Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
View: https://www.youtube.com/live/wUVtQ2kDck8
Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara John Heche ni mgeni rasmi katika kongamano la wasomi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar Es Salaam.
Pamoja na mambo mengine ataeleza maazimio ya Kamati Kuu ya Chama kilichoketi kwa siku mbili Makao Makuu ya Chama tarehe 23 na 24 Mei 2025.
===
Katibu mkuu John Heche, amewataka wasomi wanaoiunga mkono CHADEMA kufuata misingi na falsafa za chama hiko. Amewataka wasome kitabu cha Intellectuals at the hill cha Prof Issa Shivji, cha pili ni Mr punch na cha tatu ni azimio linaloitwa Dar es salaam declaration on academic freedom and social responsibilities of academicians.
Makamu Mwenyekiti John Heche ameeleza kuwa kwa pamoja wameazimia kutofuata maagizo ya msajili wa vyama vya siasa kwa sababu yeye hana mamlaka hiyo ya kuwaingilia. Aidha ameeleza kuwa kwa anayelalamika ama kutoa malalamiko vipo vyombo ndani ya chama vya kujadili masuala hayo na hivo katibu mkuu ni yule yule aliyepitishwa.
Katika hatua nyingine Heche ameeleza kuwa kamati kuu imebariki kampeni ya No reforms No election kuendelea kuchanja mbuga katika Kanda sita.
Pia soma
- Pre GE2025 - DSM - Majibu ya CHADEMA kwa Msajili kuhusu malalamiko ya Lembrus Mchome ya Ukiukwaji wa Katiba
- Mchome amuomba Msajili kutengua maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA kwa kukiuka Katiba
- Msajili wa Vyama vya Siasa aipa wiki moja CHADEMA ijibu barua ya Mchome
- Barua ya CHADEMA ikimjibu Lembrus Mchome kuhusu malalamiko ya kupitishwa kwa viongozi kinyume na katiba ya chama