,tembo,twiga nk lakini ndio wanaogombea

halafu makamba alisema lowassa alikuwa namba ya 9 kwenye list of shame inamaanisha ccm kuna 1-8
 
Back
Top Bottom